NACTE iwe na mitihani kama NECTA

kindikwili

JF-Expert Member
Oct 5, 2016
1,862
2,871
Kwanza nachukua fursa hii kumpongeza waziri wa elimu prof Ndalichako japo najua wachache watanielewa kutokana na mtazamo hasi zilianza kujengwa kwake. Ukweli ni kwamba sisi watanzania kwa sehemu kubwa hatujui hasa tunachokitaka. Tulilia mabadiliko sana lakini hatukujua ni kipi tulitaka, watu walitaka rushwa na ufisadi udhibitiwe bila kujua kuwa kwa kufanya hivyo kuna impact kubwa utaonekana hadi kwa watu ambao walikuwa hawali rushwa wala si mafisadi. Watu walitaka mabadiliko kwenye sekta ya elimu lakini wakiwa na ndoto kuwa hawatayumbishwa hata kidogo. Ukitaka mabadiliko jiandaye kuyapokea maumivu yake maana ni kama kubomoa na kujenga upya nyumba yako.

Nasikitika sana jinsi kauli ya prof Ndalichako ulivyopotoshwa kwa makusudi, mimi nilipoisikia kwenye You tube nilisikia kipande alichokuwa akiongelea foundation courses kwa aliyefeli form six. Akidai kuwa foundation haimpi mtu uhalali wa kusoma chuo kikuu, lakini watu walipotosha kuwa kasema hakuna kwenda chuo kikuu kupitia certificate kisha diploma. Hadi wasomi walikuja juu na kumshambulia prof Ndalichako bila hata kusikia kauli yake. Dk Bana alipoulizwa na mwandishi kuhusu kauli hiyo alisema ''kama kweli kasema hivyo basi kakurupuka na hakushauriwa vizuri''. Hivi ilikuwa inamgarimu dk Bana kitu gani kumwambia mwandishi samahani mimi hiyo habari sijamsikia akisema nipe muda niitafute kisha nitatoa maoni baadaye. Kwani ni lazima kutoa maoni kwa kauli ambayo hujaisikia tena ukijua kuwa baadaye utanukuliwa kwenye hiyo habari?. Kwa maoni yangu wale wote waliomshambulia prof Ndalichako ni WASOMI UCHWA HATA KAMA WANA PhD ngapi. Mtu mwenye Phd huwezi kukosoa kitu ambacho hujakisikia.

KUHUSU NACTE KUWA NA MITIHANI YA TAIFA KAMA NECTA
Baraza la mitihani la taifa (NECTA) kama tunavyojua huwa na mtihani moja kwa shule zote za sekondari nchinzi nzima. Mtihani hii huwa ni kipimo cha marifa na uelewa unaotakiwa mwananfunzi apate ili kukidhi vigezo vya kuendelea na masomo ya advance au chuo kikuu. Ni vyema NACTE ikatoa syllabus kwa vyuo vyote vya kati kwa ajili ya kufundishia courses zao kisha Nacte itunge kna kuratibu mitihani ya cheti na diploma ili anayefaulu mtihani huo wa NACTE aendelee na diploma au degree. Vyuo vingi vya kati vimegeuza elimu hiyo biashara, mtoto anaandikishwa katikati ya muhula maana kinachoangaliwa ni pesa. Hawataki mtoto afeli ili kuvutia wengine waje kusoma kwao. Kinachoangaliwa kwenye usahishaji ni jinsi mwanafunzi alivyomwaga wino na si vitu alivyovijibu. Kuna baadhi ya vyuo hivi ambavyo uongozi wa shule hutoa memo rasmi kwa walimu kutokuwafelisha wanafunzi kwa madai kuwa watahamia vyuo vingine au kufanya wengine wasije kusoma kwao . Maafisa mitihani wa baadhi ya vyuo hivi wametajirika kwasbabu wana uwezo wa kubadili matokeo ya mwanafunzi na hata matokeo ya mwisho na kumfanya mwanafunzi kuwa na GPA isiyo yake. Hapa rushwa ya ngono na pesa hutawala kwa sehemu kubwa. Wakuu wa vyuo hivi hutoa ruksa wanafuzi kuongezewa marks ili kupandisha GPA ili wapate nafasi ya kwenda vyuo vikuu. Haya ninayoyasema nina uhakika nayo. Kama umesoma degree angalia uwezo wa wanafunzi wanaotoka form six na hawa wa equivalent utanielwa. Hawa wanafunzi huwa ni wazito hatari, Wakati fulani nikisoma degree waliwahi kudisco wanafunzi 12 na wote walikuwa kutoka diploma.
Nashauri Mheshiwa ndalichako aamuru NACTE kutunga na kusahihisha mitihani ya certificate na diplama kama NECTA wanavyofanya hii itapunguza uholela kwenye elimu hii ya kati. Waziri ana nia nzuri ya kugeuza elimu yetu kutoka ilipokuwa ikitolewa kiholela bila usimamizi. Meshimiwa waziri nitabaki nawe hata ikibidi kubaki wawili, nakutakia kila la heri na Mungu akubariki.
 
