Mzozo wa Congo, kwanini mchokozi asiwajibishwe?

Hapa unatudanganya sana, kagame hawezi kuwa kama putin hapa EAC, kagame ni muasi kama waasi wengine waliojichukulia madaraka kibabe kwasababu walikuwa na dhamana katika jeshi la rwanda pia ukiangalia mfumo wa rwanda ni tofauti na kwetu Tanzania, wakati rwanda inajitafuta kujitawala Tanzania alishashiriki vita nyingi sana la ukombozi wa bara la afrika, wanyarwnda wengi wanakubali jitihada za JWTZ katika kutuliza vita nchini kwao na kagame kujitoa msituni kupewa nchi ktk makubaliano yaliofanyika arusha. Kagame analeta vijana wake hapa nyumbani kufunzwa ktk nyanja mbalimbali pia ukumbuke Tanzania ndio nchi pekee yenye intelijensia mama ukanda wa afrika mashariki. Tanzania inawqtu ambao imewahifadhi tayari ya violence ili amani ya nchi iendelee kuwepo Tanzania imekuwa mfano wa kuigwa ktk jumuiya ya madola kwenye ushiriki wa ulinzi wa dunia pia ukiongelea silaha kila taifa linanunua silaha pia kutokana na sababu za kiusalama nchi kama nchi haiwezi kuexpose kila aina ya silaha inayomiliki. Rwanda haiwezi na kamwe haina ubavu wa kujaribu kutumishiana misuli na mtanzania au hata mkenya au mganda mbaya zaidi huko burundi kuna vita ya ujasusi baina ya rwanda na burundi na warwanda wengi wanapoteza maisha yao ndani ya ardhi ya ndayishimiye. Paul kagame hawezi kumzonga evariste kama ilivyokuwa kwa nkurunzinza anamjua ni mtu wa aina gani. Hivyo kabla hujamfananisha muasi na jasusi uwe na evidence nzito za kutetea hoja yako
Huu ujinga unaaminiwa tu na wajinga wasiokuwa na exposure.
Weka facts and figures za nchi zote za EA community kuhusu intelijensia ili tulinganishe manake iseje ikawa hauna facts bali umekuwa brainwashed au una uzalendo uchwara wa kuogopa kukataa ukweli.
Ukienda kidunia(tumi Google au Wikipedia au reliable sources zozote) nchi zinalinganishwa kwa facts hata kwenye mambo ya intelijensia.
 
Hakuna mtu asiyekuwa na jema hata moja. Kudhani kuwa mtu anaweza kukosa jema kabisa ndiyo ukichaa wenyewe sasa.
Najua kuwa hata saa mbovu kuna muda inakuwa iko sahihi lakini ukichaa ni kuitumia kama reference.
 

You're very right, wanamuogopa lakini hawawezi kuyanena hayo hadharani. Hako kanchi kadogo lakini matata.
Miaka kadhaa nyuma nikiwa Dubai tulikuwa tunapiga story na Waarabu wanasema 'hako ka Israel kadogo sijui kwanini tusikavamie tukakadhibiti kakaacha kuwaburuza Palestinians', it's the same shit I'm seeing our EA zone.
Sasa na huyu hako ka nchi unakokasema ndio kapo nyuma yake ataacha kuwa na kiburi?
 
Congo ni nchi yenye jeshi matako kabisa linakera na halistahili kuwa na hata one star General mmoja. Ukiwaona wanavyopigana wanadai mapigano makali ila ukifuatilia ni kwamba M-23 wakifanya movement hao FARDC wanaondoka eneo hilo bila heavy resistance.
Kazi ya M-23 ni kutangaza tunaenda kuvamia eneo hili, wakishajitokeza na kufyatua risasi mbili tatu FARDC kazi yao ni kuretreat. Jeshi gani linapigana kwa retreat kuliko advancement.

Na serikali ya DRC ni walaini. Muda ambao Felix kawa Rais unamtosha kabisa kuwa ameshika madaraka ipasavyo na akiamua jambo political will inaenda kwa moyo mmoja. Sababu za deko wanazotoa Congo kushindwa ni upuuzi tu.

Abiy Ahmed pale Ethiopia alikaa miaka michache tu akawasoma kwanza kisha ghafla akaondoka mamluki, Tigrayans walivyojifanya wanaleta armed resistance aliwanyoosha mara moja. Hapo kaingia hamna silaha za kutosha ila kafanya procurement ya haraka sana. Uturuki, UAE, China wamempa drones tofauti, kanunua artillery na silaha ndogondogo hata za Iran. Ile vita aliyopigana ni heavy na Tigrayans wanajua vita ya kisasa sio hawa M-23. Wamekufa watu maelfu na mamilioni wamehamishwa makazi ila uamue moja nchi isambaratike kwa kuendekeza upuuzi au ulazimishe serikali iheshimiwe na nchi ibaki na utengamano.

Congo haihitaji silaha za hata $1 billion kuanzisha operation ya maana. Ground attack jets zenyewe wanazo tatu tu Su-25, drones hawana, artillery za maana hawana. Sijui priority yao hao lala lala ni nini.

Kwani Mali Republic ina hela gani kushinda DRC, mbona inafanya procurement ya maana na training ya nguvu na waasi inawatandika ipasavyo. Congo sio nchi ya kushindwa na mamluki wa Uganda na Rwanda kwa pamoja, ni uwendawazimu wao tu jeshi la kukata mauno bora hata mgambo wetu.

Vita inayoshindikana kwa kupambana inajulikana, na inayoshindikana kwa uzembe inajulikana.

ninaamini wakiwa na hizo SUKOI 15 tu au MIG 15 tu na kutrain askari 5000 tu +vifaru kadhaa vya kirusi na kukodisha wale mamluki 200 tu wanamkalisha Rwanda kwa week moja tu..
 
ninaamini wakiwa na hizo SUKOI 15 tu au MIG 15 tu na kutrain askari 5000 tu +vifaru kadhaa vya kirusi na kukodisha wale mamluki 200 tu wanamkalisha Rwanda kwa week moja tu..
Hawahitaji Su-25 hata moja nyingine, drones tu
 
Katika mizozo yote, kila siku pana mchokozi na mhanga.

View attachment 2497295

Congo imekuwa ikiinyoshea kidole Rwanda siku zote kuwa ndiyo yenye lake jambo kwenye mzozo huu.

"Kulikoni kushindwa kumfunga Paka kengele? "

View attachment 2497475

Tanzania ya Nyerere haikuukubali katu upuuzi wa namna hii. Haikujali ulikuwa ukitokea Saharawi, Palestine, Iraq, Grenada, Mozambique au Vietnam. Tanzania haikuwahi kukaa kimya.

"Mchokozi asiyesikia hutiwa adabu kabla ya maisha kuendelea."

View attachment 2497307

Kulikoni mzozo wa Congo kuwa wa kudumu na kwa miongo zaidi ya miwili sasa, watu wasiokuwa na hatia wakiendelea kutaabika na hata kufa?

Kulikoni wanajeshi kwa maelfu kutoka nje walioko Congo kwa malengo ya kuuzima mgogoro huu kuendelea kuwapo bila ya mafanikio?

Kwanini mtuhumiwa huyu asisimamishwe uanachama EAC japo kwa kuanzia ili kujiridhisha na ikithibitika akafunzwa adabu vilivyo?
Ngoja nikuongezee jambo:
Hivi unajuwa hadi juzi hapa DRCongo walikuwa wamewekewa vikwazo na wakubwa wa dunia wasinunue silaha kokote duniani bila ya ruhusa ya wakubwa?

Hivi, unajuwa, juzi juzi hapa viongozi kadhaa(wawili/watatu) wa nchi za Jumuia ya Afrika Mashariki (EAC), wakawa wanajipiga tuvifua twao na kujiapiza kwamba watapeleka jeshi huko likamalizane na hao waasi? Kumbe, jamaa wanatumia tu jina la Jumuia kwenda kuwalinda hao M23!
Hadi leo M23 anachekelea tu na kuendelea kuteka maeneo ya nchi. Hilo jeshi linaloitwa la Jumuia ya Afrika Mashariki hata risasi moja tu hawajaitumia.

Nchi pekee inayoweza kuumaliza mzozo wake ni Congo yenyewe. Ni lazima wajizatiti na wafanye kazi inayowahusu wao wenyewe. Waache kutegemea watu wengine waje kuondoa matatizo yao.

Hicho kiinchi kinachotafuta kumega nchi za wengine wakishughulikie; bila hivyo wataendelea kulialia tu kama mabinti.
 
Rwanda inaongozwa na Paul Kagame. Huyu Paul Kagame ni Putin wa EAC, anaogopwa na kila kiongozi wa ukanda huu wa Afrika.

Nani atamgusa Kagame?

Huyu mama....kwa jeshi gani? Waliuaws na M23 enzi za JK kama kuku.

Ruto....kwa jeshi gani? Walipukutishwa na wasomali (Alshabab) miaka michache iliyopita

Museveni huyu ni swahiba wa Kagame. Lkn hata hivyo hafui dafu kwa Rwanda. Burundi na na vinchi vingine wala siviongelei
Dah!

Mkuu 'Sex', unamwongelea Kagame wa wapi huyo?

Hata 'uchawa' tunaouongelea Tanzania naona umekupeleka mbali sana.

Au sikukuelewa: hao "M23 enzi za JK," waliopukutisha kama kuku; hivi uliwaokota wapi, au unawatengeneza kichwani mwako?
Ninakushangaa kwelikweli na andiko lako hili leo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom