mzenjiboy
JF-Expert Member
- Aug 28, 2010
- 907
- 387
CCM inapaswa kumuomba radhi mzee Aboud Jumbe kwa kumnyang'anya madaraka aliyokuwa nayo pamoja na cheo cha urais wa ZANZIBAR hapo 1984. Hayo yalitokea baada ya rais Aboud Jumbe kushabikia suala la serikali tatu jambo ambalo Mw/Nyerere alilipinga kwa nguvu zake zote kisha kumvua Jumbe nyadhifa zake zote. Jaji Warioba kuleta tena suala la serikali tatu katika rasimu zote mbili ya kwanza na ya pili. Hii inathibitisha ya kwamba mzee Jumbe aliona mbali sana na hakukosea kwa kile alichokuwa akikiamini. Kwa hili maCCM muombeni radhi mzee Jumbe.