Kuna vyuo ambavyo Nacte wanawatungia mitihani na vingine vinafanya yake. Hivi vyuo ni tofauti na university maana kwao wanaangalia skills. Hivyo ni ufinyu wa mawazo iwapo mtu alieanzia katika CBET kwenda KBET.
 
(Kama ) ni kwel. Sasa ultaka Dr bana asubr nn majbu alyotoa yuko sahh umetumwa ww
Kama ni kweli ni majibu yenye mshaka , msomi wa aina ya bana anatakiwa kutoa majibu yenye uhakika na si ya ku guess . Hatuwezi kuwa na wasomi wanaguess kauli badala ya kusikiliza ,kuelewa ,kutafakari na kisha kutoa majibu sahihi.
 
Kuna vyuo ambavyo Nacte wanawatungia mitihani na vingine vinafanya yake. Hivi vyuo ni tofauti na university maana kwao wanaangalia skills. Hivyo ni ufinyu wa mawazo iwapo mtu alieanzia katika CBET kwenda KBET.

Lazima tuwe na mtihani moja kupima hiyo competency kama NECTA wanavyopima knowledge kwa wanafunzi wa sekondari kwa mtihani moja. Tukisema kila mtu adefine competency hatutafika, utajuaje wale cheti wa MU wako competent kusoma degree na wale cheti wa magogoni hawako competent?
 
Kwanza Nacte ni wababaishaji tu! ni taasisi iliyokaa kisiasa! Wanakula hela za watu alafu hakuna kinachofanyika cha maana.
1. Zile hela wanazokusanya toka vyuo vyote zinafanya kazi gani?
2. Nani anawafanyia auditing kwa mambo yao yote?
3. Utaratibu wa kiutendaji kazi wao ni wa ubabaishaji .. mtu anaomba kusoma kusoma kozi fulani .. analipa hela .. majibu hawamtumii .. kila akiingia kwenye mtandao wao unakuwa very slow... nani wa kuwaadabisha?
 
Kwanza Nacte ni wababaishaji tu! ni taasisi iliyokaa kisiasa! Wanakula hela za watu alafu hakuna kinachofanyika cha maana.
1. Zile hela wanazokusanya toka vyuo vyote zinafanya kazi gani?
2. Nani anawafanyia auditing kwa mambo yao yote?
3. Utaratibu wa kiutendaji kazi wao ni wa ubabaishaji .. mtu anaomba kusoma kusoma kozi fulani .. analipa hela .. majibu hawamtumii .. kila akiingia kwenye mtandao wao unakuwa very slow... nani wa kuwaadabisha?

watoke nje waone hii elimu ya kati inavyonunuliwa kwa hela na wanafunza kwa kike kuvuliwa bikini zao. Yaani ni balaa tupu hii elimu inahitaji usimamizi wa hali ya juu kama NECTA tu la sivyo wanafunzi waonwatapenya hivi mpaka wawe degree, masters na PhD za hovyo bila kuwa na kitu kichwani.
 
watoke nje waone hii elimu ya kati inavyonunuliwa kwa hela na wanafunza kwa kike kuvuliwa bikini zao. Yaani ni balaa tupu hii elimu inahitaji usimamizi wa hali ya juu kama NECTA tu la sivyo wanafunzi waonwatapenya hivi mpaka wawe degree, masters na PhD za hovyo bila kuwa na kitu kichwani.
Kwa sasa elimu sio makaratasi; elimu ni kile kilichopo kwenye ubongo wa mtu! Haya makaratasi wanayopewa toka kwenye vyuo ni majanga matupu!
 
