Mzimu wa Vicent Nyerere ulimuangusha Makongoro Nyerere

Indume

Member
Apr 11, 2011
81
36
Uchaguzi wa nafasi ya Mwenyekiti wa mkoa wa Mara uligubikwa na mizengwe mingi kiasi kwamba ikaonekana Jina la Vicenti lilitumika kumdhoofisha Makongoro. Kilichojitokeza ni wapinzani wa Makongoro kudai kuwa Makongoro alikataa kumkana Vicent kipindi cha uchaguzi wa ubunge. Kamati ya siasa mkoa wa Mara ulimtaka Makongoro aibuke na kumkana Vicenti jambo ambalo alikataa a ndipo chuki za kisiasa zikaanza.
Wahasimu wa kisiasa ndani ya CCM wakahakikisha lazima Makongoro atapigwa chini. Rushwa ilitumika na jina la Vicent likitumika kwa madai kuwa CHADEMA ilipenya sana kwa jitihada za Vicenti na Makongoro aliruhusu CHADEMA kushinda.
Kwa hali ilivyo ni kuwa CCM imejimaliza kisiasa mkoa wa Mara maana hata aliyechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa mkoa hana uwezo wa kuunganisa mkoa kisiasa na hivyo kuna mazingira makubwa CHADEMA itashinda majimbo yote mkoani Mara.
 
hakuzaliwa kuongoza maisha yake yote; na uongozi si m/kiti ccm mkoa tu anaweza akawa kiongozi sehemu nyingine hata kwenye mambo yake binafsi;
kumlazimisha mtu kusema uongo kwa kulinda cheo chake si ungwana na kama uzuzu vile; kusema uongo mbele ya watu wale wenye umri angalau hata kama wa kwangu tu tulifundishwa si adabu; kwanini tubadilike tunapokuwa wakubwa! kama hiyo ndo sababu ya kukosa umwenyekiti naamin hata yeye atakuwa na amani hata sasa;
 
ccm inanuka uovu kila baya wanafanya wao tu! Sasa nina elimu ya utambuzi, sidanganyiki tenaa!
 
Mimi nafikiri alipomsema mheshimiwa sana wa Loliondo kuwa saiti wanasema aondoke,ndio zengwe likasukwa,au hujui wapinzani wote wa mheshimiwa alihakikisha wanashindwa kwenye chaguzi za CCM,wamelishindwa Joka la Mdimu tu
 
kama ndio siasa za mara hakuna kitu walichofanya!kwa mtu aliyelelewa ktk maadili huwezi kumkana ndugu yako hk nafsi ikijua kabisa unatenda dhabi!kizazi cha Nyerere hakiwezi ingekuwa hii dot com mbona rahisi hata kumkana mama alombeba miezi tisa na kumtoa kwa uchungu!
 
Ya Vincent haikuwa issue sana sema matumizi ya dau kubwa na shinikizo la kambi ya rushwa ya mtandao viliamua nani mshindi kwenye uchaguzi huo.
 
Kama Makongoro ameanguka kwa sababu aligoma kumkana ndg yake basi anastahili kuwa mtu wa kuigwa kwa uadilifu wake. Mzee Mkapa aliyewahi kujinasibu kuwa mwanafamilia wa hayati Baba wa taifa alimkana Vicent kwenye majukwaa ya kisisa huko Arumeru akiwaacha Watanzania midomo wazi kwa mshangao. Acha apoteze uenyekiti lakini siyo 'loyalty' kwa familia yake.
 
Back
Top Bottom