Biblia inasema zipimeni roho kama zatoka kwa Bwana au la Maana hata wajumbe wa shetani hufanya miujiza pia , lakini pia niwashauri kuwa kuna ulimwengu wa roho ulimwengu wa roho una pande mbili , upande wa Mungu aliyeumba Mbingu na nchi na upande wa shetani hapa lazima uwe mwanachama katika upande mmoja tu. Walioko upande wa shetani hupenda kuigiza kwamba ni watumishi wa Mungu ukitaka kujua kwamba mtumishi aliyepo mbele yako ni wa upande gani 1. Mtumishi wa Mungu aliyehai kumuona ni bure kabisa hakuna fedha yoyote utakayotakiwa kutoa 2. Mtumishi wa Mungu yoyote Shauku yake kubwa ni kuona watu wanaokolewa kila baada ya kufanya mkutano ataita watu waokoke. 3 Mtumishi wa Mungu yoyote haelezei mambo ya kichawi awapo madhabahuni bali humtukuza Mungu
4. Mungu hazoeleki kama anataka kukuponya hawezi kutumia njia moja wengi manabii wanatumia mafuta Mafuta mengi hutoka kuzimu , ikumbukwe kuwa Mafuta kwa mfalme Daudi yalitumika kwa sababu aliandaliwa kuwa mtawala , inashangaza kuona siku hizi kwenye maombi ya manabii hutumia mafuta, hata kama kusoma hujui itoshe tu ujue Watumishi wengi sio wa Mungu ni kutoka kuzimu.
5 . pia ukimuona mtumishi yoyote wa Mungu hana msaidizi katika huduma yake hamuachii mtumishi wa Mungu yoyote kanisa akisafiri anaweka kanda au hataki kusafiri , wandugu hayupo Mungu wa hivyo kumbuka Elisha na eliya, Musa na Joshua walikabidhiana kazi za utumishi kwa kufundishana na kuwa karibu , hii inaitwa on job training hata wanadam wanafanya hivyo sembuse Mungu wa miungu .
6. Pia suala la upako ambao unatoka kwa Mungu aliumba vyote ni kwamba unaongezeka kuanzia mwanzo mpaka mwisho unakua mwingi Mungu humuonyesha mwanadamu huduma yake akitonyesha mwisho akitokea mwanzo hii ndio tabia ya Mungu aliyeumba wanadamu kwa hiyo huwezi kukuta mtu from know where akawa na upako mwingi na hauongezeki , na staili yake ya kuombea lazima awawekee mkono kila siku pana shida , anaChokiongea huwa hafikirii anaropoka tu ujue pana shida kwa mtu huyo .
Nimeamua niwaandikie mabo machache yatayowapa picha ya kujua mtumishi gani ni wa Mungu na yupi sio wa Mungu sitaji mtu ila pimeni wenyewe , "Wanadamu yafuateni haya kwa umakini mkubwa maana wajumbe wa shetani wapo wachungaji wanamapepo ambayohufanya kama vile Mungu aponyavyo , Msiwe wabishi kwakuwa mliwahi kwenda mkaponywa Shida zenu , ila kumbukeni Mtaikosa Mbingu pia Mtakosa kutembea na Mungu huku Duniani , mtapata na Laana kwa Mungu yote hufunguliwa kwa pamoja . Nimalizie kwa kusema Mungu yupo mtafuteni kwa Bidii hakika mtamuona mwaka 2017 ni mwaka wa kuwatambua watumishi waongo na wakimbieni maana Mungu anawaumbua watu hao mwaka huu. Mungu awabariki katika kristo Yesu