mzozano: Elimu ya sasa VS ya zamani!

mzozano: Elimu ya sasa VS ya zamani!

de98

JF-Expert Member
Joined
Aug 13, 2017
Posts
737
Reaction score
760
habari wanajamvi,
hii mada nimeamua kuileta kwenu maana naona kama imekua gumzo huku na kule,
hasa ukimkuta kijana wa zamani alie pata elimu huwa na kasumba za kuwananga (kuwabeza) vijana wa sasa iv 2010's kwa kusema kuwa,
1. Elimu tunayoipata mashuleni na hasa vyuoni haiko deep kama zamani
2. vijana hatujielewi nn tunafanya mashuleni na vyuoni (future yetu hatujui)
3. vijana tuna kalili na sio kuelewa
4. tunasoma kwa kufata mikumbo
5. tuna base na majibu ya juu juu hasa ya kutumia internet
kwako mwana JF huu mtazamo unauchukuliaje!,
karibu katika mada!
 
Elimu ya kileo ni tatizo...watoto wanaletewa hadi hesabu za multiple choice
Hesabu za multiple choice hazina tatizo maana lazima mwanafunzi akokotoe kabla hajachagua jibu! Hivyo, hazina ubaya wowote, na zinamsaidia mwanafunzi kupata accuracy ya majibu.
 
Ha ha ha! Lakini si unasolve kwanza kisha ndiyo unachagua hizo, (A), (B), (C), & (D)?
Eee man...yani watoto wa siku hizi ni empty headed...mtu kamaliza form-four lakini ukimuuliza swali la quadratic equation (form two) anabaki anatoa mboni...na wapo wengi tu
 
Hesabu za multiple choice hazina tatizo maana lazima mwanafunzi akokotoe kabla hajachagua jibu! Hivyo, hazina ubaya wowote, na zinamsaidia mwanafunzi kupata accuracy ya majibu.
Pia hata usahihishaji wa mitihani unakuwa rahisi ukizingatia ongezeko kubwa la idadi ya wanafunzi.
 
Hesabu za multiple choice hazina tatizo maana lazima mwanafunzi akokotoe kabla hajachagua jibu! Hivyo, hazina ubaya wowote, na zinamsaidia mwanafunzi kupata accuracy ya majibu.
Hamna dingi....hivo hesabu zinawafanya watoto wawe wavivu wa kufikiri....kuna mwingine anaweza kuanza kubashiri tu...hivyo hawezi kuwa mkokotozi mzuri
 
habari wanajamvi,
hii mada nimeamua kuileta kwenu maana naona kama imekua gumzo huku na kule,
hasa ukimkuta kijana wa zamani alie pata elimu huwa na kasumba za kuwananga (kuwabeza) vijana wa sasa iv 2010's kwa kusema kuwa,
1. Elimu tunayoipata mashuleni na hasa vyuoni haiko deep kama zamani
2. vijana hatujielewi nn tunafanya mashuleni na vyuoni (future yetu hatujui)
3. vijana tuna kalili na sio kuelewa
4. tunasoma kwa kufata mikumbo
5. tuna base na majibu ya juu juu hasa ya kutumia internet
kwako mwana JF huu mtazamo unauchukuliaje!,
karibu katika mada!
Zote mbwembwe lakini darasa la 7 la 1995 kurudi nyuma lina watu wenye akili,weredi,hekima na busara pia watatuzi wa mambo mengi ya kimaisha kuliko degree ya mwaka 2005 kuja mpaka leo

JAH Rastafari Morning Africa.Trust JAH respect nature
 
Hamna dingi....hivo hesabu zinawafanya watoto wawe wavivu wa kufikiri....kuna mwingine anaweza kuanza kubashiri tu...hivyo hawezi kuwa mkokotozi mzuri
Hata usipopewa multiple choice unaweza kuwa mjinga tu vile vile kama huwezi kukokotoa!! Ndio maana miswaki ya hisabati haijawahi kuisha tangu uhuru.
 
