Suip
JF-Expert Member
- Sep 21, 2010
- 1,374
- 848
Kuna vijana niliwasaidia kuomba vyuo vya afya kupitia NACTE, mmoja aliomba nursing na alichaguliwa katika second selection na kuthibitishwa kuwa anaenda chuo fulani(sitaki nikitaje) lakini alipowasiliana na chuo wakamjibu chuo kimejaa na jana wamembadilishia chuo na bado hakuthibitishiwa hiyo nafasi yaani pending, sasa ni vyuo vinajipangia au NACTE wanapanga baada vyuo kuwapatia idadi ya wanafunzi wanaohitajika?
Wa pili aliomba kozi ya Community Health na katika third selection ya leo hakuchaguliwa ila wanasema anavigezo(eligible) abadilishe machaguo yake, sasa hoja kama anavigezo mbona hawakumchagua wakati yeye ana point 27 na ana D zaidi ya 4 na moja ikiwa ya Biology lakini katika vyuo vitatu alivyochagua cut off point ya mwanafunzi wa mwisho kuchaguliwa ni point 29, 28, na 28.
Ni vigezo gani vilivyotumika kumwacha wa division 4 ya point 27 unamchukua division 4 ya point 29 na 28.
Yawezekena NACTE hakuna meno ya kuthibiti vyuo hivi,basi waacheni wanafunzi waoombe moja kwa moja vyuoni badala ya ninyi kukusanya fedha za watu bure ilhali hamna uwezo.
Wa pili aliomba kozi ya Community Health na katika third selection ya leo hakuchaguliwa ila wanasema anavigezo(eligible) abadilishe machaguo yake, sasa hoja kama anavigezo mbona hawakumchagua wakati yeye ana point 27 na ana D zaidi ya 4 na moja ikiwa ya Biology lakini katika vyuo vitatu alivyochagua cut off point ya mwanafunzi wa mwisho kuchaguliwa ni point 29, 28, na 28.
Ni vigezo gani vilivyotumika kumwacha wa division 4 ya point 27 unamchukua division 4 ya point 29 na 28.
Yawezekena NACTE hakuna meno ya kuthibiti vyuo hivi,basi waacheni wanafunzi waoombe moja kwa moja vyuoni badala ya ninyi kukusanya fedha za watu bure ilhali hamna uwezo.