Nahisi naibiwa ,naombeni ushauri

yenyewe

JF-Expert Member
Joined
Feb 1, 2014
Posts
621
Reaction score
94
Hbr wakuu?

Siku moja nilichukua simu ya mpenzi wangu nikakuta mesegi alizokua anachat na jamaa, alikua akimwita mpenzi na majina mengne yalonipa mashaka.

Niliongea na mpenzi wangu akakataa na kusema jamaa ni rafiki ake tu eti wamezoea kuchat vile, pia marafik zake walimtetea sana.

Sikuridhishwa na majibu yale ikabidi nimwambie amwite jamaa, alivyokuja akaeleza kuwa ni marafiki tu na akaomba msamaha kuwa hatorudia, nilimwambia amkome mpnz wng.

Kinachoniumiza zaid hivi karbuni ameanza kumtag mpenzi wangu kila picha anayoeka fb, nimeumia zaidi alipoeka picha ya maandishi iliyoandikwa LINI UTAKUWA WANGU na kumtag mpenzi wangu na dada mwingne.

Napoongea na mpenzi wangu anaomba sana msamaha na kusema atamzuia jamaa hiyo tabia.

Mi sielewi la kufanya ndugu zangu na huyu nampenda sana, naombeni ushauri.

Ahsanteni.
 
Mimi sitaki presha simu ya mama Ngina ni yake mie siigusi na simu yangu ni yang mama Ngina haigusi, kwanini
 
Hivi bado tu kuna watu wanawivu wa mapenzi? Siku hizi mpenzi ni wako pale unapokuwa naye tu, mkiachana tu, ni mpenzi wa mwingine.
 
Kama unadhani huwezi kuhimili maumivu ya moyo acha kuangalia simu ya mpenzi wako.
 

Ongeza mapigo kwenye 6x6 atatulia !
Au achana nae haraka !
 
Ukweli mtupu!!!! Halaf mtamuuuuuuuuu!!!

From A to Z????
"a"="b"
"b"="c"
"c" is a number
"a" must be a number
 
Sa kumpenda kwako kunakusaidia nini we mbulula? huyu dem wako ka ni kicheche si umpige chini tu, la sivyo uendelee kumpenda na jamaa aendelee kukugegedea
 
Unashindanishwa wewe.

Chagua kuwa mshindani au nawe mshindanishe pia.

Shtuka mapema kabla hujaanza kujiliza kama mtoto mdogo!
 
Nikitumia JF posts kama sample, asilimia kubwa ya matatizo ya kimapenzi siku hizi yanaanzia kwenye simu. Na asilimia kubwa yanakuja pale mmoja anapojipa jukumu la kupekua simu ya mwenzie...

Conclusion: Nitaendelea kuiona simu ya mke wangu kama BOMU... sigusi...
 
Ukiona manyoya ujuwe keshaliwa huyo!

By the way, kama jamaa anauliza kwenye face book LINI UTAKUWA WANGU?- Pengine jamaa anaendelea kuimbisha bado hajapewa mambo!
KITU KIMOJA CHA KUFAHAMU NDUGU YANGU NI KWAMBA WANAWAKE HUTONGOZWA DAILY, KWA HIYO INAKUBIDI UKUBALI REALITY TU, HUWEZI KUMZUIA DEMU/MKE WAKO KUTONGOZWA, CHA MSINGI NI WEWE UIMERGE KAMA THE WINNER ALL THE TIME, KWA HIYO FANYA THE NECESSARY ILI UIBUKE KIDEDEA SIKU ZOTE
 
Nadhani hii ni ndoa ya watoto wadogo...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…