Naanza kumkubali Naibu Spika Ndugai....

Nimekuwa nafuatilia vikao vya bunge kwa kipindi sana hasa katika bunge hili lililoanza mwaka 2010 ambalo limekuwa linakaribiana na changamoto kubwa nadhani kuliko mabunge yote yaliyowahi kutokea. Katika hali hii uongozi imara ni jambo kubwa kabisa lilikuwa linahitajika ambapo wote mtakuwa mashahidi kwamba ulionekana kutokuwepo katika vikao vya mwanzo vya bunge hili.

Hali naona kama imeanza kurekebika kidogo hasa kwa Naibu Spika ambaye naona kadri siku zinavyokwenda amekuwa akibadilika kwa mtazamo chanya kiasi cha kuanza kuaminiwa kwa uongozi wake. Napenda nikiri kwamba kwa Spika mwenyewe bado hajaonyesha hivyo na pia kwa wenyeviti (Hasa yule mwenyekiti ambaye mara zote akiongoza anaondoka na balaa)

Kwa ufupi napenda niseme kwamba naanza kumuamini naibu spika na nakuwa na imani ya kikao kwenda salama pale anapokuwa anaongoza bunge


Ni mtazamo wangu tu................

Mtazamo wako ni hasi+++++!

Hivi wewe unategemea mwanamme mzima anayeongozwa na mwanamke anaweza kuwa na maamuzi sahihi kweli???
Ndugai hana lolote wala chochote nim mbambaishaji mmoja tu kutoka Chama Cha Magamba aliyeukwa ulaji wa Uspika.
Jiulize ni kwanini swala la Posho linawatesa Wabunge wa CCM kwa sasa. Ndugai na Bibi yake Makinda walikubaliana kuwadanganya Wabunge kuwa Rais alikuwa amesha saini kibali cha kuruhusu ongezeko la Posho, kitu ambacho hakikuwa kweli!

Ndugai huyu huyu alienda kuropoka mbele ya vyombo vya habari kwamba NYONGEZA WATAKAYOLIPWA WABUNGE ilikuwa eti ni fedha kidogo sana ukilinganisha na malipo ya mihimili na taasisi zingine!
Hapa ndipo unaweza kugundua ukihiyo wa Ndugai kwa kutaka kutumia kigezo cha ofisi za watu wengine kama kigezo cha kuongezewa posho!!!

Narudia tena Ndugai na Bibi Anna Mikanda wameshindwa kuongoza Bunge.
 
2015 atakuwa spika kwakuwa makinda atakuwa waziri mkuu wa kwanza mwanamke!!
Siwezi kusema hapana, lakini this will be the biggest mistake of them all. Kuongoza ni kipaji kama huna huna tu na kwa mtizamo wangu huyu mama hana sio tu kama yeye lakini pia anakosa ule mvuto kwa watu
 
Mtazamo wako ni hasi+++++!

Hivi wewe unategemea mwanamme mzima anayeongozwa na mwanamke anaweza kuwa na maamuzi sahihi kweli???
Ndugai hana lolote wala chochote nim mbambaishaji mmoja tu kutoka Chama Cha Magamba aliyeukwa ulaji wa Uspika.
Jiulize ni kwanini swala la Posho linawatesa Wabunge wa CCM kwa sasa. Ndugai na Bibi yake Makinda walikubaliana kuwadanganya Wabunge kuwa Rais alikuwa amesha saini kibali cha kuruhusu ongezeko la Posho, kitu ambacho hakikuwa kweli!

Ndugai huyu huyu alienda kuropoka mbele ya vyombo vya habari kwamba NYONGEZA WATAKAYOLIPWA WABUNGE ilikuwa eti ni fedha kidogo sana ukilinganisha na malipo ya mihimili na taasisi zingine!
Hapa ndipo unaweza kugundua ukihiyo wa Ndugai kwa kutaka kutumia kigezo cha ofisi za watu wengine kama kigezo cha kuongezewa posho!!!

