Mzee Akilimali achafua hali ya hewa Jangwani amtuhumu Makamu Rais wa Yanga

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,543
108,877
Yule Mzee ' machachari ' wa Klabu ya Yanga Ibrahim Akilimali muda si mrefu akizungumza ' mubashara ' kupitia Kipindi cha Sports Headquarters cha Efm ameamua ' kufunguka ' na kutoa ' Siri ' ya Yanga SC kufanya vibaya kwa kusema kwamba Kaimu Mwenyekiti wa Yanga Ndugu Clement Sanga ndiyo adui namba moja wa Yanga na anaihujumu Yanga.

Aidha Mzee Akilimali amefichua pia ' Siri ' nyingine kwamba ni kweli jana Wachezaji wa Yanga SC waligoma kutokana na ' njaa ' narudia tena ' njaa ' namalizia kwa kusisitiza ' njaa ' ambayo sasa imekomaa kama siyo kuota mizizi hapo Klabuni huku akiwaonea huruma Wachezaji kwa maisha magumu ambayo wanapitia sasa huku wengi wao wakishindia tu Mlo mmoja na wengine wakishindia tu maji.

Mwisho Mzee Akilimali alimlaumu sana Nahodha wa Yanga SC Beki Nadir Haroub ' Cannavaro wa Pemba ' kwamba na Yeye anatumika na Kaimu Mwenyekiti wa Yanga SC Ndugu Clement Sanga katika ' kuihujumu ' Timu yao. Mzee Akilimali amewataka wana Yanga SC wote duniani kusahau kuwa msimu huu Yanga SC itatetea Ubingwa wake huku akiitaka TFF kama wataona inafaa waipe mapema tu Kombe Klabu ya Simba kutokana na kwamba haoni Timu ya Kuizuia katika Kuchukua Ubingwa msimu huu kwa kusema Simba SC imesajili si tu vizuri bali ' Kisayansi ' zaidi kuliko wao Yanga SC ambao wamesajili ' Kiswahili Swahili ' au ki ' hovyo hovyo '.

Jamani wana Yanga SC wenzangu wote duniani huyu Mzee Akilimali siyo kwamba labda ana ' mahaba ' na Simba SC na pengine siyo mwenzetu huyu? Hivi Katiba yetu ya Yanga SC haina ' Kipengele ' cha Kumfukuza Mwanachama ' asiyeeleweka ' kama Mzee Akilimali? Jamani wana Yanga SC wenzangu popote mlipo haraka sana tuandamane ili huyu Mzee ' afukuzwe ' Yanga SC kwani tumeshamchosha.

Nawasilisha.
 
Akilimali akiongea ujue Yanga kuna shida!

Mkuu uko sahihi Yanga SC sasa kuna ' Njaa ' sana kwani jana niliwaona akina Kamusoko na Tshishimbi ' wakigongea ' Soda moja maeneo ya Kinondoni dukani nilisikitika mno sema tu nilikuwa sina Hela ndogo ndogo mfukoni kwani ningemnunulia Tshishimbi nae Soda yake.

Jamani wana Yanga SC wenzangu tufanyeje ili hii ' njaa ' ipungue katika Timu yetu?
 
Kuna pengo yanga naliona la mchezaji mahimu mno...hutuwezi kuchukua ubingwa bila kiungo wetu mbunifu

Yusuph Manji hili pengo bado halijazibwa.

Yafuatayo ni sehemu tu ya mazungumzo mafupi kati ya Nahodha wa Yanga SC Nadir Haroub ' Cannavaro wa Pemba ' na aliyekuwa Mwenyekiti na Mfadhili wa Klabu ya Yanga Yusuph Mehboob Manji baada ya kukutana ile juzi pale Kisutu Mahakamani

Nahodha Cannavaro: Shikamoo Tajiri Manji
Manji: Marahaba Cannavaro vipi mzima?

Nahodha Cannavaro: Mzima tu mdomoni Tajiri ila rohoni kuna masononeko ya kufa Mtu
Manji: Kulikoni tena Cannavaro?

Nahodha Cannavaro: Tajiri huwezi amini sasa ni mwezi wa Nne huu Wachezaji wa Yanga tuna ' njaa ' isiyo na mfano
Manji: Sasa Mimi unataka nifanyeje?

Nahodha Cannavaro: Tajiri tunaomba angalau basi utusaidie tu Hela kidogo kwani kiukweli tunaumbuka hapa mjini
Manji: Yaani Cannavaro kipindi chote nina matatizo si wana Yanga SC wote mlinisusa na leo ndiyo mmeibuka

Nahodha Cannavaro: Ni kweli Tajiri nakiri Kosa kwa niaba ya wenzangu kwani tulidanganywa na baadhi ya Wakubwa
Manji: Mmechelewa sana na hakuna Watu ninaowachukia sasa kama Yanga na Wewe nimekuheshimu tu

Nahodha Cannavaro: Kwahiyo Tajiri nikufuate baadae au?
Manji: Kuna unachonidai?

