Nadhani JK ni Rais anayeongoza kwa kujumuika katika masuala ya Jamii

Amavubi

JF-Expert Member
Dec 9, 2010
30,146
13,216
Jamani tumfanye na Rais asomage humu mara moja moja kwa kuchombeza yale mazuri anayoendelea kufanya katika jamii yetu

Hapana shaka kwa hili hatutamsahau Rais wetu, ni mtu anayependa sana kuhudhuria katika masuala ya jamii hususan ni MISIBA, kutembelea wagonjwa, majanga (of course hili ni jukumu though optional) nk

Big Up kwa hili Kiongozi!!!

Ningeomba na mimi ukanikumbukage nitakaposinzia milele mkuu!!!

Amavubi-jf
 
Kwa hilo nakuunga mkono JK ni raisi pekee ambaye hujali sana kuwatembelea watu wapatapo matatizo ,utamukuta hata Tandale kaenda kutembelea wagonjwa au wafiwa,mara hospitalini kuwatembelea hata wabaya wake,nakumbuka alienda kumpa pole Kubenea ambaye kila leo anamunanga Kikwete,je uliwahi kumuona Mkapa,Nyerere na Mwinyi wakifanya hivyo?jibu ni hapana,Katika maraisi wote Kikwete ana utu sana wa kuwajali watu hata watu wa kawaida ,kwa hilo nampa hongera Kikwete, kwa utu na ubinadamu wake.
 
Hyo effort ya kuwajulia hali wagonjwa na kuhudhuria misiba angeiwekeza kwenye mambo mengne ya msingi yanayoikabili nchi yetu hakika tungekuwa mbali sana, though hyo socialization anayofanya sio kitu kibaya lakini akumbuke kuwa hakumchagua kwa kazi hzo.na wala asitumie kigezo hicho kumjenga kwamba yy ni kiongozi bora.
 
Lazima afanye hivyo kwani yeye mwenyewe pale alipo ni spana mkononi any time anakongoroka.
Ndiyo mana anajihami .
Ndiyo mana msafala wake sasa hivi haukosi ambulance nyuma.
 
Lazima afanye hivyo kwani yeye mwenyewe pale alipo ni spana mkononi any time anakongoroka.
Ndiyo mana anajihami .
Ndiyo mana msafala wake sasa hivi haukosi ambulance nyuma.

umekosa cha kuandika? Yaani msafara wa kiongozi wa nchi ukose amburance hii ni sawa, na huduma hii inawekwa c kwa ajiri ya rais tuu bali kwa yeyote atakayepata tatizo akiwa kwenye msafara.
 
Kikwete ni rais mnafiki sn.................kwa mfano suala la kumtembelea kubenea alikuwa anaua soo kwani ilishasemwa kuwa zile ni njama zake kummaliza....................pia alimtembelea kubenea ili kuthibitisha kuwa bado yu hai kwani alijua kwa mipango aliyokuwa amefanya asingeweza kupona...................................
Nyuma ya pazia kuna mambo mengi sana..............


kwa hilo nakuunga mkono jk ni raisi pekee ambaye hujali sana kuwatembelea watu wapatapo matatizo ,utamukuta hata tandale kaenda kutembelea wagonjwa au wafiwa,mara hospitalini kuwatembelea hata wabaya wake,nakumbuka alienda kumpa pole kubenea ambaye kila leo anamunanga kikwete,je uliwahi kumuona mkapa,nyerere na mwinyi wakifanya hivyo?jibu ni hapana,katika maraisi wote kikwete ana utu sana wa kuwajali watu hata watu wa kawaida ,kwa hilo nampa hongera kikwete, kwa utu na ubinadamu wake.
 
Hana vitu vya kumkeep bize!
Bse angekuwa bize ingekuwa mwendo wa kuwakilishwa tuu
 
Mmi binafsi yako mambo nakubaliana na Rais pia yako mengine nasema hapana! But kwa Rais kwenda kwao kujumuika na Ndugu zake je kosa lake ni lipi au nyani haoni kundule! Yeye ni Binadamu aliyezaliwa na wazazi wote wwawili hivyo kwao yeye ni Mtoto mbele ya wazazi wake na anatumwa kama wewe unavyotumwa na wazazi wako hata kama una umri mrefu!

Rais Kikwete Bagamoyo ni kwao na kutaendelea kuwa kwao na hawezi kubadilisha Bagamoyo kuwe Dar es Salaam!

Kuhusu Rais Kikwete kutembea na Gali la Wagonjwa jamani ifahamike kuwa Rais ni Taasisi ndugu zangu na Gari halipo kwa Ajili yake tu bali na Msafara mzima unamhusu yeye kama Mkuu wa Nchi na si vinginevyo!

Mimi binafsi nilikuwa katika Msafara wa Rais Kikazi na ghafla Joto la Mwili likabadilika na kuwa juu sana na hatukuwa Dar es Salaam lakini Afisa anayehusika na Masuala ya Tiba katika Msafara wa Rais haraka waliniingiza ndani ya Gari na Kupatiwa Tiba na si Huduma ya kwanza hivyo kama kusingekuwa na Gari hali yangu ingekuwaje!

Lazima tujue kuwa wakati mwingine mambo ya Kisiasa yana wakati wake na utekelezaji wa Majukumu ya kila siku una wakati wake!

Bado tukubaliane pamoja na Mabadiliko yanayochangia hali ya ngumu ya Maisha bado Taasisi ya Urais itaendelea kuwa na Ulinzi Mkali na Vyote vinavyotakikana maana Hata Leo akiingia Dr.Slaa bado atalindwa na Gharama zilezile za Ulinzi na Itifaki ileile maana Hakuna Rais anayeapishwa kisha akaachwa huru kujiamulia Mambo yake juu ya Ulinzi wa Kulindwa kwake na Matumizi ya Mengine!

Na hakuna Rais yeyote Duniani ambaye akichaguliwa anakuwa Juu ya Wazazi wake waliomzaa! Maana yeye ni Mtoto kwa Baba na Mama!
 
Jamani tumfanye na Rais asomage humu mara moja moja kwa kuchombeza yale mazuri anayoendelea kufanya katika jamii yetu

Hapana shaka kwa hili hatutamsahau Rais wetu, ni mtu anayependa sana kuhudhuria katika masuala ya jamii hususan ni MISIBA, kutembelea wagonjwa, majanga (of course hili ni jukumu though optional) nk

Big Up kwa hili Kiongozi!!!

Ningeomba na mimi ukanikumbukage nitakaposinzia milele mkuu!!!

Amavubi-jf


100% No problem with that......bravo Mr. PREZDAA
 
Jamani tumfanye na Rais asomage humu mara moja moja kwa kuchombeza yale mazuri anayoendelea kufanya katika jamii yetu

Hapana shaka kwa hili hatutamsahau Rais wetu, ni mtu anayependa sana kuhudhuria katika masuala ya jamii hususan ni MISIBA, kutembelea wagonjwa, majanga (of course hili ni jukumu though optional) nk

Big Up kwa hili Kiongozi!!!

Ningeomba na mimi ukanikumbukage nitakaposinzia milele mkuu!!!

Amavubi-jf
Una hakika kuwa wewe ndo utatangulia kufa ana pia ukitangulia yeye atakuwa bado mkulu pale Magogoni?Otherwise ni tabia zake tu kiswahili,maana ankosa muda wa kutosha wa kusocialise ndo maana ana bidii.
 
Hivi kutembelea wagonjwa nayo ipo miongoni mwa kazi za raisi? Mie nilidhani wasaidizi wake ndio wanatakiwa kumwakilisha yeye. Kwa hiyo atakuwa anahudhuria misiba ya watanzania wangapi? Au wagonjwa wangapi mahospitalini? Au ndo anawahani/na kuwatembelea wale anaowajua? Kuna makatibu kata, madiwani wenyekiti wa mitaa nilidhani hao ndo watakaomwakilisha. Najua kuwa ni ubinadamu kwenda kuwapa pole watu wenye matatizo. Lakini kwanini basi asitumie muda kama huo kufanya mambo ya maendele ya wananchi. Kama anatafuta kukubalika na jamii ni heri afanye mambo ya maendeleo. Wape watu umeme, maji sio kwenda kutoa tabasamu na kuweka miguu juuu!!
 
ukiona hivyo ujue hiyo misiba kasababisha yeye kwa hiyo anaenda kujipa happy ndo maana akifikaga huko anachekacheka tu kwanza msafara wake utakuja kumuua maana unakimbia utadhani anakimbizwa na al-shababy
 
Kikwete ni rais mnafiki sn.................kwa mfano suala la kumtembelea kubenea alikuwa anaua soo kwani ilishasemwa kuwa zile ni njama zake kummaliza....................pia alimtembelea kubenea ili kuthibitisha kuwa bado yu hai kwani alijua kwa mipango aliyokuwa amefanya asingeweza kupona...................................
Nyuma ya pazia kuna mambo mengi sana..............

Wewe hivi unadhani Kubenea alimwagiwa tindikali kwa nini? Alichukuwa mke wa mtu ndio maana mpaka leo ajasema nani aliemwagia tindikali!
 
Back
Top Bottom