confidential person
Member
- Feb 11, 2013
- 76
- 7
Mtoto mmoja alitoka shule huku analia kweli kweli hadi alipofika kwao. Baba yake kuona mwanaye analia,ikabidi amuulize kulikoni;
Baba: Unalia nini mwanangu mzuri? Nini kimekusibu huko utokako?
Mtoto:Nimepigwa sana baba,nimeambiwa twende wote shule.
Baba na mwanaye wakaongozana kwenda shule pamoja. Walipofika moja kwa moja wakaingia katika ofisi ya mwalimu mkuu.
Mwalimu: Karibu sana mzazi,mwanao tumemuuliza Nairobi iko wapi,kashindwa kujibu ndio maana tukamuadhibu.
Baba akamgeukia mtoto wake na kumpiga bonge la kibao tena usoni halafu akamwambia;
Baba: Kila siku nakukataza kuchezea vitu vya watu hukomi, haya Nairobi ya mwalimu iko wapi?
RISASI:NOVEMBA 14, 2015.
==========
Kwenu waalimu, na wengineo endapo kama mngekuwa waalimu mngechukua hatua gani hapo?
Baba: Unalia nini mwanangu mzuri? Nini kimekusibu huko utokako?
Mtoto:Nimepigwa sana baba,nimeambiwa twende wote shule.
Baba na mwanaye wakaongozana kwenda shule pamoja. Walipofika moja kwa moja wakaingia katika ofisi ya mwalimu mkuu.
Mwalimu: Karibu sana mzazi,mwanao tumemuuliza Nairobi iko wapi,kashindwa kujibu ndio maana tukamuadhibu.
Baba akamgeukia mtoto wake na kumpiga bonge la kibao tena usoni halafu akamwambia;
Baba: Kila siku nakukataza kuchezea vitu vya watu hukomi, haya Nairobi ya mwalimu iko wapi?
RISASI:NOVEMBA 14, 2015.
==========
Kwenu waalimu, na wengineo endapo kama mngekuwa waalimu mngechukua hatua gani hapo?