Nadhani kuna tatizo mahali fulani hapo NACTE.
Hili baraza linapaswa kuchunguzwa kwa mambo mengi.
1. Uendeshaji wa kibabaishaji kwenye vyuo
Mfano vyuo kutapeli wazazi kwa malipo yasiyo rasmi.Unayakuta chuoni tu wakati mwingine yanapokelewa bila risiti.
Pia malipo ya NHIF na wakati hawatoi kadi za matibabu au wanatoa kwa watu wachache tu.
2. Baadhi ya vyuo kuwa na wanafunzi wengi kuliko uwezo wa miundombinu iliyopo.Hakuna anayejali bora wakusanye pesa tu!
3. Vyuo binafsi kutokuwa na bodi na hivyo mmiliki kuamua chochote anachojisikia bila kujali hata kama taaluma itaathirika.Mfano kukusanya pesa za field halafu wanafunzi hawaendi field au wabaenda siku chache tu.
4. Vyuo kutokuwa na walimu wa kutosha na bado vinaendelea kudahili wanafunzi wengi