Mzee aliyetuhumiwa kumuua bintiye auawa

kilimasera

JF-Expert Member
Dec 2, 2009
3,068
268
MKAZI wa Kijiji cha Kilembo wilayani Sumbawanga katika Mkoa wa Rukwa, Venance Ntogwa(65) ameuawa na mwili wake kuchomwa moto na wanakijiji wenzake wakimtuhumu kumuua binti yake kwa kumroga.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa,Isuto Mantage amemtaja marehemu kuwa ni Stella Ntogwa (15) ambaye alikuwa mwanafunzi wa Shule ya Msingi Kilembo.

Kwa mujibu wa Mantage mzee Venance ni baba mdogo wa marehemu.

Kamanda Mantage alisema kuwa tukio hilo lilitokea juzi saa saba mchana kijijini humo wakati waombolezaji wakiwa kwenye maziko ya binti huyo aliyefariki dunia ghafla Mei 9 mwaka huu.

Alisema, siku hiyo ya tukio waombolezaji hao wakiwa makaburini kwenye maziko ya marehemu kijijini humo ilianza minong'ono kuwa Venance amemroga na kumsababishia kifo marehemu.

“Chanzo cha mauaji ya mzee Venance ni imani za kishirikina kwani baada ya kifo cha binti huyo ndipo ilianza kusikika minong'ono kuwa kifo hicho si cha kawaida kwamba amerogwa na baba yake mdogo yaani mzee Venance” alisema.

Inadaiwa kuwa baada ya maziko ya marehemu kundi la wananchi lilimvamia mzee huyo na kuanza kumpiga.

Kwa mujibu wa Mantage, ilimlazimu mzee Venance kukimbia na kuingia kwenye nyumba ya mwanawe aitwaye Ibrahim Akilindogo na kujifungia humo kwa usalama wake.

Inadaiwa kuwa, baada ya kujifungia humo waombolezaji hao waliichoma moto nyumba hiyo iliyoteketea ambapo mzee huyo akafia humo na mwili wake kuteketezwa na moto.

Kwa mujibu wa Mantage hakuna aliyekamatwa kuhusiana na mauaji hayo lakini msako unaendelea ili wahusika waweze kukamatwa.
 
Khaaa,bora nimezaliwa kazkazini,watu kule uc hawi ndio upo lakini upuuzi wa kichomana viberiti kushnehii,wanajua shilingi kwa saaana!kwanza hao wauwaji pia ni wanga wamejuaje??? Km muuaji ni huyo dingi mdogo?loooool
 
Back
Top Bottom