My Husband Is Acting Funny ..msaada pls

First lady mwambie huyo dada ambane mumewe amweleze ametoka wapi na akikataa awaite wazee wa pande zote awaeleze. hakuna ndoa ya namna hii jamani na huu ni ubabe wa ajabu sana men kumfanyia wife. Inawezekana kuna vitu alivyotarajia kuviona katika mahusiano yenu baada ya kuoana akaja kugundua ni kawaida tu hakuna kubwa.
 
Jaribu tu kuchakachua Mkwe! haya mambo unaweza kuoa kumbe katika msafara wa harusi Flower girls akakuvutia ukaanza kupanga mpaka wa kuchakachua baada ya harusi

HA HA HA HA mama mkwe nimecheka mpaka basi hizo mbona nimeishakutana nazo kuna mshikaji aliisaliti ndoa yake hivi hivi sababu ya hao FLOWER GILRS NA MAIDS, saa zingine unakuta wako bomba kweli kuliko hata bi harusi ndipo hapo unaanza kuchakachua na usiombe naye ukute ni green light yaani mwendo mdundo
 

hakuna ndoa iliyopo 100% perfect, mwenye hiyo ndoa na anikosoe hapa, hata kama walitokea kwenye ndoa ya namna hiyo hawakuona lolote coz wazazi wao walikuwa wanajua kumaliza mambo yao chumbani wakija sitting room mambo ni mengine.
 

Binti anaonekana anatumia lugha ya upole sana inabidi amkomalie na pia afanye uchunguzi pia wa kujua mume wake anapotoka anaenda wapi maana akizidi kuwa mpole ataletewa mtoto wa mwenziwe lakini hii ndoa itabidi FL1 amuulize huyo bidada vizuri isije ikawa mtu alilazimishwa kuoa hapo matokeo yake ndiyo hayo
 

h haaaaaaaaaaaaaa, sasa contacts za flower girl mnazichukua saa ngapi? ukumbini, kanisani, au ndo kazi ya best man? unamwonyesha tu yuleeeeeeeeeeeee! then anakutafutia kiaina?
 

NOP hakuna ndoa iliyo 100% perfect na kabla ya kuingia unaambiwa purukushani zote hata kabla haujao au kuolewa unaona ndoa za wengine purukushani wanazopata kwahiyo mtu lazima ukae ukijua kuwa expext something negative some day, lakini kuna vitu vingine vinaenda beyond kama hii issue duh si mchezo not even a year
 

Ni kweli The Finest mkwe wangu kuna mmoja tuko nae hapa yeye alioa mdada mrembo wa haja lakini baada ya miaka miwili akaoa tena Flower Girl sasa wana miaka minne kwenye ndoa kila nikimtazama huwa simmalizi hata kidogo
 
Ni muhimu sana kuangalia ni wapi mlikutana je mlipendana kwa dhati kabla ya kuoana au ww ulikua umeficha makucha yako baada ya ndoa ukaanza kuyakunjua?wanaume wanahitaji kubembelezwa dadangu.Vuta subira kumbuka aahdi ulizozitoa kanisani au msikitini wakati mkifungua ndoa.Vumilia mmbembeleze wanaume wadhaifu sana kwa nyie mpe mapenzi ya dhati hata kama akichelewa usimuwekeee uso wa mbuzi.we utaona tu kalegea then mnaongea baada ya hapo mambo yanasonga kama kawaida.
 
h haaaaaaaaaaaaaa, sasa contacts za flower girl mnazichukua saa ngapi? ukumbini, kanisani, au ndo kazi ya best man? unamwonyesha tu yuleeeeeeeeeeeee! then anakutafutia kiaina?

