Nadhani serikali haiwezi kuwa na hoja ya kutorushwa matangazo ya live ya TBC

mpk

JF-Expert Member
Sep 26, 2012
3,115
3,862
Tulihoji rais aliporusha matangazo live siku ya sheria dunian tukaambiwa Tv zilijitolea. Tukahoji tena siku alipohutubia wanaoitwa wazee wa Dar es Salaam hatukupewa majibu ya kuridhisha. Sasa tangu jana Tv ya taifa inaonyesha moja kwa moja mkutano wa wakuu wa Afrika Mashariki hata kufungua bara bara nako kumeonyeshwa moja kwa moja.

Swali la kujiuliza TBC ni mali ya Ikulu hata waitumie wanavyotaka? Hivi bunge na mkutano wa wakuu wa nchi ni kipi bora wananchi kuonyeshwa?
 
Hahaaaa kumbe bado mnamachungu ya kutoonyeshwa live bunge, si mlipie muonyeshwe jamani
 
Hahaaaa kumbe bado mnamachungu ya kutoonyeshwa live bunge, si mlipie muonyeshwe jamani
Ninyi nani kawambia tunataka kumuona rais wenu kwenye Tv kila siku kuliko wawakilishi wetu tuliowachagua na wanaowakilisha matakwa yetu?
 
Kuna tofauti ya gharama kati ya matukio ya masaa machache na vikao vya wiki tatu kutwa nzima
 
Back
Top Bottom