Naanza kuiona haja ya "semina elekezi"

Naanza kuiona haja ya "semina elekezi"

SONGOKA

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
1,836
Reaction score
1,845
Mawaziri, wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya wamepanic, tena wamepanic vibaya, na matokeo ya kupanic huko wanafanya maamuzi ya kukurupuka na yanayovunja haki za bunadamu.

Mara huyu kawatia ndani watendaji (Kinondoni), mara huyu kawalazimisha watu kufanya kazi bila likizo(Moshi), mara huyu kawalazimisha watendaji kukaa chini kwenye darasa lenye vumbi eti ili wajue watoto wakikaa inakuwaje (Rorya), kila kukicha ziara za kushtukiza ambazo mwisho wake hatuambiwi zime achieve nini (tena Dar peke yake)

Mara huyu kawafungia watumishi geti, Yaani ni fujo na sifa tu.

Kimsingi kauli ya Mh Rais kuwa wateuliwa wake watajielekeza wenyewe inaleta vurugu huku maofisini. Hawa waheshimiwa wameshindwa kuelewa maana ya 'HAPA KAZI TU' na kimsingi kila mtu ana tafsiri yake.

Bila semina elekezi tutayashuhudia mengi.


Kwa kweli nimeanza kuona umuhimu wa Dkt. Magufuli kuwapa hawa wateuliwa wake semina elekezi, ili wajue ideology hii ya
Mh Rais utekelezaji wake unaendaje..

Nawasilisha..
 
muhimu sana na kwa haraka sana zitumike hela zote hazina jamaa uwezo zero
 
Magufuri kinacho mpa shida nikutaka kujipa uperfect nakutaka kufata mfumo wa mwalimu ambao hauwezekan kwa sasa.
 
Mawaziri, wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya wamepanic, tena wamepanic vibaya, na matokeo ya kupanic huko wanafanya maamuzi ya kukurupuka na yanayovunja haki za bunadamu. Mara huyu kawatia ndani watendaji (kinondoni), mara huyu kawalazimisha watu kufanya kazi bila likizo(moshi), mara huyu kawalazimisha watendaji kukaa chini kwenye darasa lenye vumbi eti ili wajue watoto wakikaa inakuwaje (lorya), kila kukicha ziara za kushtukiza ambazo mwisho wake hatuambiwi zime achieve nini (tena dar peke yake)?? Mara huyu kawafungia watumishi geti ?? Yani ni fujo na sifa tu

Kimsingi kauli ya Mh Rais kuwa wateuliwa wake watajielekeza wenyewe inaleta vurugu huku maofisini. Hawa waheshimiwa wameshindwa kuelewa maana ya ?HAPA KAZI TU? na kimsingi kila mtu ana tafsiri yake. Bila semina elekezi tutayashuhudia mengi .Kwakweli nimeanza kuona umuhimu wa Dr Magufuri kuwapa hawa wateuliwa wake semina elekezi, ili wajue ideology hii ya Mh Rais utekelezaji wake unaendaje

.
Nawasilisha
Kwani haya wanayoyafanya wameyapata wapi kama sio kufuata nyayo za bwana mkubwa wao? Unataka semina elekezi gani? Unategemea rais atawaelekeza nini zaidi ya hayo hayo wanayotenda? Unataka awaelekeze mara ngapi kama ameshawaelekeza kwa vitendo alipofanya hivyo hivyo hazina na muhimbili? Mmeanzaaa!!!!! wakati wa kitwete milisema watendaji ndiyo wabaya yeye akabaki kama malaika! Sasa waziri amewaeleza cha kufanya kwa vitendo watendaji wanatekeleza mnasema awapesemina elekezi!!!! mpaka sasa kuna tofauti gani ya wanayofanya mawaziri na rais? Hapa Kazi tu!
 
Bila Shaka watanzania ni mapopoma. Mntaka kufanya kazi kimazoea
 
Kwani haya wanayoyafanya wameyapata wapi kama sio kufuata nyayo za bwana mkubwa wao? Unataka semina elekezi gani? Unategemea rais atawaelekeza nini zaidi ya hayo hayo wanayotenda? Unataka awaelekeze mara ngapi kama ameshawaelekeza kwa vitendo alipofanya hivyo hivyo hazina na muhimbili? Mmeanzaaa!!!!! wakati wa kitwete milisema watendaji ndiyo wabaya yeye akabaki kama malaika! Sasa waziri amewaeleza cha kufanya kwa vitendo watendaji wanatekeleza mnasema awapesemina elekezi!!!! mpaka sasa kuna tofauti gani ya wanayofanya mawaziri na rais? Hapa Kazi tu!

ndugu hii kurupuka ya wateule wa magufuri wataishia kupelekwa mahakamani na itacost a lot of money. hawafuati utaratibu some of them. ili mradi tu waonekane wanafanya kazi. kazi bila utaratibu ni hatari
 
Darasa ni muhimu,nimeshuhudia waziri mmoja ktk taarifa Itv,akicheza no kama nne,miundombinu,tamisemi,mazingira na kazi.
Division of labour and specialization ni muhimu.
 
