mzozano: Elimu ya sasa VS ya zamani!

mzozano: Elimu ya sasa VS ya zamani!

Ubora wa elimu unapimwa kwa vitu vingi vinavyochochea taaluma.

Kwanza, ubora na idadi ya waalimu! Tangu nyakati za uhuru tuna walimu wangapi, na ubora wao ni upi! Utabaini kuwa kwa sasa idadi ya walimu inapanda kulingana na ukubwa wa namba ya wanafunzi, lakini pia ubora wa waalimu unaridhisha kutoka kuwa na waalimu wa UPE mpaka kupata waalimu wenye weledi waliopitia mafunzo kamili vyuoni.

Pili, idadi ya shule! Hapa ni mjumuiko wa vyuo vya ufundi, VETA, vyuo vya kati na vyuo vikuu! Bila shaka katika nyakati hizi za sasa idadi ya taasisi za elimu ni nyingi na zinatoa mafunzo kwa wanafunzi wengi. Hivyo elimu imepanda.

Tatu, idadi ya wahitimu. Zamani tulikuwa na wasomi wachache sana. Idadi kubwa ya watanganyika walikuwa mbumbumbu kupita kiasi. Miaka ya karibuni tumefanikiwa kuzalisha wahitimu wengi wenye ujuzi na taaluma mbalimbali kuanzia madaktari, walimu, wanasheria, mafundi, mainjinia, na wengine wengi.

Nne, Ubora wa syllabus na nyenzo za kufundishia. Zamani syllabus zilikuwa duni na mbovu maana malengo ya elimu ya kipindi hicho ilikuwa ni kupata wataalamu wa voda fasta ili kujaza nafasi wazi serikalini na taasisi mbali mbali. Syllabus za kipindi hichi cha sasa zimeboreshwa sambamba na usimikwaji wa nyenzo za kiteknolojia na za kisasa kama vile maabara bora, kompyuta, na mitaala yenye kuchochea maswala ya teknohama na tehama mashuleni.
Well said
 
Hesabu za multiple choice hazina tatizo maana lazima mwanafunzi akokotoe kabla hajachagua jibu! Hivyo, hazina ubaya wowote, na zinamsaidia mwanafunzi kupata accuracy ya majibu.
kwani hawezi kuotea?
 
kwani hizi PhD tunazoziona ambazo kiongozi mmoja aliwahi kuita zinamilikiwa na wapumbavu ni za mwaka gani
 
nilishawahi kufanya mtihani wa multiple choice wa hesabu bila kukokotoa na nikapata zote yani kama unabet kwa kanjibahi vile
 
nilishawahi kufanya mtihani wa multiple choice wa hesabu bila kukokotoa na nikapata zote yani kama unabet kwa kanjibahi vile
Sasa kama hujui hisabati unafikiri utafanya nini zaidi ya kubashiri na kubeti! Hata mimi ningekuwa wewe ningebashiri majibu huku nimefumba macho ili angalau nipatemo tuwili twa kubahatisha.
 
Elimu ya zamani ilikuwa inafaa kwa mifumo ya maisha ya zamani.

Leo kumekuwa na maendeleo makubwa sana kwenye science na technology, lakini sisi bado syllabus zetu ni very old.

Mtoto anakuja kukutana na computer chuoni, wakati huo ofisi zote zinatumia computers, walimu wanaomfundisha std 1 mpaka form 4 hawazijui computer.

Leo hii unategemea ufanisi wake uwe sawa na mtoto aliyeanza kudili na word na excel primary?
 
Aah elimu ya miaka ya 2010's shida kabisa yani mwanafunz wa premary anadaftari takribani 14 af dalasa la 5 now days anafundishwa kubarehe tena mada ipo kwenye stadi za kazi!!!!! bado wazee wetu watajisifu kwa hakika

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ubora wa elimu unapimwa kwa vitu vingi vinavyochochea taaluma.