Narudia tena Ndugai na Bibi Anna Mikanda wameshindwa kuongoza Bunge.
Kama unakumbuka alisema kwamba "Ni kweli hali ya wananchi ni mbaya sana kwa sasa ila hebu tusiangalie bunge peke yake tuangalie na maeneo mengine ambayo kimsingi kuna posho zaidi ya mara mia ya hizi za bunge"

Well mimi mwenye sitaki hata kusikia habari ya hhizo posho za wabunge maana posho ya siku moja ni mshahara wangu wa mwezi mzima ambao nao naupata kwa mbinde
 
kesho atakusurprise,..huwajui magamba wewe,kwanza inawezekana wakamwekea kikao kwa kuiacha serikali isulubiwe kama sitta halafu hizi ni hasira/visasi vya kupigwa danadana posho zao....don't expect anything white from the charcoal..yuou spoke too soon mkuu.
 
Kitendo cha kukubali muongozo na kutoa maamuzi kwa busara, alafu nimegundua kumbe spika Anna Makinda ana hasira sana.!

Abdallah na Musimo Jr!
Hata mie naafiki mitazamo yenu, ni kweli kwa kiasi fulan Ndugai anajifanyia marekebisho katika maamuzi yake na busara inatumika zaidi na pia wakati mwingine huwa haangalii itikadi za vyama iwapo hoja ina msingi.

Si vibaya kupongeza pale tunapoona mazuri sio kulaumu pekee, pongezi zinasaidia kujenga imani kwa mhusika!

Ni maoni tu!
 
Hapana anatumi hasira kuficha ujinga wake, na uwezo mdogo wa kiuongozi alionao.

kweli kabisa,unajua mtu anaweza kufanya kitu fulani akijua kabisa wengine watafikiri kuwa ni udhifu wa kimaumbile kumbe nyuma ya pazia anafanya hivyo kuficha upande wa pili wa shilingi.huyu mama hana uwezo kabisa wa kuongoza hata kijiji au mtaa.
 
kweli umesema vyema!! nami nakuunga mkono!!!! tumpe haki yake, hata alivyo lichukua suala la mgomo wa madaktari!! mpaka kuwekwa kenye kamato ya kibunge ya huduma za jamii, ni uamuzi wa spika baada ya wabunge kugoma kulijadili, hata kuomba kauli ya serikali kuhusu mgomo, ni uamuzi wa mh JOb, baada ya wabunge wa upinzani kuomba hivyo wabunge wakakataa kuunga mkono!! Naibu spika akaamua ilivyo sasa!!

ni mtizamo wangu ananibariki!!
 
kesho atakusurprise,..huwajui magamba wewe,kwanza inawezekana wakamwekea kikao kwa kuiacha serikali isulubiwe kama sitta halafu hizi ni hasira/visasi vya kupigwa danadana posho zao....don't expect anything white from the charcoal..yuou spoke too soon mkuu.
I know what you mean brother, and i have been saying always that i hate these stuff they call "Party Coccus" wanaenda wanaambizana maneno yao then wanakuja na maamuzi ya kipuuzi.

Thats their biggest problem asee
 
Nimekuwa nafuatilia vikao vya bunge kwa kipindi sana hasa katika bunge hili lililoanza mwaka 2010 ambalo limekuwa linakaribiana na changamoto kubwa nadhani kuliko mabunge yote yaliyowahi kutokea. Katika hali hii uongozi imara ni jambo kubwa kabisa lilikuwa linahitajika ambapo wote mtakuwa mashahidi kwamba ulionekana kutokuwepo katika vikao vya mwanzo vya bunge hili.Hali naona kama imeanza kurekebika kidogo hasa kwa Naibu Spika ambaye naona kadri siku zinavyokwenda amekuwa akibadilika kwa mtazamo chanya kiasi cha kuanza kuaminiwa kwa uongozi wake. Napenda nikiri kwamba kwa Spika mwenyewe bado hajaonyesha hivyo na pia kwa wenyeviti (Hasa yule mwenyekiti ambaye mara zote akiongoza anaondoka na balaa)