Nahodha Cannavaro: Njaa Tajiri Manji
Manji: Pambaneni na hali zenu na safari hii mtakula hadi Mende na Mijusi siwasaidii ng'o Wanafiki wakubwa nyie

Nahodha Cannavaro: Dah....sawa Tajiri Manji
Manji: Tena uwaambie na wana Yanga wenzio kuwa msipoteze muda nami na mniache tafadhali. Mtakoma mwaka huu.

OMBI / USHAURI

Jamani wana Yanga SC wenzangu kwa hali hii ya ' njaa ' kali iliyopo kwanini tusifumbe tu macho na twende kwa kupiga hata ' magoti ' Ofisini kwa Tajiri na Mfadhili wa Simba Mo Dewji ili aweze kutusaidia kwa Pesa na ikiwezekana basi na sisi pia tumpe Timu yetu kama ambavyo Simba sasa wanaelekea kumkabidhi Timu?

Nasubiri majibu yenu wana Yanga SC wenzangu kwani hii ' njaa ' naona kila sekunde, dakika, saa na siku inazidi tu Jangwani.
 
Yule Mzee ' machachari ' wa Klabu ya Yanga Ibrahim Akilimali muda si mrefu akizungumza ' mubashara ' kupitia Kipindi cha Sports Headquarters cha Efm ameamua ' kufunguka ' na kutoa ' Siri ' ya Yanga SC kufanya vibaya kwa kusema kwamba Kaimu Mwenyekiti wa Yanga Ndugu Clement Sanga ndiyo adui namba moja wa Yanga na anaihujumu Yanga.

Aidha Mzee Akilimali amefichua pia ' Siri ' nyingine kwamba ni kweli jana Wachezaji wa Yanga SC waligoma kutokana na ' njaa ' narudia tena ' njaa ' namalizia kwa kusisitiza ' njaa ' ambayo sasa imekomaa kama siyo kuota mizizi hapo Klabuni huku akiwaonea huruma Wachezaji kwa maisha magumu ambayo wanapitia sasa huku wengi wao wakishindia tu Mlo mmoja na wengine wakishindia tu maji.

Mwisho Mzee Akilimali alimlaumu sana Nahodha wa Yanga SC Beki Nadir Haroub ' Cannavaro wa Pemba ' kwamba na Yeye anatumika na Kaimu Mwenyekiti wa Yanga SC Ndugu Clement Sanga katika ' kuihujumu ' Timu yao. Mzee Akilimali amewataka wana Yanga SC wote duniani kusahau kuwa msimu huu Yanga SC itatetea Ubingwa wake huku akiitaka TFF kama wataona inafaa waipe mapema tu Kombe Klabu ya Simba kutokana na kwamba haoni Timu ya Kuizuia katika Kuchukua Ubingwa msimu huu kwa kusema Simba SC imesajili si tu vizuri bali ' Kisayansi ' zaidi kuliko wao Yanga SC ambao wamesajili ' Kiswahili Swahili ' au ki ' hovyo hovyo '.

Jamani wana Yanga SC wenzangu wote duniani huyu Mzee Akilimali siyo kwamba labda ana ' mahaba ' na Simba SC na pengine siyo mwenzetu huyu? Hivi Katiba yetu ya Yanga SC haina ' Kipengele ' cha Kumfukuza Mwanachama ' asiyeeleweka ' kama Mzee Akilimali? Jamani wana Yanga SC wenzangu popote mlipo haraka sana tuandamane ili huyu Mzee ' afukuzwe ' Yanga SC kwani tumeshamchosha.

Nawasilisha.
Makosa makubwa yamefanywa na yanga wenyewe kuwaweka karibu wazee kama hawa ambao ni wapenda sifa na wachumia tumboni. Miaka yote yanga ninayoifahamu imekuwa na wazee [kama kina mzee kondo kipatwa n.k] ambao fahari yao kubwa nia kuona timu inashinda. Michango mingi walitoa ya hali na mali lakini kuanzia utoto wangu sijawasikia wakizungumza mambo ya ndani[nyeti] ya klabu hadharani. Hata ule wakati yanga ilipogawanyika na wazee nao kugawanyika sehemu 2 sikuwahi kuwasikia wakizungumza mambo ya ndani ya klabu.
Huyu mzee ni opportunist na Uongozi umempa nafasi. Ametumia nafasi kama hiyo wakati manji anaingia klabu na wengi tunafahamu alipata tijara gani na kila anaponyimwa atakacho amekuwa akiwa tia madoa viongozi hao.
Ushauri wangu kwa uongozi ni kwamba wawasilishe hoja ya tabia ya mzee huyu wakati wa mkutano mkuu wa yanga na wenye mali wafanye kazi ya kutumbua hili jipu pevu. 'Mwana umleavyo ndivyo akuavyo'
 
