Yo Yo
JF-Expert Member
- May 31, 2008
- 11,217
- 1,706
Wakuu joining the army is serious business i hope you know that part of the application is the signing of your death bond, you can die in training or loose some vital part.
source: tpdf (dot) go (dot) tz
Good luckUANDIKISHWAJI
Askari
Mtu yeyote ataandikishwa kujiunga na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kwa sifa zifuatazo: -
· Awe raia wa Tanzania
· Awe na Elimu ya kidato cha nne na kuendelea na awe amefaulu..
· Awe hajaoa/hajaolewa
· Awe na umri kuanzia miaka 18 hadi 25
· Awe na tabia na mwenendo mzuri
· Awe na akili timamu na afya nzuri
Masharti ya Utumishi
· Askari atapewa nambari ya utumishi baada ya kufaulu mafunzo ya awali.
· Atalitumikia Jeshi kwa kipindi cha mwanzo cha miaka sita, baada ya hapo atafanya kazi kwa mkataba wa miaka miwili miwili kwa kibali cha Mkuu wa Majeshi.
Maafisa
· Bodi ya Uteuzi wa Maafisa (Officers Selection Board)
huwafanyia usaili askari wenye elimu ya kidato cha sita na kuendelea toka Vikosini na Shule za askari wapya (Recruitment Schools).
· Watakaofaulu masailiano hayo hupewa hadhi ya Afisa Mwanafunzi (Officer Cadet), na hupelekwa Chuoni (Tanzania Military Academy) kwa mafunzo ya uafisa kwa muda wa mwaka mmoja.
source: tpdf (dot) go (dot) tz