Kwa ufupi napenda niseme kwamba naanza kumuamini naibu spika na nakuwa na imani ya kikao kwenda salama pale anapokuwa anaongoza bunge


Mkuu kama ni kwa kipimo cha leo bungeni kukubali mwongozo wa Mh mbunge wa Kigoma Serukamba na kuutolea ufafanuzi bado mimi sijaona kama anafaa,ila ametumia mbinu za kuwalaghai kwa kujifanya suala hilo lina mgusa na ligusa bunge,lakini ukweli ni kwamba hoja iliyotolewa mbele yake haikuhitaji kikao cha chamber tena chenye kumuhusisha Spika ambaye jana aliikataa hoja hiyo ya dharura,na hata hivyo mantiki ya hoja iliyotolewa na Mh Serukamba ni ya dharura,maana ya dharura unaijua mkuu,iweje isubiri kesho au siku nyingine?na je kuielekeza kwa Spika na kamati ya maadili inayohusisha wenyeviti wa kamati unategemea kuna kitu gani hapo,wakati Makinda huyo huyo aliiikataa hoja hiyo jana?na ni kwa lipi unamkubali Ndugai wakati ameliahirisha bunge hadi kesho?bado hiyo dharura inakuwapo?kwa kusubiri kesho unadhani ni wagonjwa wangapi watapoteza maisha leo kwa kusubiri wakakae chamber?
Ndugai ni kama JK anataka lawama zimwendee Makinda tu na yeye aonekane mwema,kumbe wote ni wabovu tu,na haiwezekani spika mwema na mpenda haki akatokea CCM hii ya leo,never ever!
Dharura mkuu haisubir kesho,dharura unaanza kui-addreess on the sport.hao wote hawana uchungu na watanzania,hata wabunge mimi napata shida nao,maana kama watu wanapinga hoja ya dharura ambayo kimsingi iko wazi kwa kila mtu nanyi wabunge mko wengi watawashindaje watu wawili tu?kweli kama kuna wabunge wanasikia uchungu na vifo vinavyosababishwa na ukosefu wa tiba wanaendelea kukaa bungeni kufanya nini?si wawagomee hao maspika?hivi utaendelea kuheshimu mtu anaekuzuia kujadili vifo vya watu wako,vifo vya wapiga kura wako,utamweheshimu vipi,hata kama ni kanuni za bunge ni kanuni ipi specific inayozuia wabunge kujadili jambo la dahrura?dharura hii kwani ni ya kufikirika au ni uhalisia?hapa kinachofanyika ni kuilinda serikali isianguke bila kujali ni kwa gharama ya roho za watu.si suala la kutuambia eti Mh nduagi umeanza kumkubali,unamkubali kwa lipi?yeye si Spika angesema sasa jamani wahaeshimiwa wabunge suala hili ni zito na tuanze kujadili,na majinbu yangepatikana,maana bunge lina sura mbili pale,kuna serikali kwa maana ya mawaziri na kuna wawakilishi wa wananchi ambao ni wabunge lakini wabunge hao ndio wanapitisha bajeti na matumizi mengine ya serikali na hakika kuna majibu leo yangepatikana ambayo yamo kwenye orodha ya madai ya ma-daktari.
JAMANI NAKERWA SANA NA USHABIKI HUU,NAKERWA SANA MTU ANAPOSHAWISHIKA KWA MANENO YA KILAGHAI YA VIONGOZI WETU.LEO NDUGAI KAFANIKIWA KUWALAGHAI WATU KWA KUONYESHA YUKO UPANDE WA WABUNGE WANAOTAKA KUJADILI JAMBO LA DHARURA MWISHO WA SIKU KAWAAMBIA KAMATI YA MAADILI IKAJADILI CHAMBER,HALAFU WENGINE MMERIDHIKA NA NDUGAI,NO PLEASE TUTAFAKARI UPYA

 
Tabia za nchi masikini ndo kama hii.Viongozi awapendi kujadili matatizo wa wananchi wao,Tumbo mbele kwa kila kitu
Toa mfano kipi naibu spika kafanya cha kuwanufaisha wananchi.?

