Habr zeny wana jf. Me nikijana mwenye umri wa miaka 23, tatizo langu sinaga mwisho mzuri na wasichana ninaowatokea. Niliwah kuwa na mahusino na msichana mmoja nikiwa na umri wa miaka 18. Tulikuja tengana kwa kukosa uhaminifu. Tokea hapo sikuwahi tena kuwa na mahusiano ya kimapenzi na msichana yeyete hadi leo hii. Kutongoza najua, shida inakuja pale ninapokubaliwa nakuwa sijui cha kuendelea mbeleni, yaani nakuwa kama mgeni kwenye mapenzi. Kwa mfano naweza kumpigia dem niliemtongoza mwnyw akanikubalia then nisiongee chochote cha maana, mwisho wa sku tunaagana kila mtu kivyake, hata nikipanga tukutane bado hali ni kama hiyo. Basi kwa hali najikuta ndani ya 2week tumesha achana, na utakuta sijaambulia hata kiss. Na huwaga inatoke mara kwa mara ninapotongoza msichana mpya. Naomba mnisaidie kimawazo maana sielewi hii ni type ya domo zege au ni tabia 2.