Lazima tuwe na mtihani moja kupima hiyo competency kama NECTA wanavyopima knowledge kwa wanafunzi wa sekondari kwa mtihani moja. Tukisema kila mtu adefine competency hatutafika, utajuaje wale cheti wa MU wako competent kusoma degree na wale cheti wa magogoni hawako competent?
Naomba unisamehe kuchangia uzi wako maana inaonyesha hujui ulitendalo na hujui tofauti kati ya aina hizi mbili za elimu. Ukitaka kuelimishwa uliza ila kama ni ubishi, bye!
 
Naomba unisamehe kuchangia uzi wako maana inaonyesha hujui ulitendalo na hujui tofauti kati ya aina hizi mbili za elimu. Ukitaka kuelimishwa uliza ila kama ni ubishi, bye!

Usisubiri mimi nikuombe unielimishe kama una cha kunielimisha wewe toa elimu kwangu na kwa wengine. Mimi uzi wangu umetokana na experience ya kutosha katika hii field ya elimu ya kati, kuna maovu yasiyopimika, inatolewa chini ya viwango na hata wanafunzi wanaoenda vyuo vikuu wakitokea diploma huwa ni hafifu sana. wewe fikiria mtu anatoka advance alikosoma HGE anaenda kuoma BAF pale mzumbe anakutana na mtu aliyesoma diploma ya Accounts CBE,TPSC nk halafu huyu wa form six anafanya vzr kutoka mwanzo hadi mwisho kumzidi aliyesoma diploma wakati def ya accounts anaenda kuikutia mwaka wa kwanza. Hoja yangu ya pili ni kwamba kama syllabus ni moja nchi nzima still NACTE wanaweza kuwa na mtihani moja standard kwa vyuo hivi, PSPTB na NBAA wameweza kwani wao hawapimi competency?. Ukijifanya kuja na CBET NA KBET ukidhani ni maneno mageni basi pole maana jua unaongea na mwanataaluma.
 
kuwavutia wanawambia njoo ujiunge uende chuo kikuu! yaan ukishafanyiwa usajil tu hkn kufel, km uliingia na D zako 4 unatoka na first class ya 4.8.

Ndg mimi hii nimeiona kwa macho yangu na still naiona, hii elimu hata kwenye vyuo vya umma kama TPSC na branches zake, Hombolo , CBE, Mzumbe, Theofilo na vingine vyote mchezo huu upo. Kama waziri anataka kutimiza lengo lake la kuboresha elimu ni vizuri hili akalishughulikia kwa nguvu zote.
 
Usisubiri mimi nikuombe unielimishe kama una cha kunielimisha wewe toa elimu kwangu na kwa wengine. Mimi uzi wangu umetokana na experience ya kutosha katika hii field ya elimu ya kati, kuna maovu yasiyopimika, inatolewa chini ya viwango na hata wanafunzi wanaoenda vyuo vikuu wakitokea diploma huwa ni hafifu sana. wewe fikiria mtu anatoka advance alikosoma HGE anaenda kuoma BAF pale mzumbe anakutana na mtu aliyesoma diploma ya Accounts CBE,TPSC nk halafu huyu wa form six anafanya vzr kutoka mwanzo hadi mwisho kumzidi aliyesoma diploma wakati def ya accounts anaenda kuikutia mwaka wa kwanza. Hoja yangu ya pili ni kwamba kama syllabus ni moja nchi nzima still NACTE wanaweza kuwa na mtihani moja standard kwa vyuo hivi, PSPTB na NBAA wameweza kwani wao hawapimi competency?. Ukijifanya kuja na CBET NA KBET ukidhani ni maneno mageni basi pole maana jua unaongea na mwanataaluma.
Naamini wewe ni mwanafunzi!
 
ww jamaa una mawazo mzr, eb tafuta e-mail ya wzr uwatumie huu ujumbe utamfkia mheshimiwa.
Uwe unafikiri na kutafakari kile ufikiriacho!!; Kiunagaubaga nikuambie hivi Watanzania hatuko tayari kurudi huko nyuma tulikotoka! NACTE walikuwa na FTC maana yake walikuwa wanafanya hayo mwandishi aliyoyasema na kwa sasa hivi ni Diploma yaani Chuo wanatunga na kusahihisha mitahani zao tena kwa gharama zao wenyewe!
 
