Nafikiri binadamu alitoka hapa...!

Umeleta mda muzuri na ukatuaminisha kwamba wewe ni mfikiriaji huru,sasa umeanza kutuaminisha tofauti.

Uwezo wa mtu kufikiroa unaongezeka siku hadi siku na kizazi hadi kizazi,hilo nalo kweli ni fumbo!%-%
Hakika mkuu, naamini hivyo, uwezo wa mtu kupambanua mambo huongezeka siku baada ya siku kulingana na mazingira. Naamini hata kwa hizi fikira zangu huru umeshaanza kufikiria tofauti kichwan mwako tofauti na ilivyokuwa jana au juzi.
 
Kwanza katika solar yetu hakuna penye visible viumbe kama Earth may be invisible, Ulimwengu ni mpana mno mno kuamini kuwa tupo wenyewe ni Ngumu sana hio theory ya uhai kuletwa na viumbe wa anga za mbali ipo tayari japo sio proved ila ina mantiki sana ukisoma mkuu
 
....alidhaniae mjinga ndilo linalomtokea....kwani hujui babu na bibi yetu Adam na Hawa walifurushwa kutoka Bustani ya Eden (katika sayari nyingine) nao ndio ukawa mwanzo wa sisi hapa Duniani....sio swali la kuumiza kichwa...ni kweli kuna viumbe wengine katika baadhi ya sayari...mfano malaika na majini...(kwa mujibu wa VITABU vitukufu) na ipo ahadi toka kwa Mungu mwenyezi kuwa ipo siku tutakufa wote na kufufuka tukiwa na njia moja tu kuielekea sayari ya ahadi nayo ndio ya MILELE...huko ni kula raha tu mwanzo mwisho....N.B kwa wale wanaofuata maagizo yake hapa Duniani...
 
Kila kitu mara wanasayansi wamefanya mara wamesema,hatujui la ukweli lipi wala la uongo lipi.
 
Mkuu Sote tunatambua hakukuna sayari 9 ulimwenguni alafu inajulikana kwamba kuna sayari zaidi ya 9 ulimwenguni
 
Kuna move moja nimeangalia inaitwa the 100.
(The hundred)
Inafanana sana na hichi unachotaka kutuaminisha mkuu.
Hiyo niliona ila nikawa kama sijaipenda ila hembu nipe intro kidogo nishawishike mkuu.....
 
Wakati mwingine jambo likiwa gumu sana kwa level ya akili za kibinadamu ni ushahidi wa uwepo wa nguvu kubwa zaidi inapoanzia... yaweza kuwa mungu au mfano wako
 
Hebu iweke hapa ili tuisome hiyo theory kama hautajali mkuu.
 
Wakati mwingine jambo likiwa gumu sana kwa level ya akili za kibinadamu ni ushahidi wa uwepo wa nguvu kubwa zaidi inapoanzia... yaweza kuwa mungu au mfano wako
Unamaanisha nn mkuu
 
Kwasababu hatujui maisha baada ya kifo inakuwaje nahisi wafu ndio wanaludi kwenye hizo sayari kuendelea na maisha mengine ni kama style ya wadudu kubadilika
 

Mkuu umefikiri sawa, ila fikira zako zimekaa katika hali ya kujipendelea sisi binadamu kwa vile tuna uwezo wa kufikiri tofauti na wanyama wenzetu kama ng'ombe, mbuzi nk.
Tujiulize, kama sisi tutakuwa tumeletwa toka sayari nyingine, je hawa wanyama wengine pamoja na viumbe wote ikiwemo mimea ambavyo tunashirikiana uhai, navyo vitakuwa vimeletwa pia?

Ninajua wote tuna imani zetu, ila tukiziweka kando na kuruhusu akili kufikiri tofauti unaweza kuyaona maisha katika "Angle" nyingine na ukajifunza kitu.
Dunia tunayoishi ina umri wa miaka mingi, katika umri huo kuna aina tofauti ya viumbe walioishi hapa(mf.Mijusi wakubwa-Dinosaurs) na kutoweka kabisa kutokana na mabadiliko ya hali katika dunia yenyewe.
Kwa mantiki hiyo, kuishi au kuwepo kwa kiumbe yoyote hapa duniani inategemea na hali ya dunia ukilinganisha na uhitaji wa kiumbe husika. (Mfano. Kama kiumbe kinahitaji baridi dunia ikawa ya joto basi, kiumbe ni lazima kitoweke).
Kwa maana uwepo wetu kwa wakati huu katika hii dunia, unatokana na hali na mazingira ya dunia kwa kipindi hiki yameruhusu.(Mahitaji yetu kama viumbe wa aina tuliyopo yanaendana na hali ya dunia ilivyo kwa sasa).
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…