wa stendi
JF-Expert Member
- Jul 7, 2016
- 26,416
- 29,089
Siku moja nimetoka zangu tizi njiani kabla ya kufika sehemu yenye barabara pacha kuna daraja ukilivuka mbele hatua 5 ndio njia 4 yaani barabara kuna inayonyoosha kuna inaingia kushoto na kuna inaingia kulia,sasa nakumbuka katikati ya barabara inayoingia kulia na baada ya kuvuka daraja nilikuta mwanaume (kijana kama wa miaka 14 -17 amekalia limfuko).
Yule dogo alinisalimia na mimi nikaitika ile kama naanza kumpita hivi akaniambia "samahani kaka naomba unitwike huu mzigo"mimi nikageuka na yeye akasimama na kuinama kama anaubeba na mimi nikainama kumsaidia ile kuubeba na kwa kweli ilikuwa kitu kizito kiasi kwamba nilijikuta nimeguna nikamuuliza "mbona mzigo mzito sana huu umetoka nao wapi na unapeleka hadi wapi? yeye aliishia kusema asante nashukuru. Mimi nikamwambia utafikisha huo mzigo? Hakunijibu kitu akawa ndo anapiga hatua kama anaenda na mimi nikageukia upande wangu naanza kwenda.
Ile nimepiga hatua mbili bado nikaw najiuliza kimoyomoyo 'huyu dogo huu mzigo kweli huyo aliembebesha huko atakuwa ana roho mbaya sana mzigo mzito kiasi kile anambebesha mtoto?basi wakati najiuliza maswali nikageuza shingo nimwangalie,la hau laa sikuamini mamcho yangu pamoja na eneo lile kuwa wazi sikuambulia kumwóna narudi nyuma kama hatua 3 hivi kutizama vizuri sikumwona nimeenda kuchungulia adi kule darajani labda ameend kutumbukia huko sikuambulia kitu zaidi ya mimi kujisikia kutoka jasho na hofu huku woga umenitanda na miguu kukosa nguvu.
Nilisali sala pale pale huku nakemia na kuondoka nafika nyumbani sielewi ingekuwaje.
Basi mpaka leo nikipita lile eneo hata kama niko na gari bado napatwa na woga sana.
Onyo:kama ukikutana na mtu mazingira ambayo hayaeleweki hata akikusemesha plies usijisumbue kumjibu wee pita tuu.
Yule dogo alinisalimia na mimi nikaitika ile kama naanza kumpita hivi akaniambia "samahani kaka naomba unitwike huu mzigo"mimi nikageuka na yeye akasimama na kuinama kama anaubeba na mimi nikainama kumsaidia ile kuubeba na kwa kweli ilikuwa kitu kizito kiasi kwamba nilijikuta nimeguna nikamuuliza "mbona mzigo mzito sana huu umetoka nao wapi na unapeleka hadi wapi? yeye aliishia kusema asante nashukuru. Mimi nikamwambia utafikisha huo mzigo? Hakunijibu kitu akawa ndo anapiga hatua kama anaenda na mimi nikageukia upande wangu naanza kwenda.
Ile nimepiga hatua mbili bado nikaw najiuliza kimoyomoyo 'huyu dogo huu mzigo kweli huyo aliembebesha huko atakuwa ana roho mbaya sana mzigo mzito kiasi kile anambebesha mtoto?basi wakati najiuliza maswali nikageuza shingo nimwangalie,la hau laa sikuamini mamcho yangu pamoja na eneo lile kuwa wazi sikuambulia kumwóna narudi nyuma kama hatua 3 hivi kutizama vizuri sikumwona nimeenda kuchungulia adi kule darajani labda ameend kutumbukia huko sikuambulia kitu zaidi ya mimi kujisikia kutoka jasho na hofu huku woga umenitanda na miguu kukosa nguvu.
Nilisali sala pale pale huku nakemia na kuondoka nafika nyumbani sielewi ingekuwaje.
Basi mpaka leo nikipita lile eneo hata kama niko na gari bado napatwa na woga sana.
Onyo:kama ukikutana na mtu mazingira ambayo hayaeleweki hata akikusemesha plies usijisumbue kumjibu wee pita tuu.