Ha ha ha, FP acha tu ishu nzima inavyochezwa kama vile watu wanavyocheza mchezo wa bao au karata
 
hakuna ndoa iliyopo 100% pefect, mwenye hiyo ndoa na anikosoe hapa, hata kama walitokea kwenye ndoa ya namna hiyo hawakuona lolote coz wazazi wao walikuwa wanajua kumaliza mambo yao chumbani wakija sitting room mambo ni mengine.

si ndo watu wanafikiri wakiwaona mtaani mnavyotabasamu wanadhani mpo 100% perfect. kuna rafiki yangu siku moja aliniambia ananionea wivu sana eti kila anapotuona tupo happy. na hata marafiki wengi wanasema hivyo. sasa mmoja siku akaniuliza hivi huwa mnagombana? nikacheka sana, nikamwambia hata nyumbani (watoto) huwa hawajui kuwa tunagombana lakini huwa inatokea kugombana. ukiona mwnzako kakukwaza tu break ya kwanza chumbani ( huko si ni mtakuja?) unahakikisha hutoki mpaka aingie chumbani umalize hasira zako ndo unatoka nje. maana sometimes ukiwa na hasira hujali nani yupo hapo unaropoka tu
 
lakini wamama ndo kawaida yetu, yanapoanza inabidi ubeg beg ukidhani ndo utamrudisha. kumbe sometimes mijamaa inahitaji kubuluzwa, unakuja kulijua hilo muda umeshapita............. so tusimlaumu sana

ile dizain limtu limelala nje huko akirudi unapiga hadi magoti kumuomba akujulishe alilala wapi....msxssii...nachukia sana, mie bwana cnaga kiporo kwa kweli, tuweke mambo sawa tusonge na maisha ishu za kuuana taratibu czitaki mie...na ndio inafanya baadhi ya wanaume washindwe kuwaheshimu wake zao, mana anajua hata akifika home baada ya cku 4 atabembelezwa aseme alikuwa wapi wakati unajua kabisa ni rafu imechezwa...
 
Ha ha ha, FP acha tu ishu nzima inavyochezwa kama vile watu wanavyocheza mchezo wa bao au karata

kaazi kweli, yaani bi harusi anaona kashikwa mkono saa zooooteeeeee anadhani ndo kapata, kumbe jamaa linamlia timing flower girl! lol!
 

Nyamayao jibu la swali lako hili hapa

Nimejaribu sana kukaa nae chini kuongea Since he doesnt discuss issues wit me as they arise, it gets to a pt whr he explodes, & that normally results in him beating me, squeezing my neck, bruises evywhr. hhhmmmmmmmm, i pray God gives me the strenght to hang on here all the way ..
 
Ni kweli The Finest mkwe wangu kuna mmoja tuko nae hapa yeye alioa mdada mrembo wa haja lakini baada ya miaka miwili akaoa tena Flower Girl sasa wana miaka minne kwenye ndoa kila nikimtazama huwa simmalizi hata kidogo

Doh Doh huyu jamaa mkali naona alimua kufanya kweli na kuvuta kitu ndani kabisa halafu unaweza kukuta huyo flower girl au maid ni rafiki wa karibu wa bibi harusi lakini mtu still anapinduliwa aisee
 

sawa kabisa, hizo fikira colleagues wa mr wanazo sana,ukimpitia jioni kumchukua wanaona kama watu tupo paradise mpaka wanamuuliza kama tumeshawahi hata kukaa nusu saa bila kuchekeana....mwenyewe akinihadithia hivyo ananiambia:"wangejua huyu chizi wangu nikimuazima mtu kwa dk 5 atanical nije nimchukue haraka iwezekanavyo"...naishia kufurahi tu mana anajua ana chizi na ndio chizi anamfanya tusonge na maisha vizuri.
 

mimi na wewe ni sawa kabisa Nyamayao, yaani kabla ya kuliongelea swala mambo mengine hayaendi. napenda kuwa na amani ya moyo wangu, hata ukinidanganya ila tuwe tumeshaliongelea.
 

Tatizo lake kubwa ni kuwa bado anamhesabia huyo mwanamumwe kuwa ni mume wake, akiachana na wazo hilo, atajua la kufanya
 

NO NO NO NO this is too much binti wa watu asivumilie naona kifo kinamnyemelea kama imefikia to that stage:nono::nono::nono::nono: yanayofuata ni mauaji
 
wajameni samahani kidogo hao FLOWER-GIRLS ndo watu gani wajameni?

inawezekana nimeanza ''kuzeeka'' sasa.....!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…