My story

Barua yake ya maombi haijanivutia hata kidogo......nashindwa kutoa msaada. Nna hakika wapo waliovutiwa kwa hiyo watatoa wao msaada
Mkuu Gaijin, sizani kama nilikusudia hiyo kuifanya ni barua ya maombi, but kuelezea nini hasa ninachoomba na nipo ktk mazingira gani. Likewise, nazani jambo la kuangalia si namna gani "barua" inavutia, bali ni kuangalia how need I am! What i am sure of ni kwamba nilichoongea ni true 100%
 
Mkuu, wala siwezi kujisikia vibaya kwa hicho ulichoongea kwani ni kweli yanatokea sana siku hizi. Hata hivyo, nakuhakikishia niliyoongea ni kweli kwa 100%.
 
Pole sana Chige:

Wakati unaomba usaidizi jitahidi kuandika kwa ufasaha: Unapoandika kuwa una Bsc na umefanya kazi miaka mitano, inatakiwa pia unachoandika kiwe kina "reflect" uwezo wako (competence)....

Thanx Baba Enock for ur advice, but i hope nilizitaja my areas of comptence, na kati ya hizo sijataja Lugha(English) na labda ndio maana umeona makosa kibao! Ingawaje kuna waliodhihaki kwanini nimetumia kiingereza, nazani nilifanya jambo la busara zaidi kwani ningejua lini kwamba ni mbovu kiasi hicho!
 

Kwa nini usingekuja na ombi kwa lugha yetu-swahili, mbona inaelekea ni mjuzi wa kujieleza???
Kama magraduates wa Tz kiingereza ndo hiki basi nji yetu maendeleo ni ndoto.Kiingereza kama hiki si cha kujivunia kwa mtu mwenye DEGREE. Anyway pole sana kwa maswahibu yaliyokukuta.
 
chige ............nafikiri hukunielewa, sijafanya dhihaka ya kwa nini umeandika kwa kiingereza. nimeuliza tu kwa nini? labda ulikuwa na maana nyengine.

hata ungeandika kwa kiswahili, ulitakiwa uandike kwa ufasaha na ueleweke kirahisi ili kumshawishi mlengwa kuwa wewe sio tu kuwa una tatizo but you deserve to be helped.

Tunashukuru wasamaria wema wamejitokeza watakaokupatia msaada unaouhitaji na Mungu akufanyie wepesi katika yale unayotaka kuyafanya.
 

Mkuu Mauzauza, ni nani alikuambia kwamba maendeleo yanaletwa na Kiingereza! Hata mimi nilishangaa kwanini hakutumia Kiswahili lakini kwangu haikuwa issue ya kufanya hadi niandike! Hivi pamoja na ubovu wa lugha yake(kama wajuzi wa lugha mnavyosema), hivi ni nani anayeielewa lugha hiyo akashindwa kuelewa alichokiongea Chige! Badilikeni, endapo hamna cha kuchangia ni bora kukaa kimya kwani si lazima kuchangia. Mimi nazani issue yake ni kuomba msaada, hayo mengine sizani kama yatamsaidia!
 
Chige: Ingekuwa vizuri sana kama ungeandika kiswahili.
 
Chige ushauri mdogo
Ni lazima ukae mbagala?
Kama si ivyo hamia maeneo yaliyo karibu na chuo utakachokuwa unasoma.
Pili jibidishe mwenyewe kwa kutafuta kazi manake misaada haijengi na itakufanya uendelee kuwa tegemezi. Swala la kazi si ishu ya kupata siku moja lakini ukiendelea kutafuta kuna siku utapata, na vile vile ukiendelea kutegemea wasaidizi hutopata daima.
 
Na kilimo kwanza yote na uwekezaji wote wa sekta za fedha katika kilimo, ukose kazi .... either u r not serious... or u really messed up!!! somewhere..!! Sorry to lash u out... get out and knock doors and sell ur skills...!!:mad2:
 
  • Kwa elimu uliyonanyo unatakiwa kujua wewe una njia na milango mingi ya kupata ajira kuliko wasiokuwa na matatizo.

  • Ukisema ulipoteza kazi in contradicting way sijakuelewa .Kubali ulifanya kosa au kama ulionewa kuna njia za kisheria.
  • Sijui unatumia njia gani kutafuta kazi. Je kama kweli uko seroi niambie miezi miwili iliyopita umeaomba kazi gani na shirika gani zilizotangazwa.
  • Na sidhani mtu waanayesoma mareketting mwenye shida ya pesa kama laptop ni hitaji muhimu sana.
Otherwise samahani bado sijarizika na maelezo yako naungana na jamaa hapo juu kusema unatania may be unataka kuona response tu na huna shida.

Ushauri wa wangu pia ni Dont see or use ure disability as a weakness, view it as strength. Hope utafanikiwa.
 
Sitaki kuamini kama kamaliza Chuo Kikuu. Hicho kiingereza chake mmmmm. Ndio maana mataifa mengine wanatulalalmikia.
 
Pole Chige, If I may know the location of your college,I might find you a room for that matter for 6 month. This is a Forum,any one can contribute what he think is right for you. Its like you have 10 tapes all giving different quality water-you just choose which you think is clean. All the best!but I did not like"...... that he knows my poor family in and out!most of the members here are from the same class but we are fighting not to belong there again and again. K
 
Sitaki kuamini kama kamaliza Chuo Kikuu. Hicho kiingereza chake mmmmm. Ndio maana mataifa mengine wanatulalalmikia.
Kwani kingereza alichotumia kina shida gani? kwani chuo kakuambia alikuwa ansoma linguistic na phonology ya kingereza. Acha kubeza. Hii ndio standa english ya sisi graduate wengi wa tanzania. Yes ina makosa lakini sio ya kushobokea kiasi hicho.

Na ingekuwa vizuri ukaja na version ya maelezo kama yake ya mtu unayedhani amemaliza chuo kwa standard zako.
 
e bwana huyu jamaa kama anastahili kusaidiwa asaidiwe maswala ya kizungu wengi tumesoma saint kayumba.hao wengine waliosoma saint marry tuwaache bwana.
 
Ee bwana pole sana. Mtu unaweza kuwa na akili sana lakini kwa sababu ama ya kupanik au
vinginevyo ukajikuta unajielezea visivyo. Ndugu zanguni tumpeni ushauri badala ya kuzidi
kumdiscourage zaidi. Mtaan kuna magraduate wengi sana ambao wako jobless sio kwamba hawajui
kiingereza na wala sio kwamba wako disabled, system ya Tanzania iko hivyo hadi sasa bado hatuna ule uthubutu
wa kufanya mambo kama wenzetu. Mini na wewe tunapaswa kushauriana tufanyeje.





[HE WHO KNOWS HE KNOWS HE KNOWS NOT, BUT HE WHO KNOWS HE KNOWS NOT HE KNOWS.
 
Sitaki kuamini kama kamaliza Chuo Kikuu. Hicho kiingereza chake mmmmm. Ndio maana mataifa mengine wanatulalalmikia.
vp ww mbona unaonekana kama hujaenda shule?unamjaji mtu kwamba ameenda shule kwa lugha uko ni kuathiriwa na ukoloni!
 



Your not serious are you?? The experience and qualification ?? Am not even a graduate and I have a job already, Your physical disability shouldn't be a set back to you you can get a better job with what you have already you won't need any sponsors !!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…