Aisee wewe inaonekana ulikuwa mvivu darasani, lakini pia kama ndiyo uko cheti au foundation maana naona unaogopa mtihani wa pamoja. Sasa kwanini uogope wakati kwa sekondari imewezekana, kumbuka mwanafunzi wa shule ya kata isiyo na waalimu wa sayansi au waalimu wa kutosha wanafanya mtihani moja na wale wa Tusiime, marian, feza nk kwanini wewe unayechukua cheti hombolo usifanye mtihani moja na wa magogoni au cbe? Naona unafurahia sana kubebwa kwa wanafunzi jinsi inavyofanyika hivi sasa kwenye hivyo vyuo vyenu.