Indume
Member
- Apr 11, 2011
- 81
- 36
Uchaguzi wa nafasi ya Mwenyekiti wa mkoa wa Mara uligubikwa na mizengwe mingi kiasi kwamba ikaonekana Jina la Vicenti lilitumika kumdhoofisha Makongoro. Kilichojitokeza ni wapinzani wa Makongoro kudai kuwa Makongoro alikataa kumkana Vicent kipindi cha uchaguzi wa ubunge. Kamati ya siasa mkoa wa Mara ulimtaka Makongoro aibuke na kumkana Vicenti jambo ambalo alikataa a ndipo chuki za kisiasa zikaanza.
Wahasimu wa kisiasa ndani ya CCM wakahakikisha lazima Makongoro atapigwa chini. Rushwa ilitumika na jina la Vicent likitumika kwa madai kuwa CHADEMA ilipenya sana kwa jitihada za Vicenti na Makongoro aliruhusu CHADEMA kushinda.
Kwa hali ilivyo ni kuwa CCM imejimaliza kisiasa mkoa wa Mara maana hata aliyechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa mkoa hana uwezo wa kuunganisa mkoa kisiasa na hivyo kuna mazingira makubwa CHADEMA itashinda majimbo yote mkoani Mara.
Wahasimu wa kisiasa ndani ya CCM wakahakikisha lazima Makongoro atapigwa chini. Rushwa ilitumika na jina la Vicent likitumika kwa madai kuwa CHADEMA ilipenya sana kwa jitihada za Vicenti na Makongoro aliruhusu CHADEMA kushinda.
Kwa hali ilivyo ni kuwa CCM imejimaliza kisiasa mkoa wa Mara maana hata aliyechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa mkoa hana uwezo wa kuunganisa mkoa kisiasa na hivyo kuna mazingira makubwa CHADEMA itashinda majimbo yote mkoani Mara.