To every General Rule there is an Exception.. Huelewi wewe mwenyewe usigeneralize
 
Hata usipopewa multiple choice unaweza kuwa mjinga tu vile vile kama huwezi kukokotoa!! Ndio maana miswaki ya hisabati haijawahi kuisha tangu uhuru.
Siafiki watoto kupewa hesabu za multiple choice.....
 
Zote mbwembwe lakini darasa la 7 la 1995 kurudi nyuma lina watu wenye akili,weredi,hekima na busara pia watatuzi wa mambo mengi ya kimaisha kuliko degree ya mwaka 2005 kuja mpaka leo

JAH Rastafari Morning Africa.Trust JAH respect nature
Kwani tatizo ni nini mkuu? Degree ya mwaka 1980 ina tofauti gani na degree ya 2017?
 
Zote mbwembwe lakini darasa la 7 la 1995 kurudi nyuma lina watu wenye akili,weredi,hekima na busara pia watatuzi wa mambo mengi ya kimaisha kuliko degree ya mwaka 2005 kuja mpaka leo

JAH Rastafari Morning Africa.Trust JAH respect nature
Maajabu ni kwamba walioandaa syllabus ya sasa hivi wengi wao kama sio wote wamesoma hio miaka unayosema wewe..
Hapo mwenye akili ni nani?

Aliyeandaa syllabus ya kipuuzi (chanzo cha ujinga wote)
Au anayesoma syllabus iliyoandaliwa na wazee wa 80's

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaani hapa tatizo kubwa ni wazee wa elimu ya zamani kushindwa kuandaa mazingira mazuri ya vizazi vijavyo..

Kwahio elimu ya zamani ndio ya kipuuzi sana .
Maana ilishindwa kuwafundisha hawa wazee jinsi ya kukiendeleza kizazi cha mbele mwisho wa siku ndio wakatunga maswali ya MCQ kwenye mathematics..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ubora wa elimu unapimwa kwa vitu vingi vinavyochochea taaluma.

Kwanza, ubora na idadi ya waalimu! Tangu nyakati za uhuru tuna walimu wangapi, na ubora wao ni upi! Utabaini kuwa kwa sasa idadi ya walimu inapanda kulingana na ukubwa wa namba ya wanafunzi, lakini pia ubora wa waalimu unaridhisha kutoka kuwa na waalimu wa UPE mpaka kupata waalimu wenye weledi waliopitia mafunzo kamili vyuoni.

Pili, idadi ya shule! Hapa ni mjumuiko wa vyuo vya ufundi, VETA, vyuo vya kati na vyuo vikuu! Bila shaka katika nyakati hizi za sasa idadi ya taasisi za elimu ni nyingi na zinatoa mafunzo kwa wanafunzi wengi. Hivyo elimu imepanda.

Tatu, idadi ya wahitimu. Zamani tulikuwa na wasomi wachache sana. Idadi kubwa ya watanganyika walikuwa mbumbumbu kupita kiasi. Miaka ya karibuni tumefanikiwa kuzalisha wahitimu wengi wenye ujuzi na taaluma mbalimbali kuanzia madaktari, walimu, wanasheria, mafundi, mainjinia, na wengine wengi.

Nne, Ubora wa syllabus na nyenzo za kufundishia. Zamani syllabus zilikuwa duni na mbovu maana malengo ya elimu ya kipindi hicho ilikuwa ni kupata wataalamu wa voda fasta ili kujaza nafasi wazi serikalini na taasisi mbali mbali. Syllabus za kipindi hichi cha sasa zimeboreshwa sambamba na usimikwaji wa nyenzo za kiteknolojia na za kisasa kama vile maabara bora, kompyuta, na mitaala yenye kuchochea maswala ya teknohama na tehama mashuleni.
 
Back
Top Bottom