Mzee Mwinyi asamehewe kwani ameteleza

Mzee Mwinyi asamehewe kwani ameteleza

Unashangaa nini uhuru gani unaousemea? Kukosoa na kukosolewa, kupongeza na kupongezwa... Mtoa mada amekosoa wewe pia hukupenda mawazo yake umemkosoa ndio uhuru huo unaousema ndugu.... Au unasema usichokielewa? Tatizo mnataka kumsifu 'yeye' siku zote hata kama anapotoka.

Bila ya shaka hujaelewa bandiko langu ndugu yangu.....
 
Nimetoa mchango wangu humy jf khs kauli ya Mwinyi. Msio elewa ni kuwa kwa kauli hiyo inaonyesha wazi kuwa watangulizi wa jpm hawakua wazarendo aliogopa kuwakosoa. Sasa kapatikana mzarendo mwenye uchungu na nchi yake Mzee kafurahi sana maana hakuna upigaji tena. Hivyo asingelipenda majizi yarudi tena Ikulu ndo maana ya kusema angelipenda Magufuli atawale milele maana yake majizi yasiludi tena Ikulu. Huyu mzee ana akili sana wala hajateleza. Hakutaka kuwa chafua Mkapa na Kikwete au lini na wapi mliwahi msikia Mwinyi akiwasifia watangulizi wa Magufuri hivyo? Inakupasa kua na akili timamu kuligundua hlo. Big up mzee kweli majizi yasiludi Ikulu.
 
amenena vizuri katiba sio msaafu inaweza kurekebishwa na tukamwongezea mheshimiwa rais wetu mda zaidi miaka 10 naona michache sana kwa kazi kubwa iliyo mbele yake naona angalao aongezewe hata miaka 15 mingine zaidi katiba inabadilishwa tu wapeleke mapendekezo bungeni safi mie presidaa namkubali sana hapa ni kazi tu
 
Wananikera sana hawa wanotaka huyu baba atawale.
Wanamuandaa dictator
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Mzee Mwinyi Ana haki ya kuwaza Tofauti na Mawazo yako

Tena kwa Werevu wake akasema kama SI KATIBA hiyo ilitosha kuwafanya mfikirie Nje ya Box, hakusema ibadilishwe Katiba kasema Kama Si Katiba akimaanisha Katiba iheshimiwe pamoja na utendaji Mzuri wa Rais
 
Mimi huwa nashangazwa na watu wasio pendezwa na maoni ya wengine kana kwamba tuna fikra zinazofanana....!!!

Kwa hiyo mzee Mwinyi hana tena uhuru wa kutoa maoni au uhuru upo kwenye kutoa maoni yanayowapendeza nyinyi.....!!??

Kama ambavyo wewe unapenda maoni yako yaheshimike ingawa wakati mwingine hayapendezi basi na wewe jitahidi kuyaheshimu maoni ya wengine hata kama hayapendezi masikioni mwako...na huo ndio ukomavu........

Uhuru upi wa kutoa maoni unaopiganiwa hapa nchini hali ya kuwa hao wanaopigania huo uhuru hawaheshimu ya wengine.......!??

Akiwa yeye,Mkapa na hata Kikwete hawapaswi kutoa kauli kama hiyo kwani madhara yake yanaweza kuwa makubwa endapo anayeongoza akiamua kuyasikiliza
Hata waongee wakulima wote wa rujewe (kwamfano)
nisinge shituka maana hawana ushawishi wala hawawezi kuchochea uasi.Mimi ninaweza kusema,Kinana,Polepole,Mrema,Lipumba na hata Jecha lakini sio viongozi hao waandamizi pamoja na viongozi wakuu wa dini,ni hatari kwa taifa kwani wao (maranyingi) huwa kama rejea/mifano ya kuigwa na jamii

Nihatari kiongozi mwandamizi akitamani katiba ivunjwe inaweza kuvunjwa

Ninaamini mzee kuna siku ataomba radhi kwa watanzania maana anatujali kuliko anavyojijali yeye,

NASEMA TENA ALITELEZATU NA HAJAANGUKA
 
Unapozidi 90.unakuwa insane. Hapa huwa wanavalishwa hata nepi .Ni dhambi kumruhusu insane aongee. Wachaga tunajua hii.
 
Mzee anazeeka vibaya huyu! Hivi kasema kweli au wanamlisha maneno!? Maana haya MAZUZU YA MACCM si watu wa kuwaamini hata kidogo. Kasemea katika hafla ipi na lini!? Labda ShilawaDU mwenyewe anataka watu wampigie debe ili atawale milele na si ajabu hajiamini ndani ya MACCM 2020 kutokana na kujijengea maadui wengi kuliko marafiki.


Wananikera sana hawa wanotaka huyu baba atawale.
Wanamuandaa dictator
 
Hukumwelewa
Mzee Mwinyi
Wengi hamukumwelewa mzee Mwinyi kwa ile kauli yake juu ya Raisi kutawala milele.
Yule mzee alitumia fasihi ndogo tu.
Kwanza alimsifu Raisi kama kawaida ya tabia yake ya kupongeza pale anapoona inafaa.
Pili ile kauli ilikuwa na maana kuwa.
Pamoja na uongozi mzuri wa Raisi anao uonyesha, kama kutapatikana mrithi baada yake ni vizuri akaendeleza hayo mazuri aliyoyaanzisha Raisi, (yaendelee milele hayo mazuri)
kama yale maamuzi ya kijasiri anayoyafanya.
Kuhusu vipindi vya uongozi Mwinyi aliweka wazi kuwa Raisi hata kama angependa aendelee, au wale wanaopenda aendele, jambo hilo halitawezekana kwani katiba haisemi hivyo.
Kufanya hivyo ni kukiuka katiba hivyo pamoja kuwa mtu atapenda kuendelea kuongoza haita wezekana.
Hebu angalia hii kauli.

"Kama katiba yetu isingetanabaisha ukomo wa uongozi basi ningependa mheshimiwa Rais atawale milele"

Umeona fasihi ilivyotumika hapo.
Kwamba pamoja na mazuri anayoyafanya, katiba ni lazima iheshimiwe.

Kwaherini.
 
Mzee anazeeka vibaya huyu! Hivi kasema kweli au wanamlisha maneno!? Maana haya MAZUZU YA MACCM si watu wa kuwaamini hata kidogo. Kasemea katika hafla ipi na lini!? Labda ShilawaDU mwenyewe anataka watu wampigie debe ili atawale milele na si ajabu hajiamini ndani ya MACCM 2020 kutokana na kujijengea maadui wengi kuliko marafiki.
Kasema kweli jana sikukuu ya eid kwenye swala ya eid. Msikiti sikumbuki lakini nimemsikia kwa masikio yangu akisema kupitia itv
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Kumbe ndio maana alitandikwa kofi msikitini[emoji28][emoji28][emoji28]

Mtoto akiongea neno la kiutu uzima tunasema mtoto anakua

Mtu mzima tena mzee akiongea neno la kitoto tunasema anawehuka!
 
Mzee rukhsa, acha kuvunja katiba. Miaka 10 tu ndiyo katika inavosema.
 
Sasa nimeelewa kwanini yule mufti aliamua kumpiga kofi la dharau huyu mzee
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom