Naendelea kuamini kuwa Mungu hasemi uongo. Alisema ukiibariki Israeli, utabarikiwa. Ukiilaani, utalaaniwa. Ushahidi huu hapa

Naendelea kuamini kuwa Mungu hasemi uongo. Alisema ukiibariki Israeli, utabarikiwa. Ukiilaani, utalaaniwa. Ushahidi huu hapa

Setfree

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2024
Posts
5,527
Reaction score
7,121
Mungu alimwahidi Ibrahimu akisema: “Nitawabariki wakubarikio, na atakayekulaani nitamlaani” (Mwanzo 12:3). Kauli hii haikubaki historia tu, inajidhihirisha mpaka leo kwa mataifa na watu binafsi.

Marekani ni mfano wa taifa la watu waliobarikiwa kwa sababu wanaiunga mkono Israeli. Tangu kuanzishwa kwa Taifa la Israeli mwaka 1948, Marekani imekuwa mshirika wake mkuu. Matokeo yake, Marekani ni taifa lililoinuka kiuchumi, kiteknolojia, na kijeshi kuliko mataifa mengi. Hata pale changamoto zinapokuja, bado Marekani imeendelea kuwa na nguvu kubwa katika dunia. Hii ni ishara ya wazi kuwa Neno la Mungu ni kweli na halibadiliki.

Mataifa yaliyoishambulia Israeli mwaka 1967 wakati wa Vita vya Siku Sita ni mfano mzuri wa madhara ya kuilaani au kuipinga Israeli. Katika vita hivyo, Israeli ilishinda majeshi ya nchi nyingi kwa siku chache tu, na hadi leo mataifa hayo bado yanahangaika kisiasa na kiuchumi. Mashirika na viongozi wa kigaidi wanapata uharibifu mkubwa, kila mara wanapoinua mikono yao dhidi ya Israeli. Badala ya mafanikio, wamekuwa wakipata maangamizi na kupoteza uhalali mbele ya dunia.

Wakristo wa mataifa mbalimbali, wale wanaoomba kwa ajili ya Yerusalemu na kuiunga mkono Israeli mara nyingi hushuhudia baraka binafsi: maendeleo, mafanikio ya huduma, na ulinzi wa ajabu wa Mungu. Ndio sababu, wengine hata katika ofisi zao, wanaweka bendera ya Israeli, kuonesha kuwa wanaibariki nchi hiyo.

I bless Israel.jpg
 
Ndugu zangu, tujihadhari tusiitamkie mabaya Israeli. Hilo ni taifa teule la Mungu. Ndio sababu linaendelea kubarikiwa kama jinsi Mungu alivyoahidi.(Mwanzo 12:2-3)

Habari za hivi punde kutoka katika taifa hilo zinasema, Israel imefanikiwa kurusha satelaiti mpya ya kijasusi angani, hatua ambayo itaimarisha kwa kiwango kikubwa uwezo wake wa upelelezi katika eneo la Mashariki ya Kati. Kwa mujibu wa maafisa wa Israel, satelaiti hii inaweza kupiga picha za vitu vidogo hadi ukubwa wa sentimita 50, mchana na usiku.

Waziri wa Ulinzi wa Israel, Israel Katz, amesema uzinduzi wa satelaiti hiyo, iliyopewa jina la "Horizon 19," ni ujumbe wa moja kwa moja kwa maadui kwamba "tunawaangalia kila wakati na katika hali zote."
Source: BBC
 
✝️✝️✝️✝️✝️✝️✝️✝️✝️
🇮🇱🇮🇱🇮🇱🇮🇱🇮🇱🇮🇱🇮🇱🇮🇱🇮🇱
 
Marekani ni mfano wa taifa la watu waliobarikiwa kwa sababu wanaiunga mkono Israeli.
Imebarikiwa kivipi wakati vita kuu ya pili iliikuta marekani imeshakua super power!! Unaijua Marshall plan wewe? Little boy na Fatman? Zote hizo zinaonyesha USA alishakua advanced kabla hata Israel haijaundwa. Tokea hapo USA imekua ikipata utajiri kupitia kuanzisha vita holela, kupora rasilimali, kufadhili ugaidi na mapinduzi n.k sasa kama Mungu anabariki taifa litahitaji kweli kutumia mbinu za kimafia kupata utajiri?
 
Mataifa yaliyoishambulia Israeli mwaka 1967 wakati wa Vita vya Siku Sita ni mfano mzuri wa madhara ya kuilaani au kuipinga Israeli
Upotoshaji nchi kibao zilizounga mkono vita ile kama Saudia mbona ni matajiri wa mafuta leo hii? Qatar inaingiza mabilioni ya gesi, Libya iliilaani Israel ila ilikua tajiri mkubwa wa mafuta mpaka ilipokuja kuvamiwa na wazungu!! So sio kweli kuwa walioilaani basi ndio wamepotea otherwise middle east ingejaa nchi maskini tu!!
 
Wakristo wa mataifa mbalimbali, wale wanaoomba kwa ajili ya Yerusalemu na kuiunga mkono Israeli mara nyingi hushuhudia baraka binafsi
Gwajima anaiombeaga kila jumapili vipi mbona kanisa lake limefungiwa na hatujaona chochote kimetokea? Same to Ruto ni pro israel mbona nchi imemshinda na imejaa mikosi tu?
 
Habari za hivi punde kutoka katika taifa hilo zinasema, Israel imefanikiwa kurusha satelaiti mpya ya kijasusi angani, hatua ambayo itaimarisha kwa kiwango kikubwa uwezo wake wa upelelezi katika eneo la Mashariki ya Kati. Kwa mujibu wa maafisa wa Israel, satelaiti hii inaweza kupiga picha za vitu vidogo hadi ukubwa wa sentimita 50, mchana na usiku.
Waambie wazitumie kutafuta mateka!! Maana mwanawasifia kwa ujasusi ilihali kuokoa tu mateka kwenye kaeneo kama mbagala imewashinda.
 
Mungu alimwahidi Ibrahimu akisema: “Nitawabariki wakubarikio, na atakayekulaani nitamlaani” (Mwanzo 12:3). Kauli hii haikubaki historia tu, inajidhihirisha mpaka leo kwa mataifa na watu binafsi.

Marekani ni mfano wa taifa la watu waliobarikiwa kwa sababu wanaiunga mkono Israeli. Tangu kuanzishwa kwa Taifa la Israeli mwaka 1948, Marekani imekuwa mshirika wake mkuu. Matokeo yake, Marekani ni taifa lililoinuka kiuchumi, kiteknolojia, na kijeshi kuliko mataifa mengi. Hata pale changamoto zinapokuja, bado Marekani imeendelea kuwa na nguvu kubwa katika dunia. Hii ni ishara ya wazi kuwa Neno la Mungu ni kweli na halibadiliki.

Mataifa yaliyoishambulia Israeli mwaka 1967 wakati wa Vita vya Siku Sita ni mfano mzuri wa madhara ya kuilaani au kuipinga Israeli. Katika vita hivyo, Israeli ilishinda majeshi ya nchi nyingi kwa siku chache tu, na hadi leo mataifa hayo bado yanahangaika kisiasa na kiuchumi. Mashirika na viongozi wa kigaidi wanapata uharibifu mkubwa, kila mara wanapoinua mikono yao dhidi ya Israeli. Badala ya mafanikio, wamekuwa wakipata maangamizi na kupoteza uhalali mbele ya dunia.

Wakristo wa mataifa mbalimbali, wale wanaoomba kwa ajili ya Yerusalemu na kuiunga mkono Israeli mara nyingi hushuhudia baraka binafsi: maendeleo, mafanikio ya huduma, na ulinzi wa ajabu wa Mungu. Ndio sababu, wengine hata katika ofisi zao, wanaweka bendera ya Israeli, kuonesha kuwa wanaibariki nchi hiyo.

View attachment 3465015
Asee, kuna watu wako serious na mambo ya Mungu. Huyo sijui ni meneja, ameweka mpaka bendera ya Israel ofisini?
 
Ukondoo tabu sana , Ina maana hata wawe mashoga , madhalimu , waasherati unapaswa uwafuate tu na kuwasifi kisa Wa Israeli ?

