Nahisi nilitwika jini mzigo

Nahisi nilitwika jini mzigo

wa stendi

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2016
Posts
26,449
Reaction score
29,139
Siku moja nimetoka zangu tizi njiani kabla ya kufika sehemu yenye barabara pacha kuna daraja ukilivuka mbele hatua 5 ndio njia 4 yaani barabara kuna inayonyoosha kuna inaingia kushoto na kuna inaingia kulia,sasa nakumbuka katikati ya barabara inayoingia kulia na baada ya kuvuka daraja nilikuta mwanaume (kijana kama wa miaka 14 -17 amekalia limfuko).

Yule dogo alinisalimia na mimi nikaitika ile kama naanza kumpita hivi akaniambia "samahani kaka naomba unitwike huu mzigo"mimi nikageuka na yeye akasimama na kuinama kama anaubeba na mimi nikainama kumsaidia ile kuubeba na kwa kweli ilikuwa kitu kizito kiasi kwamba nilijikuta nimeguna nikamuuliza "mbona mzigo mzito sana huu umetoka nao wapi na unapeleka hadi wapi? yeye aliishia kusema asante nashukuru. Mimi nikamwambia utafikisha huo mzigo? Hakunijibu kitu akawa ndo anapiga hatua kama anaenda na mimi nikageukia upande wangu naanza kwenda.

Ile nimepiga hatua mbili bado nikaw najiuliza kimoyomoyo 'huyu dogo huu mzigo kweli huyo aliembebesha huko atakuwa ana roho mbaya sana mzigo mzito kiasi kile anambebesha mtoto?basi wakati najiuliza maswali nikageuza shingo nimwangalie,la hau laa sikuamini mamcho yangu pamoja na eneo lile kuwa wazi sikuambulia kumwóna narudi nyuma kama hatua 3 hivi kutizama vizuri sikumwona nimeenda kuchungulia adi kule darajani labda ameend kutumbukia huko sikuambulia kitu zaidi ya mimi kujisikia kutoka jasho na hofu huku woga umenitanda na miguu kukosa nguvu.

Nilisali sala pale pale huku nakemia na kuondoka nafika nyumbani sielewi ingekuwaje.
Basi mpaka leo nikipita lile eneo hata kama niko na gari bado napatwa na woga sana.
Onyo:kama ukikutana na mtu mazingira ambayo hayaeleweki hata akikusemesha plies usijisumbue kumjibu wee pita tuu.
 
Siku moja nimetoka zangu tizi njiani kabla ya kufika sehemu yenye barabara pacha kuna daraja ukilivuka mbele hatua 5 ndio njia 4 yaani barabara kuna inayonyoosha kuna inaingia kushoto na kuna inaingia kulia,sasa nakumbuka katikati ya barabara inayoingia kulia na baada ya kuvuka daraja nilikuta mwanaume (kijana kama wa miaka 14 -17 amekalia limfuko).

Yule dogo alinisalimia na mimi nikaitika ile kama naanza kumpita hivi akaniambia "samahani kaka naomba unitwike huu mzigo"mimi nikageuka na yeye akasimama na kuinama kama anaubeba na mimi nikainama kumsaidia ile kuubeba na kwa kweli ilikuwa kitu kizito kiasi kwamba nilijikuta nimeguna nikamuuliza "mbona mzigo mzito sana huu umetoka nao wapi na unapeleka hadi wapi? yeye aliishia kusema asante nashukuru. Mimi nikamwambia utafikisha huo mzigo? Hakunijibu kitu akawa ndo anapiga hatua kama anaenda na mimi nikageukia upande wangu naanza kwenda.

Ile nimepiga hatua mbili bado nikaw najiuliza kimoyomoyo 'huyu dogo huu mzigo kweli huyo aliembebesha huko atakuwa ana roho mbaya sana mzigo mzito kiasi kile anambebesha mtoto?basi wakati najiuliza maswali nikageuza shingo nimwangalie,la hau laa sikuamini mamcho yangu pamoja na eneo lile kuwa wazi sikuambulia kumwóna narudi nyuma kama hatua 3 hivi kutizama vizuri sikumwona nimeenda kuchungulia adi kule darajani labda ameend kutumbukia huko sikuambulia kitu zaidi ya mimi kujisikia kutoka jasho na hofu huku woga umenitanda na miguu kukosa nguvu.

Nilisali sala pale pale huku nakemia na kuondoka nafika nyumbani sielewi ingekuwaje.
Basi mpaka leo nikipita lile eneo hata kama niko na gari bado napatwa na woga sana.
Onyo:kama ukikutana na mtu mazingira ambayo hayaeleweki hata akikusemesha plies usijisumbue kumjibu wee pita tuu.
Unaogopa nini?
Kwa jinsi tulivyoumbwa na Mungu, binadamu tumewezeshwa kuwa na nguvu ya kiroho kuliko majini.
Ni kuihuisha tu imani yako.
Waefeso 6, 11-12.
11 Vaeni silaha zote za Mungu ili mpate kusimama na kupin gana na hila zote za shetani.
12 Kwa maana hatupambani na bina damu, bali tunapambana na tawala na mamlaka na nguvu za ulimwengu huu wa giza na majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.

