Ustaadh
JF-Expert Member
- Oct 25, 2009
- 413
- 19
MKAZI wa Kijiji cha Mohoro amepeleka malalamiko kwa mwenyekiti wa kijiji hicho akiomba apewe ushauri wa nini cha kufanya baada ya mwanawe wa kiume kufaulu mtihani wa darasa la saba wakati hajui kusoma na kuandika.Akizungumza katika kikao cha Kamati ya Maendeleo ya Kata ya Chumbi kilichofanyika juzi katika Kijiji cha Kiwanga, Mwenyekiti wa Kijiji cha Mohoro, Saidi Makwangu alisema kuwa mkazi huyo alifika ofisi kwake akiomba apewe ushauri wa nini cha kufanya baada ya mwanawe ambaye hajui kusoma na kuandika amefaulu.
Makwangu alisema kwa kuwa kikao cha Kamati ya Maendeleo ya Kata kina wataalamu wengi katika fani mbalimbali alitaka apate majibu ya kwenda kumjibu mzee huyo ambaye amekuwa akimfuata kila wakati kupata ushauri.
Nilimjibu kuwa ushauri sina nakwenda kwenye kikao cha WDC nikirudi nitakuwa na majibu, alisema mwenyekiti huyo.
Akijibu swali hilo Mkuu wa Shule ya Sekondari Mohoro ambako mtoto huyo amechaguliwa kwenda Masyanga Mwita alisema kuwa mwanafunzi huyo anatakiwa kuanza masomo yake haraka iwezekanavyo na kama atakuwa hana uwezo mtihani wa kidato cha pili utamuengua.
Mwita alisema kuwa akiwa kidato cha pili atafanya mtihani kwa mara ya kwanza na akifeli atapewa nafasi nyingine ya kurudia na akishindwa atarudishwa nyumbani.
Kumekuwa na madai kuwa wanafunzi wanaomaliza darasa la saba wamekuwa wakipewa majibu na wasimamizi wa mitihani hali inayosababisha baadhi ya wanafunzi kufaulu wakiwa hawana uwezo kitaaluma
Makwangu alisema kwa kuwa kikao cha Kamati ya Maendeleo ya Kata kina wataalamu wengi katika fani mbalimbali alitaka apate majibu ya kwenda kumjibu mzee huyo ambaye amekuwa akimfuata kila wakati kupata ushauri.
Nilimjibu kuwa ushauri sina nakwenda kwenye kikao cha WDC nikirudi nitakuwa na majibu, alisema mwenyekiti huyo.
Akijibu swali hilo Mkuu wa Shule ya Sekondari Mohoro ambako mtoto huyo amechaguliwa kwenda Masyanga Mwita alisema kuwa mwanafunzi huyo anatakiwa kuanza masomo yake haraka iwezekanavyo na kama atakuwa hana uwezo mtihani wa kidato cha pili utamuengua.
Mwita alisema kuwa akiwa kidato cha pili atafanya mtihani kwa mara ya kwanza na akifeli atapewa nafasi nyingine ya kurudia na akishindwa atarudishwa nyumbani.
Kumekuwa na madai kuwa wanafunzi wanaomaliza darasa la saba wamekuwa wakipewa majibu na wasimamizi wa mitihani hali inayosababisha baadhi ya wanafunzi kufaulu wakiwa hawana uwezo kitaaluma