Mzungu ni kama maji huwezi kumkwepa

Mzungu ni kama maji huwezi kumkwepa

Phillipo Bukililo

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2015
Posts
18,473
Reaction score
13,629
Ukimkwepa mzungu kwenye utalii utakutana nae pale ambapo unahitaji kuweka rada nne nchi nzima kimkakati.

Ukimkwepa mzungu kwenye suala la kilimo cha kisasa, utakutana nae kwenye suala zima la watalii ambao wakija kwa wingi pato la taifa linaongezeka.

Ukimkwepa kwenye utalii utakutana nae kwenye suala la wataalam mbalimbali wa afya.

Namuongelea mzungu kwa maana ya mtu mweupe na makandokando yote aliyonayo.

Ninaipenda sana hii jeuri ya awamu ya tano, ya kwamba sisi tunaweza, ni waafrika wachache sana ambao wanajengana kisaikolojia kwa kuambiana kuwa wanaweza.

Lakini aliyeiumba asili aliumba ile hali ya binadamu na viumbe vingine kushirikiana na kutegemeana.

Kwa muafrika (mtanzania) mzungu hakwepeki ni kama maji vile. Usinawa uso asubuhi mchana utayanywa kabla ya kula. Usipoyanywa utayahitaji jioni kwa ajili ya kuoga.

Matamko yanawakilisha mtazamo wa kiuongozi, lakini uhalisia ni kwamba no man is an ireland. Hayupo mwenye jeuri ya kujitegemea pasipo kupata ushirikiano wa mwingine.
 
Leo umefufukia wapi?! au umeamkia "Ufipa"?!
au katika zile "zilizokatwa" kuna baadhi zilikuwa zinaenda L7?!?(
 
Ukimkwepa mzungu kwenye utalii utakutana nae pale ambapo unahitaji kuweka rada nne nchi nzima kimkakati.

Ukimkwepa mzungu kwenye suala la kilimo cha kisasa, utakutana nae kwenye suala zima la watalii ambao wakija kwa wingi pato la taifa linaongezeka.

Ukimkwepa kwenye utalii utakutana nae kwenye suala la wataalam mbalimbali wa afya.

Namuongelea mzungu kwa maana ya mtu mweupe na makandokando yote aliyonayo.

Ninaipenda sana hii jeuri ya awamu ya tano, ya kwamba sisi tunaweza, ni waafrika wachache sana ambao wanajengana kisaikolojia kwa kuambiana kuwa wanaweza.

Lakini aliyeiumba asili aliumba ile hali ya binadamu na viumbe vingine kushirikiana na kutegemeana.

Kwa muafrika (mtanzania) mzungu hakwepeki ni kama maji vile. Usinawa uso asubuhi mchana utayanywa kabla ya kula. Usipoyanywa utayahitaji jioni kwa ajili ya kuoga.

Matamko yanawakilisha mtazamo wa kiuongozi, lakini uhalisia ni kwamba no man is an ireland. Hayupo mwenye jeuri ya kujitegemea pasipo kupata ushirikiano wa mwingine.

Ukishasimama unaweza kuwa na jeuri kubwa kama nchi za China, Russia sisi bado kidogo unashirikian nao lazima kwa sasa.

Hata kama hupendi kitu usiwatangazie, weka mikakati kuona hakifanyiki. Lakini usiwashtue kwa nguvu.

Matamko yakifanywa nchi zote za Africa labda kutakuwa na nguvu fulani lakini mmoja mmoja mwisho wa siku watakupata sehemu fulani na vikwazo vyao.
 
wengi wao wametupanda vichwani . itabidi tuwarudishe na hio meli waliokuja nayo 🚢😡😡😡😡😡
 
Ukishasimama unaweza kuwa na jeuri kubwa kama nchi za China, Russia sisi bado kidogo unashirikian nao lazima kwa sasa.

Hata kama hupendi kitu usiwatangazie, weka mikakati kuona hakifanyiki. Lakini usiwashtue kwa nguvu.

Matamko yakifanywa na zote za Africa labda kutakuwa na nguvu fulani lakini mmoja mmoja mwisho wa siku watakupata sehemu fulani na vikwazo vyao.
Ila kwa mambo yanayopingana na Misingi ya mila zetu hayo lazima tupinge hata kama ni nchi moja moja.Mengine tutaendelea kuwa nao.Sisi si Kisiwa na hatuna technologia kama ulivyosema.tatizo la kufanya kimya kimya ni kuwa unaweza minywa kimya kimya vilevile.Bora sababu za kuminywa kwako ziwe wazi
 
Wewe umeona mbali,usisahau na kwenye majanga mbalimbali bado mzungu anahtajika!
Miaka ya nyuma pale mgodini Bulyanhulu kiliharibika kifaa cha process plant. Ikabidi mtaalam aitwe kutoka Canada.

Yule mzungu alikuja Dar na mbwa wake. Siku ya kwenda mgodini kwa ndege ilipokaribia akawaambia jamaa wa KMCL kwamba ni lazima mbwa wake awe na kiti chake ambacho ni kile cha pembeni yake.

Basi ikabidi mzalendo mmoja apangiwe ndege ya Jumapili ili kiti chake kiweze kukaliwa na mbwa wa yule mtaalam siku ya Alhamisi.

Huyo ndio mzungu aliyeichora ramani yote ya Afrika wakati muafrika akiwa hajui nini kinaendelea pale Berlin.
 