Mwanzo 2:7
7. Basi, Mwenyezi-Mungu akamfanya mwanamume kwa mavumbi ya udongo, akampulizia puani pumzi ya uhai, na huyo mwanamume akawa kiumbe hai.

Ndugu yangu wa stendi, ukimuinua Mungu maishani mwako hakuna jini, pepo au kibwengo kitakuchezea.
 
Ulikosea kumchungulia darajani...ilibidi pale pale ulipomuona na ule mzigo upachimbe kwani kuna uwezekano mkubwa huyo dogo alizama kwenye mchanga kutokana na uzito wa ule mzigo.
 
Ndio lakini bado hofu ipo
Pole Mkuu lakini ukijua kuwa una nguvu moyoni kuliko hivyo viumbe, haikusumbui.
Mim yaliwahi kunikuta, tena mabaya zaidi.
Nilitembelewa na lijipaka la kutisha zaidi ya mara tatu, usiku wa manane.
Hata lilikopitia sijui.
Sikuwa na hofu hata kidogo, na naomba unielewe, sijitambi ukamilifu wa imani.

Mara ya tatu, nikaamua tupambane physically lile lijipaka.
Tuliwindana chumbani kwa robo saa kisha nikalipiga na kuliua, na kulitupa nje.

Kesho yake asubuhi sikuona mzoga wake, nilishangaa sana.
Hata hivyo siku chache baadaye tukapata msiba mkubwa wa jirani yetu bibi mzee.
Mpaka leo sijaweza kuunganisha matukio hayo mawili, lakini sikusumbuliwa tena.
 
Pole Mkuu lakini ukijua kuwa una nguvu moyoni kuliko hivyo viumbe, haikusumbui.
Mim yaliwahi kunikuta, tena mabaya zaidi.
Nilitem elewa na lijipaka la kutisha zaidi ya mara tatu, usiku wa manane.
Hata lilikopitia sijui.
Sikuwa na hofu hata kidogo, na naomba unielewe, sijitambi ukamilifu wa imani.
Mara ya tatu, nikaamua tupambane physically lile lijipaka.
Tuliwindana chumbani kwa robo saa kisha nikalipiga na kuliua, na kulitupa nje.

Kesho yake asubuhi sikuona mzoga wake, nilishangaa sana.
Hata hivyo siku chache baadaye tukapata msiba mkubwa wa jirani yetu bibi mzee.
Mpaka leo sijaweza kuunganisha matukio hayo mawili, lakini sikusumbuliwa tena.
Duu.
Pole sana
 
Wa stendi unahofu na mzigo mzito au kutoonekana kwa uyo dogo?baada ya kumtwisha wala nisingemchunguza,mda mchache mambo mengi. Ndio yaliyo mkuta lutu hayo,usingegeuka usingekuw na muweweseko.Alafu gentleman unakuwaje muoga wa vitu vidogo Kama mtoto wa kota bana
 
Siku moja nimetoka zangu tizi njiani kabla ya kufika sehemu yenye barabara pacha kuna daraja ukilivuka mbele hatua 5 ndio njia 4 yaani barabara kuna inayonyoosha kuna inaingia kushoto na kuna inaingia kulia,sasa nakumbuka katikati ya barabara inayoingia kulia na baada ya kuvuka daraja nilikuta mwanaume (kijana kama wa miaka 14 -17 amekalia limfuko).

Yule dogo alinisalimia na mimi nikaitika ile kama naanza kumpita hivi akaniambia "samahani kaka naomba unitwike huu mzigo"mimi nikageuka na yeye akasimama na kuinama kama anaubeba na mimi nikainama kumsaidia ile kuubeba na kwa kweli ilikuwa kitu kizito kiasi kwamba nilijikuta nimeguna nikamuuliza "mbona mzigo mzito sana huu umetoka nao wapi na unapeleka hadi wapi? yeye aliishia kusema asante nashukuru. Mimi nikamwambia utafikisha huo mzigo? Hakunijibu kitu akawa ndo anapiga hatua kama anaenda na mimi nikageukia upande wangu naanza kwenda.

Ile nimepiga hatua mbili bado nikaw najiuliza kimoyomoyo 'huyu dogo huu mzigo kweli huyo aliembebesha huko atakuwa ana roho mbaya sana mzigo mzito kiasi kile anambebesha mtoto?basi wakati najiuliza maswali nikageuza shingo nimwangalie,la hau laa sikuamini mamcho yangu pamoja na eneo lile kuwa wazi sikuambulia kumwóna narudi nyuma kama hatua 3 hivi kutizama vizuri sikumwona nimeenda kuchungulia adi kule darajani labda ameend kutumbukia huko sikuambulia kitu zaidi ya mimi kujisikia kutoka jasho na hofu huku woga umenitanda na miguu kukosa nguvu.

Nilisali sala pale pale huku nakemia na kuondoka nafika nyumbani sielewi ingekuwaje.
Basi mpaka leo nikipita lile eneo hata kama niko na gari bado napatwa na woga sana.
Onyo:kama ukikutana na mtu mazingira ambayo hayaeleweki hata akikusemesha plies usijisumbue kumjibu wee pita tuu.
Watanzania wengi hasa wenye hizi Imani za Kiroho hatuna tatizo la Pepo au Mapepo, ila wengi Wetu tumeathirika zaidi Kisaikolojia na Maisha tu.
 
Back
Top Bottom