Naanza kuamini alichoniambia Dr. Dre

Naanza kuamini alichoniambia Dr. Dre

Junior Rutashoborwa

JF-Expert Member
Joined
Oct 13, 2019
Posts
228
Reaction score
211
Hi everyone in here,

Kuna siku kwenye college yetu kulikuwa na concert, miongoni mwa wanamziki waliokuja ni the legend Dr. Dre. Baadae baada ya tamasha, nilipata fursa ya kukutana nakuongea naye sana kuhusiana na mstakabali wa muziki wa Afrika.

Dr. Aliniambia kuwa kwa asilimia kubwa wana-muziki wa Afrika wameacha kutumia vionjo vya nyumbani na kuiga vionjo vya nje. Kitu ambacho kimefanya muziki wa afrika uonekane kama copy ya muziki wa ulaya na marekani au Asia.

Wana-muziki wengi wa Afrika hawana ubunifu (Creativity and innovation) katika industry.

Unakuta muimbaji, nyimbo zote anatumia chord progression moja. Mbaya zaidi key inabakia ile ile. Yaani muziki unakua hauna ladha hata kidogo.

Kwa upande wa mashairi ndio unakutana na uharo wa maharage. Yaani unakuta msanii mmoja akiweka mstari unasema " Mapenzi yamegeuka shubiri" basi kula mtu ataweka. This is uncreative!

Watayarishaji wanasample beats au instruments za wenzao bila kuwa na kibali chochote kile. Kwa hali hii unadhani wataendelea kudai hatimilki kwa kazi zisizo na originity zao?

Leo wimbo wa mdogo wangu ambaye huwa namshauri kwa mengi Harmonize umefungiwa Youtube, eti kisa amesample beat ya wimbo wa King kaka ft. Kristoft na Magic Enga ujulikanao kama Dundaing.

Binafsi nimeumia sana. Sio kwa sababu wimbo wa mdogo wangu umefungiwa ila nimehuzunika kwa sababu muziki wa leo hauna ubunifu hata kidogo!

Ukiangalia anaedai kaibiwa beat naye amesample beat kutoka kwa Olomide wimbo wa Motigbana. Sasa kwa mwendo huu muziki utaendea?

Binafsi natamani sana niwekeze kwenye muziki wa nyumbani kwa kufungua label kubwa Afrika ila naogopa kuingia hasara.

Maana naweza shitakiwa na makampuni makubwa kama ya Sony Music au Universal kisa wasanii nitakao wasajiri wameiba vionjo vya wasanii wao.

Wasanii badilikeni. Jaribuni kuwa wabunifu. Mnapocopy kazi za watu mnatuvunja moyo wadau wa muziki wa Afrika tulio na nia ya kuongoza njia.

Jambo Tanzania.
 
Hizi ni mbwembwe za kihaya.
Lakini content zako ziko poa sana. Umeandika ukweli mtupu. Bongo kutoka kimuziki ni suala la ujanja ujanja mtupu
Tusiposema Afrika yetu itapotea.

Masada zetu wanabadili rangi. Na wasanii watu wanaimba tamaduni za nje.
 
Nataka nifanye utafiti naye kofi olomide kasampo kwa nani
 
Nataka nifanye utafiti nae kofi olomide kasampo kwa nani
Fanya hivyo mkuu.
Ukifanikiwa anzisha thread kisha unitag ili namimi nianze kusample wasanii ntakao wasajili kwenye label yangu kama nilipata kibali cha ukoo kuianzisha.
 
Da jamaa chai yako umechanganya na muarobaini imekuwa chungu mno, huyo Dr Dre ulikutana nae hospitali ya Bugando au?
 
Nadhani kuna watu wapo kazini kudeal na Harmonize. Tumeshuhudia copies nyingi sana bila ya huu uduanzi uliofanyika!!
 
Masikini wa imani na pesa.
Umezungumzi jambo la ukweli. Muziki huu wa sasa mtu kama mimi huwa sishughuliki nao kabisaa! Hata nikisikia sijui Diamond, Kiba au nani sijui anapiga bure siwezi kwenda.

Ila nikisikia zile nyimbo za zamani za akína Jangwa Music, Msondo, Simba Wa Nyika, Safari Trippers huwa naburudika sana. Sasa nipoteze muda wangu kusikiliza nyimbo za Diamond kwanini wakati naweza kusikiliza mwanamuziki mkubwa mwenye nyimbo nzuri mara kumi elfu?

Hao wanamuziki wa Bongo wataendelea kuchuma kutokana na wabongo wengi ni fuata mkumbo na hawana exposure.
 
Kama umewalenga wasanii basi ungevurumisha hili jiwe huko twitani!! Ungewagonga wawili/ watatu, wamejaa huko wanazodoana
 
big up!
Hawa ni watu wa kucopy na kupaste,halafu utasikia nina ziara kwenda OMAN huku akijimwambafai!!
Watz bhana!!
 
Back
Top Bottom