Kama sio siasa wivu na visasi, MANJI apewe timu aimiliki, tofauti na hapo tutegemee kushuka daraja baada ya misimu miwili au mitatu
 
Makosa makubwa yamefanywa na yanga wenyewe kuwaweka karibu wazee kama hawa ambao ni wapenda sifa na wachumia tumboni. Miaka yote yanga ninayoifahamu imekuwa na wazee [kama kina mzee kondo kipatwa n.k] ambao fahari yao kubwa nia kuona timu inashinda. Michango mingi walitoa ya hali na mali lakini kuanzia utoto wangu sijawasikia wakizungumza mambo ya ndani[nyeti] ya klabu hadharani. Hata ule wakati yanga ilipogawanyika na wazee nao kugawanyika sehemu 2 sikuwahi kuwasikia wakizungumza mambo ya ndani ya klabu.
Huyu mzee ni opportunist na Uongozi umempa nafasi. Ametumia nafasi kama hiyo wakati manji anaingia klabu na wengi tunafahamu alipata tijara gani na kila anaponyimwa atakacho amekuwa akiwa tia madoa viongozi hao.
Ushauri wangu kwa uongozi ni kwamba wawasilishe hoja ya tabia ya mzee huyu wakati wa mkutano mkuu wa yanga na wenye mali wafanye kazi ya kutumbua hili jipu pevu. 'Mwana umleavyo ndivyo akuavyo'
Well said mkuu,mzee anatumika na wasioitakia Yanga mema,Manji kuna vitu anaweka sawa baada ya hapo atarudi kundini,huyu mzee takribani miezi 4 akuwahi kuongea na media yyt kuhusu Yanga,ndani ya wiki baada ya Manji kutoka jela,kishaongea mara 2 na media!
 
Hili ni tatizo watu kung'ang'ania timu, mfumo huo umepitwa na wakati, hivi vizee ni njaa na ndo chanzo cha migogoro, kutwaa kushinda kilabuni. Simba wameanza Yanga fanyeni hima badilikeni. Hakuna mfadhili atakayetoa pesa yake bila faida.
 
Yafuatayo ni sehemu tu ya mazungumzo mafupi kati ya Nahodha wa Yanga SC Nadir Haroub ' Cannavaro wa Pemba ' na aliyekuwa Mwenyekiti na Mfadhili wa Klabu ya Yanga Yusuph Mehboob Manji baada ya kukutana ile juzi pale Kisutu Mahakamani

Nahodha Cannavaro: Shikamoo Tajiri Manji
Manji: Marahaba Cannavaro vipi mzima?

Nahodha Cannavaro: Mzima tu mdomoni Tajiri ila rohoni kuna masononeko ya kufa Mtu
Manji: Kulikoni tena Cannavaro?

Nahodha Cannavaro: Tajiri huwezi amini sasa ni mwezi wa Nne huu Wachezaji wa Yanga tuna ' njaa ' isiyo na mfano
Manji: Sasa Mimi unataka nifanyeje?

Nahodha Cannavaro: Tajiri tunaomba angalau basi utusaidie tu Hela kidogo kwani kiukweli tunaumbuka hapa mjini
Manji: Yaani Cannavaro kipindi chote nina matatizo si wana Yanga SC wote mlinisusa na leo ndiyo mmeibuka

Nahodha Cannavaro: Ni kweli Tajiri nakiri Kosa kwa niaba ya wenzangu kwani tulidanganywa na baadhi ya Wakubwa
Manji: Mmechelewa sana na hakuna Watu ninaowachukia sasa kama Yanga na Wewe nimekuheshimu tu

Nahodha Cannavaro: Kwahiyo Tajiri nikufuate baadae au?
Manji: Kuna unachonidai?

Nahodha Cannavaro: Njaa Tajiri Manji
Manji: Pambaneni na hali zenu na safari hii mtakula hadi Mende na Mijusi siwasaidii ng'o Wanafiki wakubwa nyie

Nahodha Cannavaro: Dah....sawa Tajiri Manji
Manji: Tena uwaambie na wana Yanga wenzio kuwa msipoteze muda nami na mniache tafadhali. Mtakoma mwaka huu.

OMBI / USHAURI

Jamani wana Yanga SC wenzangu kwa hali hii ya ' njaa ' kali iliyopo kwanini tusifumbe tu macho na twende kwa kupiga hata ' magoti ' Ofisini kwa Tajiri na Mfadhili wa Simba Mo Dewji ili aweze kutusaidia kwa Pesa na ikiwezekana basi na sisi pia tumpe Timu yetu kama ambavyo Simba sasa wanaelekea kumkabidhi Timu?

Nasubiri majibu yenu wana Yanga SC wenzangu kwani hii ' njaa ' naona kila sekunde, dakika, saa na siku inazidi tu Jangwani.
Utatukanwa me simo
 
Back
Top Bottom