Mzee Pinda: Hii Ndiyo Tanganyika tunayoitaka

Mzee Pinda: Hii Ndiyo Tanganyika tunayoitaka

Papa1

JF-Expert Member
Joined
Apr 21, 2012
Posts
2,023
Reaction score
2,218
Nimekuwa nikimsikia Mh. Waziri wangu Mkuu Mzee Kayanza Peter Pinda a.k.a mtoto wa mkulima akiuliza wananchi kwamba ni Tanganyika gani wanaitaka maana anayojua yeye ni ile ya miaka 2 yaani inayoanzia kupata uhuru 1962 na kishia muungano. 1964

Mzee leo nimepata nafasi naomba nikujuze Tanganyika tunayoidai ivue koti la muungano.

Katika miaka ya 1885 – 1890 kulitokea wakoloni kiivamia Afrika ndipo Wajerumani wakafaulu kupata eneo katika Afrika mashariki. Eneo hili lilijulikana na German East Africa.
Bendera ya Ma-Governor wa German East Africa (1898-1919)

VAsbFZrAeKjc1iPVBsbBbrgWJjs1gPFBubxXqg2Ngs1gPFxmaxHig2Nov1QLGxWawHio3NYj1QbGwW64FiY7NYDxQbm8V6oNjYLNYDxcZmsR4oNjaL9UCxsVmsB4qNzWI9UGxsFuuBYmOzWA8UG5vFeqDY2CzWA8XGZrEeqN8Zm2GYB8HGZpgH8j96u3JRfWjpagAAAABJRU5ErkJggg==


Baada ya vita ya 1 ya dunia, mwaka 1919 eneo hilo lilinyang'anywa kutoka koloni la Ujerumani, likagawanywa na kupatikana nchi mpya za Rwanda, Burundi na Tanganyika. Wakati Rwanda na Burundi zikiwa chini ya Wabelijiji (Belgians), Tanganyika iliwekwa chini ya usimamizi wa Mwingereza.

Hii ni Bendera ya Tanganyika 1919–1961
Bwana Kayanza Peter Pinda, Tanganyika tunayoizungunzia ni hii iliyoanzishwa mwaka 1919.
Ndiyo hii ambaye muasisi wetu Mwl. JK Nyerere alizaliwa mnamo mwaka 1922, miaka 3 tu baada ya Tanganyika kuwepo.
Ndiyo hii ambayo Musisi wetu Mwl. Nyerere alikulia na kusoma
Ndiyo hii ambayo Mwalimu aliipigania na kumuondoa mkoloni
Ndiyo hii ambayo kupitia chama cha Tanganyika African Association baadae Tanganyika African National Union ya mwaka 1954 vilikuwa vikiipigania kumuondoa mkoloni.
Ndiyo hii iliyopata uhuru tarehe 9 December, 1961.
QUuKQAAAABJRU5ErkJggg==
4HJ8CBjDZ35CwAAAAASUVORK5CYII=
Z


Tanganyika huru 1961 (Tuitakayo)
Ndiyo hii iliyoungana na Serikali ya Mapinduzi Zanziba mwaka 1964 kuzaa Tanzania
uzR6 6PkGZwAAAABJRU5ErkJggg==
7zWFjNDPjiIAAAAASUVORK5CYII=

Tanganyika ndani ya Muungano 1964 (Tuuenzi na Kuudumisha bila kuvalisha mtu koti)
Ndio hii ambayo Wananchi kupitia Rasimu ya Pili ya Katiba iliyoadaliwa na Tume ya mabadiliko ya Katiba wanataka ivue Koti la Muungano ijitokeze tuione kama tunavyoiona Zanzibar, iache kujificha, haijaiba cha mtu na haina jinai yeyote.
S2M4NwAAAABJRU5ErkJggg==


Mzee Pinda, wewe pamoja na Chama chako hamna haki ya kumbeza Mzee Jaji Joseph Warioba na Tume nzima ya Mabadiliko ya katiba kwakuwa wamewasilisha tulichowatuma kwa mujibu wa sheria.
images
Z
9k=
images

Kama warundi wanavyo jivunia Urundi wao, Wanyaruanda wanajivunia Unyarwanda wao, na sisi kama wenzao waliotokana na German East Africa tunapaswa kujivunia utanganyika wetu bila haya wala kigugumizi.

Mzee Pinda hii ni historia, kama una uwezo wa kuifuta, tupe mbinu, lakini ukweili ndio huo.
Naomba toka leo baada ya kusoma uzi huu hilo swali lako la kwamba tunataka Tanganyika ipi? Ni Hii ya mwaka 1919 ambayo mpaka sasa ina umri wa miaka 95 na si ile ya miaka 2 unayosema ya 1962 - 1964. Hako ni ka kipande tu ka umri wa Tanganyika.

Napenda kukufahamisha Bwana Pinda kwamba Tanganyika iko palepale, iwe koloni au huru, iwe katika Muungano au la, Tanganyika inaendelea kuwepo. Kuvaa koti la Muungano ni jambo la muda tu, Joto likizidi koti linavuliwa Muungano utaendelea na koti lake, Tanganyika itaendelea na T-shirt yake kama ilivyo kwa Zanzibar.

Kuongelea serikali 3 si uhaini na si kuvunja muungano, nikuuimarisha!
Mungu Ibariki Tanganyika, Mungu Ibariki Zanzibar, Mungu Ibariki Tanzania.
 
Afadhalin umemweleza kama alikuwa haijui! Hata ungekuwa mkoa una wilaya zake zenye serikali mbalimbali tangu vijiji, iweje Tanzania izimeze nchi zake zilizoizaa Tanzania? Licha ya kuwepo Mikoa bado wilaya, tarafa, kata, vijiji, vitongoji na mitaa ipo na serikali zipo kila siku zikifanya kazi! Tatizo ni lipi kwa serikali ya Tanganyika tu?
 
Papa1 nimependa unyambulisho wako. Kweli Pinda anakera. Mbona simsikii akisema Zanzibar ipi, au kwakuwa ina-exist tiyari, huko hana hoja? Afundishwe tu somo la historia na uraia, na ilibidi avuliwe kabisa u-PM kwani hajui hata nchi anayoiongoza/simamia.
 
Last edited by a moderator:
Tatizo tulozoea kuishi kwenye uwongo hatuwezi kamwe kuishi kwenye ukweli.Ifikie mwisho wa kutudanganya wadanganyika,Hakuna sababu ya kudanganya umma wa watanzania leo,kila siku watanzania toka bara hawana haki upande wa pili na si hadith bali ni kweli.Ingekuwa vyema kama viongozi wetu wakaliongea hili katika ukweli ili kupata suluhisho la kudumu kwa kutudanganya na kulazimisha kwa vitisho hakutasaidia Muungano.

Na nina uhakika hata wapinzani wanaupenda Muungano lakini uwekwe katika uwazi na usawa wa pande zote mbili.Pande zote za muungano zineemeke na muungano na si vinginevyo.

Viongozi wetu wapendwa vitisho sasa basi tuelezane ukweli,na ukweli huu ujadiliwe na kutatuliwa kwa marithiano.
 
Papa1 asante kwa majibu mazuri.
Hawa watu ni wasomi na wanajua kila kitu tunachokidai ila kwa sababu ya ''USAKA TONGE'' wao wanaamua kujifanya hamnazo!
 
Tanganyika /ˌtæŋɡənˈjiːkə/, from 1962 to 1964 the Republic of Tanganyika, was a sovereign state in East Africa. It was situated between the Indian Ocean and the African Great Lakes of Lake Victoria, Lake Nyasa and Lake Tanganyika. It gained independence from the United Kingdom as a Commonwealth realm on 9 December 1961, becoming a republic within the Commonwealth of Nations exactly a year later, on 9 December 1962. On 26 April 1964, Tanganyika joined with the islands of Zanzibar to form the United Republic of Tanganyika and Zanzibar, a new state that changed its name to the United Republic of Tanzania within a year.
 
Pinda amezaliwa Tanganyika, aangalie cheti chake cha kuzaliwa kimeandikwa nini?
 
Mkuu nashukuru kwa kuifafanua tanganyika kila mwenye sikio amesiki na sikuzote sikio la kufa halisikii dawa sijui kwa nini hilo koti halivuliwi.
 
Ni mwaka 2014 for God's sake iyo Tanganyika ya last century itamkomboaje mwananchi wa kyela anaesombwa na mafuriko leo hii na wengineo wengi.
Tanganyika ipo si lazima iwakilishwe na serikali,
Mbili zatosha, tatu ni karaha tu kwa wananchi kama sisi, kama nyie mnaona ulaji kwenye serikali ya tatu, mkae mkijua wengi tutazidi teseka kwa magharama yasiyokuwa na lazima,
Dai vitu vingine kwa katiba si serikali tatu, it is nonsense to men with common sense.
 
Ni mwaka 2014 for God's sake iyo Tanganyika ya last century itamkomboaje mwananchi wa kyela anaesombwa na mafuriko leo hii na wengineo wengi.
Tanganyika ipo si lazima iwakilishwe na serikali,
Mbili zatosha, tatu ni karaha tu kwa wananchi kama sisi, kama nyie mnaona ulaji kwenye serikali ya tatu, mkae mkijua wengi tutazidi teseka kwa magharama yasiyokuwa na lazima,
Dai vitu vingine kwa katiba si serikali tatu, it is nonsense to men with common sense.

Usiongee kama utumbo hapa, unaposema sarikal 3 ni gharama hebu weka hz gharama za serikal 3 na uweke za serikal 2 halafu utuambie zipi ni kubwa mno!!
Kutoka mawazir 50 na upuuz hadi mawazi 17 ili ni gharama? Fikiria kijana usipende kutumika bure, tuweekee gharama za srkl 2 hapa
 
Tanganyika kwanzaaaaa Zanzibar kwanzaaaaaa tunataka kila 1 iwe nchi kamili hapa serikali 3 tunataka bc
 
Ni mwaka 2014 for God's sake iyo Tanganyika ya last century itamkomboaje mwananchi wa kyela anaesombwa na mafuriko leo hii na wengineo wengi.
Tanganyika ipo si lazima iwakilishwe na serikali,
Mbili zatosha, tatu ni karaha tu kwa wananchi kama sisi, kama nyie mnaona ulaji kwenye serikali ya tatu, mkae mkijua wengi tutazidi teseka kwa magharama yasiyokuwa na lazima,
Dai vitu vingine kwa katiba si serikali tatu, it is nonsense to men with common sense.

Mkuu kwann huwa mnasema 2? Je kwann zisiwe Tanganyika na Tanzania sasa? Iwe kwa zamu kama ni gharama moja ya tosha.
 
Ni mwaka 2014 for God's sake iyo Tanganyika ya last century itamkomboaje mwananchi wa kyela anaesombwa na mafuriko leo hii na wengineo wengi.
Tanganyika ipo si lazima iwakilishwe na serikali,
Mbili zatosha, tatu ni karaha tu kwa wananchi kama sisi, kama nyie mnaona ulaji kwenye serikali ya tatu, mkae mkijua wengi tutazidi teseka kwa magharama yasiyokuwa na lazima,
Dai vitu vingine kwa katiba si serikali tatu, it is nonsense to men with common sense.

Serikali Tatu ni maoni ya wananchi,hizo mbili ni maoni ya nani?Kikwete,Nyerere,au Karume?

MTANGANYIKA DAIMA!
 
Pinda amezaliwa Tanganyika, aangalie cheti chake cha kuzaliwa kimeandikwa nini?

Nani alikuambia wakati huo wakunga na waganga wa jadi wa Katavi walikuwa wanatoa vyeti...wewe vipi? hujui kuwa Pinda ndiyo Mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi ndani ya CCM? ...
 
Papa1 nimependa unyambulisho wako. Kweli Pinda anakera. Mbona simsikii akisema Zanzibar ipi, au kwakuwa ina-exist tiyari, huko hana hoja? Afundishwe tu somo la historia na uraia, na ilibidi avuliwe kabisa u-PM kwani hajui hata nchi anayoiongoza/simamia.

...weee !anaogopa znz kama simba,alisemaga sio nchi wakamtoa kamasi,anachezea huku bara tu ndo maana hata ziara za kule hafanyi...
 
Last edited by a moderator:
Ni mwaka 2014 for God's sake
iyo Tanganyika ya last century itamkomboaje mwananchi wa kyela
anaesombwa na mafuriko leo hii na wengineo wengi.
Tanganyika ipo si lazima iwakilishwe na serikali,
Mbili zatosha, tatu ni karaha tu kwa wananchi kama sisi, kama nyie
mnaona ulaji kwenye serikali ya tatu, mkae mkijua wengi tutazidi teseka
kwa magharama yasiyokuwa na lazima,
Dai vitu vingine kwa katiba si serikali tatu, it is nonsense to men with
common sense.

Kama hoja ni gharama, na tukiongeza serekali ya tatu gharama inaongezeka. Basi tuwe wawazi tuvunje muungano tubaki na serekali moja ya Tanganyika ili gharama ipungue kabisa.
 
Ni mwaka 2014 for God's sake iyo Tanganyika ya last century itamkomboaje mwananchi wa kyela anaesombwa na mafuriko leo hii na wengineo wengi.
Tanganyika ipo si lazima iwakilishwe na serikali,
Mbili zatosha, tatu ni karaha tu kwa wananchi kama sisi, kama nyie mnaona ulaji kwenye serikali ya tatu, mkae mkijua wengi tutazidi teseka kwa magharama yasiyokuwa na lazima,
Dai vitu vingine kwa katiba si serikali tatu, it is nonsense to men with common sense.

...izo mbili ndo zimezuia mafuriko ? Tanganyika ipo ?who is the president of tanganyika ?inawajibikaje kwa masuala yasiyo ya muungano ?mbona tunaona serikali ya muungano inawajibika kwa majukumu ya tanganyika..? Eti ulaji !ulaji wakati unalalamika wananchi wanakufa na serikali yao imezikwa ?nani awatetee ?your common sense needs common sense...
 
Pinda huyu huyu ndiye alisababisha haya,pale alipoulizwa kama Zanzibar ni nchi yeye akasema Zanzibar sio nchi!Baada ya hapo Wazanzibar wakatengeneza katiba yao inayoleta matatizo hadi leo!Arudie tena basi kusema Zanzibar sio nchi!
 
Siasa! Siasa ni kutetea uongo uwe ukweli. Na ukweli kuwa uongo. Kazi kweli kweli.
 
Back
Top Bottom