Kwanza, ubora na idadi ya waalimu! Tangu nyakati za uhuru tuna walimu wangapi, na ubora wao ni upi! Utabaini kuwa kwa sasa idadi ya walimu inapanda kulingana na ukubwa wa namba ya wanafunzi, lakini pia ubora wa waalimu unaridhisha kutoka kuwa na waalimu wa UPE mpaka kupata waalimu wenye weledi waliopitia mafunzo kamili vyuoni.

Pili, idadi ya shule! Hapa ni mjumuiko wa vyuo vya ufundi, VETA, vyuo vya kati na vyuo vikuu! Bila shaka katika nyakati hizi za sasa idadi ya taasisi za elimu ni nyingi na zinatoa mafunzo kwa wanafunzi wengi. Hivyo elimu imepanda.

Tatu, idadi ya wahitimu. Zamani tulikuwa na wasomi wachache sana. Idadi kubwa ya watanganyika walikuwa mbumbumbu kupita kiasi. Miaka ya karibuni tumefanikiwa kuzalisha wahitimu wengi wenye ujuzi na taaluma mbalimbali kuanzia madaktari, walimu, wanasheria, mafundi, mainjinia, na wengine wengi.

Nne, Ubora wa syllabus na nyenzo za kufundishia. Zamani syllabus zilikuwa duni na mbovu maana malengo ya elimu ya kipindi hicho ilikuwa ni kupata wataalamu wa voda fasta ili kujaza nafasi wazi serikalini na taasisi mbali mbali. Syllabus za kipindi hichi cha sasa zimeboreshwa sambamba na usimikwaji wa nyenzo za kiteknolojia na za kisasa kama vile maabara bora, kompyuta, na mitaala yenye kuchochea maswala ya teknohama na tehama mashuleni.

nakuunga nkono mkuu kwa fact ulizotaja! lakini je unataka kusema wanafunzi wa saiv wako vizuri kichwani? inakuaje kasumba hizi wanatupia wanafunzi wa kikazi cha leo kuwa wengi kuwa
hawajui kujielezea wenyewe ila kwenye vyeti tunaona alama nzuri wamepata tu,ila maalifa walioyapata wanashinda kuyatumia
hivyo kuwafanya kuwa wategemezi wa ajira
 
Yaani hapa tatizo kubwa ni wazee wa elimu ya zamani kushindwa kuandaa mazingira mazuri ya vizazi vijavyo..

Kwahio elimu ya zamani ndio ya kipuuzi sana .
Maana ilishindwa kuwafundisha hawa wazee jinsi ya kukiendeleza kizazi cha mbele mwisho wa siku ndio wakatunga maswali ya MCQ kwenye mathematics..

Sent using Jamii Forums mobile app

shukrani mchangiaji!
 
Hesabu za multiple choice hazina tatizo maana lazima mwanafunzi akokotoe kabla hajachagua jibu! Hivyo, hazina ubaya wowote, na zinamsaidia mwanafunzi kupata accuracy ya majibu.
Kusolve hakuna tatizo tatizo ni pale unaposolve Halafu ikagoma kifuatacho ni guessing
 
nakuunga nkono mkuu kwa fact ulizotaja! lakini je unataka kusema wanafunzi wa saiv wako vizuri kichwani? inakuaje kasumba hizi wanatupia wanafunzi wa kikazi cha leo kuwa wengi kuwa
hawajui kujielezea wenyewe ila kwenye vyeti tunaona alama nzuri wamepata tu,ila maalifa walioyapata wanashinda kuyatumia
hivyo kuwafanya kuwa wategemezi wa ajira
Kujieleza kwa namna gani!?? Na ni wangapi hawawezi kujieleza? Na wanajieleza kwa lugha gani? Waliopata elimu ya zamani walikuwa na uwezo kiasi gani wa kujieleza ukilinganisha na waliopata elimu ya sasa?

Ukinijibu hayo maswali tunaweza kupata objectivity ya mizani ya kipimo cha elimu ya sasa na ya zamani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom