Nafikiria Kugombea Urais Naomba Ushauri Wenu

Nafikiria Kugombea Urais Naomba Ushauri Wenu

peche luke

JF-Expert Member
Joined
Sep 8, 2013
Posts
365
Reaction score
106
Ninataka kugombea urais, ila kuna jambo naona linanipa taabu kufikia uamuzi wangu wa mwisho.

Jambo lenyewe ni haya maoni ya wananchi waliyoyatoa kwenye rasimu ya katiba yaani tuwe na serikali tatu.

Najiuliza nigombee urais wa nchi ya JMT, ZNZ au Tanganyika.

Ni urais upi kati ya hizo utanipa changamoto na heshima zaidi katika kuwatumikia wananchi wangu.
 
Chagua mwenyewe, ila usinisahau kwenye ufalme wako utakapochaguliwa!
 
raisi atakuwa mmoja tu (yaani raisi wa JMT), Hao wengine watakuwa na cheo cha ugavana.
 
raisi atakuwa mmoja tu (yaani raisi wa JMT), Hao wengine watakuwa na cheo cha ugavana.

Kuna wakati na mimi nililiona hili, lakini nikajiuliza hivi huyu wa JMT vyanzo vyake vya mapato atakuwa anategemea wapi?
 
Gombea urais wa jamhuri ya JMT kwani utakuwa rais wa marais 2 hivyo nchi zote 2 zitakuwa chini yako.Wachakarikaji watakuwa ni marais wawili waliyoko chini yako ambao watakuwa wanakusanya mapato kutoka kwenye vyanzo vya nchi zao na wewe watakuwa wanakuheshimu na kukuletea mapato kama nyuki na mchwa wafanyavyo kwa malkiya wao.
 
Gombea urais wa JMT ili uweze kuona Nchi nyingi za nje na uhondo wa kupaa angani,vinginevyo utaishia TARIME,MTWARA,RUKWA,ARUSHA,DODOMA na sana DSM,Huoni wenzako wanavyoruka juu kila kukicha? kupanga ni kuchagua but better u compete for JMT..
 
Back
Top Bottom