Alisema (Sio nukuu ya iliyorekodiwa, ila ujumbe ni ule ule) "Msiangalie posho za wabunge tu, kwani hilo ni tone katika bahari. Mmehoji na kujua viongozi wengine wa serikali na mashirika ya umma wanalipwa posho kiasi gani?"

Ukweli ni kwamba wabunge ndio wamekuwa wa mwisho kudai posho ya TZS 200,000 kwa kikao. Tetesi ni kwmba kuna GN ambayo ilipitisha posho hizi mwaka jana, na nafikiri Pinda aliposema Rais amesaini, alimaanisha waraka huo.
 
Alisema (Sio nukuu ya iliyorekodiwa, ila ujumbe ni ule ule) "Msiangalie posho za wabunge tu, kwani hilo ni tone katika bahari. Mmehoji na kujua viongozi wengine wa serikali na mashirika ya umma wanalipwa posho kiasi gani?"

Ukweli ni kwamba wabunge ndio wamekuwa wa mwisho kudai posho ya TZS 200,000 kwa kikao. Tetesi ni kwmba kuna GN ambayo ilipitisha posho hizi mwaka jana, na nafikiri Pinda aliposema Rais amesaini, alimaanisha waraka huo.
Nakumbuka tangu mwaka jana humu tumewahi kujadili kuhusu serikali kutumia gharama kubwa kwenye mambo yasiyo ya msingi tukiwa tunaangalia hali ilivyokuwa inaendelea katika nchi za ulaya ambazo zilifikia hatua ya kupunguza mishahara kwa wafanyakazi wa serikali (mfano Ugiriki na Hispania) ili kukabiliana na hali hiyo

Sisi hapa pamoja na kuwategemea hao wanaokata matumizi tukakalia kutumia pesa hovyo na kuongezeana miposho ya kipumbavu na sasa leo tuna suffer
 
Mwendo ni KINDUGAI NDUGAI tu, kila mtu atangulize tumbo, taifa baadaye(Bumpkin Billionare wa JF).

Sahihi yangu ni poa sana. Kuna mwingine ana nyongeza?
 
Nimekuwa nafuatilia vikao vya bunge kwa kipindi sana hasa katika bunge hili lililoanza mwaka 2010 ambalo limekuwa linakaribiana na changamoto kubwa nadhani kuliko mabunge yote yaliyowahi kutokea. Katika hali hii uongozi imara ni jambo kubwa kabisa lilikuwa linahitajika ambapo wote mtakuwa mashahidi kwamba ulionekana kutokuwepo katika vikao vya mwanzo vya bunge hili.

Hali naona kama imeanza kurekebika kidogo hasa kwa Naibu Spika ambaye naona kadri siku zinavyokwenda amekuwa akibadilika kwa mtazamo chanya kiasi cha kuanza kuaminiwa kwa uongozi wake. Napenda nikiri kwamba kwa Spika mwenyewe bado hajaonyesha hivyo na pia kwa wenyeviti (Hasa yule mwenyekiti ambaye mara zote akiongoza anaondoka na balaa)

Kwa ufupi napenda niseme kwamba naanza kumuamini naibu spika na nakuwa na imani ya kikao kwenda salama pale anapokuwa anaongoza bunge


Ni mtazamo wangu tu................
Nakushauri na kukusihi sana tambua nguvu ya jamii kwanza badala ya kumkubari huyo pimbi kwani baada ya jamii kumcheka na kumdharau popote alipo onekana ndipo kaamua kusikiliza ukweli ukoje na kuanza kujifunza toka wakomavu wa cdm; na hayo ndo mabadiliko mnayoyaona kwa huyo mnamwita Ndugai mie namwita pimbi kwa ujinga alokuwanao hapo awali. Kumbuka tabia haipotei.
 
Back
Top Bottom