Mkuu kupambana na Mzungu hakuhitaji makelele.
Kupambana na Mzungu kunahitaji akili na mipango na sio kelele za uzalendo kila kona.
Lakini swali moja muhimu la kujiuliza hivi kwanini tunapambana na Mzungu?, hivi hatuwezi kuendelea mpaka tupambane na Mzungu? wale wote walioendelea walipambana na Mzungu?

Malysia, Singapore, Indonesia, Newzealand, South korea, Misri, Moroco, Tunisia, Nigeria, Kenya, Ghana, Brazil, India nk hawa wote wanapambana na Mzungu?
Binafsi nafikiri tumekosa maarifa tunajaribu kutafuta wa kumpa lawama ili chama fulani kiendelee kutawala kwa kuonyesha watu kimeshindwa kwa sababu ya wazungu.
Wakenya wametuzidi kwenye mambo mengi kiuhalisia maana wao hawana rasirimali nyingi kama tulizonazo lakini wameweza kufikia uchumi wa kati na miundombinu pale Nairobi na Mombasa angalau ni ya kiwango fulani, pia wanatuzidi kwa mbali kwenye mzunguko wa kifedha kwenye miji yao mikubwa lakini sidhani kama wao walifika huko kwa kupambana na Mzungu.
 
Miaka ya nyuma pale mgodini Bulyanhulu kiliharibika kifaa cha process plant. Ikabidi mtaalam aitwe kutoka Canada.

Yule mzungu alikuja Dar na mbwa wake. Siku ya kwenda mgodini kwa ndege ilipokaribia akawaambia jamaa wa KMCL kwamba ni lazima mbwa wake awe na kiti chake ambacho ni kile cha pembeni yake.

Basi ikabidi mzalendo mmoja apangiwe ndege ya Jumapili ili kiti chake kiweze kukaliwa na mbwa wa yule mtaalam siku ya Alhamisi.

Huyo ndio mzungu aliyeichora ramani yote ya Afrika wakati muafrika akiwa hajui nini kinaendelea pale Berlin.

hahahahahaahaha dog ilibidi apewe siti,uzuri wake umeona uhalisia hapo bulynhulu kwenye kifaa cha process plant, Mzungu hayo yalikuwa malingo juu ya yeye kuwa expart kwenye taaluma yake ambapo hata wewe ungeweza kuyaleta kama ungekuwa unajua kitu fulani deeply kiasi cha watu kukuhitaji na kukutafuta na sio utaalamu tu wa kawaida ambao kila mtu anao..
 
Mkuu hizo scoop hapo bulyanhulu, hizo ventilation za hewa underground, cage ya underground na maisha ya kule underground na mfumo mzima wa uendeshaji wa mgodi UNAFIKIRI LEO HII TUKIWAPA WAZALENDO WA UDSM WAANZE WENYEWE KWA KUTUMIA ELIMU YAO NA MAKARATASI YAO WANAWEZA KUUTENGENEZA ULE UHALISIA KUANZIA, OPERATIONS, SAFETY, MANAGEMENT nk?
 
Bado hatujafikia pahala ambapo dunia inatuhitaji kuliko sisi kuihitaji dunia, kifupi leo Tanzania na watanzania tusipokuwepo dunia hakuna itakachokuwa imepoteza ila sisi wenyewe watanzania ndio tutakuwa tunachakupoteza kwa kuiacha dunia...

Tuache jeuri, tujipangie mikakati yetu ya siri, tujiwekee malengo yetu ya siri, tuanze kutenda wenyewe kwa siri, Dunia itaona matokeo tu na kuanza kutuheshimu.
 
Mkuu hizo scoop hapo bulyanhulu, hizo ventilation za hewa underground, cage ya underground na maisha ya kule underground na mfumo mzima wa uendeshaji wa mgodi UNAFIKIRI LEO HII TUKIWAPA WAZALENDO WA UDSM WAANZE WENYEWE KWA KUTUMIA ELIMU YAO NA MAKARATASI YAO WANAWEZA KUUTENGENEZA ULE UHALISIA KUANZIA, OPERATIONS, SAFETY, MANAGEMENT nk?
Ni mpaka sayansi ya kwetu ikawa na uwezo wa kuwa na mifumo yote ya pale Bulyanhulu ndipo tutakapoweza kumlete jeuri mtu mweupe.

Vinginevyo hatuna ujanja, hatuwezi kumkwepa mtu mweupe. Tutapiga kelele lakini akiminya sehemu moja tu jasho linatutoka.
 
Hivi smart phone ya JPM sio ya mzungu kweli?

Hahahahaa wanayo kazi ya kupambana na mzungu maana hata matumbo yao yakivimba wanakimbilia kwa mzungu kutafuta tiba huko😂😂😂
 
Ni mpaka sayansi ya kwetu ikawa na uwezo wa kuwa na mifumo yote ya pale Bulyanhulu ndipo tutakapoweza kumlete jeuri mtu mweupe.

Vinginevyo hatuna ujanja, hatuwezi kumkwepa mtu mweupe. Tutapiga kelele lakini akiminya sehemu moja tu jasho linatutoka.

Mkuu science yetu yapo mambo inacover kabisa lakini bado tunakwama, mfano wataalamu wa mining tunao, mageologist tunao, civil engineer's wapo,mechanicla engineer's wapo, electrical engineer's wapo, production engineer's wapo, chemical processor wapo, procurement specilist wapo, logistics expert wapo, wahasibu wapo, watu wa finance wapo, watu wa marketing wapo, hao watalaamu wetu wote wanatoka chuo bora kabisa UDSM aka mlimani.
 
Kuna jamaa anasema muda si mwingi hawa wazungu atawakopesha hela.
 
Back
Top Bottom