Kwani haya wanayoyafanya wameyapata wapi kama sio kufuata nyayo za bwana mkubwa wao? Unataka semina elekezi gani? Unategemea rais atawaelekeza nini zaidi ya hayo hayo wanayotenda? Unataka awaelekeze mara ngapi kama ameshawaelekeza kwa vitendo alipofanya hivyo hivyo hazina na muhimbili? Mmeanzaaa!!!!! wakati wa kitwete milisema watendaji ndiyo wabaya yeye akabaki kama malaika! Sasa waziri amewaeleza cha kufanya kwa vitendo watendaji wanatekeleza mnasema awapesemina elekezi!!!! mpaka sasa kuna tofauti gani ya wanayofanya mawaziri na rais? Hapa Kazi tu!

Yan Hii Ya watendaji kukaa chini imeniacha hoi sana
 
Mmefungiwa nje nini!kwani uliambuwa uje kazini saaa nne?safi sana mimi watu wanakera sana wewe unaenda ofisini kwa mtu saa tatu tena kwa appointment alafu anakwambia nisubiri.niko njiani mkome na mkome chukua na viti vyao na meza kabisa.Semina elekezi za kutokufungia nje.Fanya kazi Dr.
 
Tangu Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania kukaa mwezi mzima bila ya Baraza la Mawaziri na alipotokea kutangaza baraza lenyewe akaacha Wizara nne bila ya Mawaziri ila aliweza kuwapata Manaibu wake. Siku moja baada ya kuapishwa kwake Rais Magufuli akaenda Wizara ya fedha na kukagua Mahudhurio ya wafanyakazi. Tangu hapo serikali yetu kwa sasa imekuwa ni ya kuviziana!

Alipokwenda Muhimbili wengine tulihoji mantiki ya kwenda kule, Maana matatizo ya Muhimbili kama ikifikia yatatuliwe na Rais maana yake Serikali nzima chini yake imeshindwa kufanya hivyo. Lakini yale matatizo yameendelea kuwepo na yataendelea kuwepo kwa kuwa chanzo au kiini cha matatizo yenye hakijashughulikiwa!

Lakini watanzania walikuwa wamechoshwa sana na hali ya ulegevu wa serikali iliyopita, kiasi kwamba kauli mbiu ya "Hapa Kazi" iliwavutia hasa pale walipoona mtoa kauli mwenyewe anapiga "Push Ups" majukwaani. Lakini matatizo yetu haya tuliyonayo hayatatatuliwa kwa mitulinga bali kwa kutumia akili. Hizi "Ziara za Ghafla" "Kufunga mageti" au "kuvamia" ni maonesha ya nguvu walizonazo watawala wetu, lakini si njia mujarabu za kuelekea kwenye lengo la kuwa na serikali Imara na taifa linalojitegemea!!

Kwa mfano tatizo la wagonjwa kulala chini Muhimbili halikuwa ni la vitanda bali aina ya huduma zinazotolewa huko wanakotoka hao wagonjwa wanaolala chini. Kama wagonjwa wote wanaokwenda kwenye Vituo vya Afya, Hospitali za Wilaya, za Mikoa na Hospitali za Rufaa za Kanda madaktari wanawaandikia wagonjwa waende Muhimbili kupimwa kwa kuwa huko tuu ndiko kwenye CT Scan na MRI basi bila shaka kulala chini kutaendelea mpaka pale vifaa hivyo vitakapokuwa kwenye ngazi za wilaya na Mkoa!!

Huu ni mfano mmoja tu ambao unaonesha kwamba hii staili ya kuviziana ambayo Ben Saanane ameiita "Slack Management" haina tija hata kidogo, ni staili ya kutaka wengine waumbuke na wengine waonekane ni wachapa kazi, itatuvuruga tu wala haitatutoa hapa tulipo. Kama tunataka kuendelea nayo Muasisi wake bado yupo, tumpe kazi na ataifanya kwa ufanisi sana. Augustine Lyatonga Mrema!!
 
Last edited by a moderator:
tumsapoti Rais wetu afanye kazi nzuri. najua ana mapungufu yake. kinachotakiwa ni kishirikiana na yeye.
 
Mmefungiwa nje nini!kwani uliambuwa uje kazini saaa nne?safi sana mimi watu wanakera sana wewe unaenda ofisini kwa mtu saa tatu tena kwa appointment alafu anakwambia nisubiri.niko njiani mkome na mkome chukua na viti vyao na meza kabisa.Semina elekezi za kutokufungia nje.Fanya kazi Dr.

hujui ulisemalo mama
 
Kurupuka, fungia nje maana wana maneno sana utawakuta wanasema nilikuwa namzidi darasani, mara alinyakwa mwaka wa ngapi fungia nje kata kilimilimi mpaka tuheshimiane
 
Nimesoma mpaka hapo ulipoandika swala la kupiga push-up nikagaili. Unaonekana moja kwa moja we ni wa kupuuzwa kwasababu huna kitu muhimu sana kichwani
 
Kurupuka, fungia nje maana wana maneno sana utawakuta wanasema nilikuwa namzidi darasani, mara alinyakwa mwaka wa ngapi fungia nje kata kilimilimi mpaka tuheshimiane

acha chuki binafsi wewe, ukizidiwa darasani ndo unashangilia ujinga
 
Pole mkuu wangu kumbe na wewe wamekufungia nilikuwa nasemea wale wasema ovyo wanaojivunia degree zao wewe si mpole tu tunakuonaga kule maskani
acha chuki binafsi wewe, ukizidiwa darasani ndo unashangilia ujinga
 
Back
Top Bottom