Hata Qu'ran imewasifu Wana Israel wale walikuwa wachaMungu na hizo sifa njema na Baraka ukisifiwa ni conditional na sio automatically ..kwa maana wakiwa katika Misingi ya Wema wanaingia katika kundi Hilo na wakiwa waovu wanajivua katika kundi la waliobarikiwa na watu WEMA .

It's insanity kudai kuwa mtu hizo baraka ni kwenye DNA wakati tunashudia wakifanya maovu mengi wakienda kinyume na Taurati na kuruhusu mambo mengi ya hovyo.
 
Mungu alimwahidi Ibrahimu akisema: “Nitawabariki wakubarikio, na atakayekulaani nitamlaani” (Mwanzo 12:3). Kauli hii haikubaki historia tu, inajidhihirisha mpaka leo kwa mataifa na watu binafsi.

Marekani ni mfano wa taifa la watu waliobarikiwa kwa sababu wanaiunga mkono Israeli. Tangu kuanzishwa kwa Taifa la Israeli mwaka 1948, Marekani imekuwa mshirika wake mkuu. Matokeo yake, Marekani ni taifa lililoinuka kiuchumi, kiteknolojia, na kijeshi kuliko mataifa mengi. Hata pale changamoto zinapokuja, bado Marekani imeendelea kuwa na nguvu kubwa katika dunia. Hii ni ishara ya wazi kuwa Neno la Mungu ni kweli na halibadiliki.

Mataifa yaliyoishambulia Israeli mwaka 1967 wakati wa Vita vya Siku Sita ni mfano mzuri wa madhara ya kuilaani au kuipinga Israeli. Katika vita hivyo, Israeli ilishinda majeshi ya nchi nyingi kwa siku chache tu, na hadi leo mataifa hayo bado yanahangaika kisiasa na kiuchumi. Mashirika na viongozi wa kigaidi wanapata uharibifu mkubwa, kila mara wanapoinua mikono yao dhidi ya Israeli. Badala ya mafanikio, wamekuwa wakipata maangamizi na kupoteza uhalali mbele ya dunia.

Wakristo wa mataifa mbalimbali, wale wanaoomba kwa ajili ya Yerusalemu na kuiunga mkono Israeli mara nyingi hushuhudia baraka binafsi: maendeleo, mafanikio ya huduma, na ulinzi wa ajabu wa Mungu. Ndio sababu, wengine hata katika ofisi zao, wanaweka bendera ya Israeli, kuonesha kuwa wanaibariki nchi hiyo.

View attachment 3465015
Acha kujikomba. Israel yako ina baraka gani zaidi ya laana tupu? Nawe ulaaniwe kama Israel yako nyambaff
 
Tatizo sio kubariki israel!Tatizo ni kujua kama Hilo taifa mnaloliita la israel he ni lenyewe!!?

Kwa maana waisrael wa Leo wanaotambulika ni jamii ya watu weupe hao tunawaona leo!!

Sasa,tatizo ni kwamba:-

"Mimi ni mweusi mweusi lakini ni mzuri enyi mabinti wa misri" huyu ni mfalme Suleiman akisisitiza katika kitabu Cha wimbo ulio Bora!

Pia
"Ngozi yangu ni nyeusi nayo yanitoka" Ayubu akiomboleza akiwa naumwa sana Hadi ngozi inababuka kama mtu alieungua,anasisitiza ye ni mweusi lakini ngozi inamtoka na kuleta wekundu au weupe!kwenye kitabu Cha Ayubu!!

Sasa Leo waisrael weusi wako wapi!!?mbona hao wote ni weupe!!?

Hata jamii ya waebrania wa kale walifanana na wamisri Kwa weusi wao Hadi Abdul naser mfalme wa misri alipoambiwa alitambue taifa la Israel la sasa aligoma na kusema "mbona alitoka hapa misri utumwani weusi imekuaje wamukua weupe!!?aligoma kutambua israel ya sasa!!

Turudi kwenye misingi!

KAZI na utu,tunasonga mbele!!
 
Back
Top Bottom