Uwe unafikiri na kutafakari kile ufikiriacho!!; Kiunagaubaga nikuambie hivi Watanzania hatuko tayari kurudi huko nyuma tulikotoka! NACTE walikuwa na FTC maana yake walikuwa wanafanya hayo mwandishi aliyoyasema na kwa sasa hivi ni Diploma yaani Chuo wanatunga na kusahihisha mitahani zao tena kwa gharama zao wenyewe!

Wewe badala uishauri NACTE namna nzuri ya kuendesha hivi vyuo kama NECTA walivyoweza unaleta bla bla, kwanini washindwe ilhali hivi vyuo ni vichache kuliko sekondari nchini. Halafu wewe huangalii hasara nchi inayopata kuzalisha watu wasio na uelewa juu ya waliyoyasomea. Vyuo hivi vimegeuza elimu biashara, mwanafunzi anamaliza diploma na GPA ya 3.5 ila kiuhalisia hakupata hivyo, wanaongezewa ili wafikie alama zinazotakiwa na TCU kujiunga vyuo vikuu. Lini umeona mwanafunzi wa form six akaongezewa marks ili zifikie zinazotakiwa na TCU?. TUKITAKA MABADILIKO LAZIMA TUKUBALI KUUMIA MABADILIKO SI MCHEZO.
 
Wewe badala uishauri NACTE namna nzuri ya kuendesha hivi vyuo kama NECTA walivyoweza unaleta bla bla, kwanini washindwe ilhali hivi vyuo ni vichache kuliko sekondari nchini. Halafu wewe huangalii hasara nchi inayopata kuzalisha watu wasio na uelewa juu ya waliyoyasomea. Vyuo hivi vimegeuza elimu biashara, mwanafunzi anamaliza diploma na GPA ya 3.5 ila kiuhalisia hakupata hivyo, wanaongezewa ili wafikie alama zinazotakiwa na TCU kujiunga vyuo vikuu. Lini umeona mwanafunzi wa form six akaongezewa marks ili zifikie zinazotakiwa na TCU?. TUKITAKA MABADILIKO LAZIMA TUKUBALI KUUMIA MABADILIKO SI MCHEZO.
Kwenye "Mitihani ya pamoja tulishatoka tena kwa maumivu makali sana"! Narudia kusema hivi Watanzania hatuko tayari kurudi kule tuliko toka ni bora tubuni njia nyingine sahihi ambayo tunaamini itatufikisha!
 
Kwenye "Mitihani ya pamoja tulishatoka tena kwa maumivu makali sana"! Narudia kusema hivi Watanzania hatuko tayari kurudi kule tuliko toka ni bora tubuni njia nyingine sahihi ambayo tunaamini itatufikisha!
mbona coz za ualimu( certficate na diploma) wamerudisha NECTA so inawezekana...acha kuiogopa itakufanya uwe na elimu bora.
 
Kwenye "Mitihani ya pamoja tulishatoka tena kwa maumivu makali sana"! Narudia kusema hivi Watanzania hatuko tayari kurudi kule tuliko toka ni bora tubuni njia nyingine sahihi ambayo tunaamini itatufikisha!

Aisee wewe inaonekana ulikuwa mvivu darasani, lakini pia kama ndiyo uko cheti au foundation maana naona unaogopa mtihani wa pamoja. Sasa kwanini uogope wakati kwa sekondari imewezekana, kumbuka mwanafunzi wa shule ya kata isiyo na waalimu wa sayansi au waalimu wa kutosha wanafanya mtihani moja na wale wa Tusiime, marian, feza nk kwanini wewe unayechukua cheti hombolo usifanye mtihani moja na wa magogoni au cbe? Naona unafurahia sana kubebwa kwa wanafunzi jinsi inavyofanyika hivi sasa kwenye hivyo vyuo vyenu.
 
Back
Top Bottom