#COVID19 Mwongozo: Wizara ya Afya imetahadharisha kuwa COVID19 bado ipo; tunaishije?

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Aug 7, 2018
625
938
Wakati dunia ikiendelea kupambana kudhibiti mlipuko wa CoronaVirus, Tanzania imetangaza kuendelea kwa shughuli nyingi za kiuchumi na kijamii.

Hii inapelekea Watanzania kulazimika kutafta namna ya kuishi na gonjwa hili miongoni mwetu huku tukiendelea kutimiza majukumu.

Katika mchakato huu, inawezekana kuna watakaopata maambukizi. Hili si mwisho wa maisha, taratibu za kujikinga zinazoshauriwa na Wataalamu wa Afya zifuatwe.

Yafuatayo ni mambo ya kuzingatia kulingana na hali yako

(a) Kwa Mtu anayeumwa/ anayeonesha dalili| Muathirika
Endapo una dalili zinazoashiria umepata maambukizi
  1. Piga namba 199 au fika kituo cha afya cha karibu nawe kwaajili ya matibabu – ni muhimu kufika kituo cha afya endapo unahisi unadalili za Ugonjwa wa Corona ili kuthibitisha na kupata tiba sahihi. Hakikisha hauwaweki watu wengine hatarini uendapo kituo cha afya.
  2. Zingatia kanuni za kujitenga na watu hadi utakapothibitika umepona kabisa ili kuepusha kusambaa kwa ugonjwa kwa watu wengi zaidi (Wanaokuzunguka)
  3. Fuata ushauri wa kidaktari – endapo utathibitika kuwa na Virusi vya Corona ni muhimu kufuata ushauri wa Wataalam
  4. Zingatia kula matunda na vyakula vyenye Vitamin C kwa wingi
  5. Jitahidi kufanya mazoezi
  6. Kutakasa kila anachokishika – unapaswa kutakasa kila utakachokishika ili kusaidia kupunguza kusambaa kwa virusi hivyo
  7. Vaa barakoa na gloves muda wote endapo unaugulia nyumbani ili kuwalinda wanaokuzunguka. Virusi vya Corona vinasambaa kwa vitone vinavyotokana na kukohoa, kupiga chafya ,mafua, kuongea na pumzi. Unapaswa kuvaa barakoa ili kuzuia kusambaa kwa ugonjwa huu.
(b) Kwa Mtu aliyepona na ambae hajawahi kuumwa anapaswa kuzingatia mambo yafuatayo;

3r2eds.jpg
  • Kunawa mikono mara kwa mara kwa sabuni na maji tiririka au kutumia kitakasa mikono
  • Kuepuka kushikana mikono au kugusana/kukumbatiana na watu
  • Kuepuka mikusanyiko na kutoka nyumbani pale inapokua na umuhimu sana
  • Kuvaa Barakoa kila utokapo nyumbani
  • Kufuatilia taarifa na kufuata ushauri wa kiafya unaotolewa na wataalam
  • Kwa yule aliyeumwa na kupona anapaswa kuwaelimisha wengine juu ya dalili za ugonjwa na namna ya kujikinga
  • Kuepuka kugusa macho, uso , pua na mdomo
  • Kula matunda na aina za vyakula vyenye vitamin C
de.jpg
  • Kuongeza umakini na kuzingatia taratibu unapoenda sehemu za umma kama sehemu za starehe, saluni, benki na matamasha mbalimbali
  • Unashauriwa kufanya manunuzi na malipo kwa njia ya kidigitali mfano, Lipa kwa M-Pesa, Tigopesa.
  • Hakikisha unachangamana na watu unaojua mfumo wao wa maisha na kuhakikisha wanafuata taratibu za kujikinga
  • Kufanya Mazoezi
  • Kuosha au kutakasa vitu unavyonunua kabla ya kuvitumia au kuvihifadhi ndani
 
Museveni ameongeza kufunga “LOCKDOWN” kwa siku 21;

Kenya wagonjwa wamefika 2,021,

Burundi Rais, Mke wa Rais na Mawaziri saba ni baadhi ya wagonjwa wapywa!!

Tanzania tumeishinda Corona na hadi sasa nchi nzima tuna wagonjwa wanne (4) tu!
 
Watu wanajiuliza wachukue tahadhari za nini wakati wagonjwa wanaripotiwa kupungua

Nadhani ili kuwa na msisitizo wa raia kuchukua hatua ni muhimu kuweka takwimu hadharani
 
Kwa imani yangu naamini hili janga bado lipo. Hivyo nawashauri wenzangu wote kuwa makini na kuendelea kuchukua taadhari. Lakini pia watu waendelee kutumia dawa za asili zinazoongeza kinga za mwili. Muitikio uliyopo mtaani kwa sasa ni kuwa Coroona imeisha. Watu wanaamini hivyo na tahadhari inachukuliwa na watu wachache.


Tuchukue tahadhari ndugu zangu.
 
Museveni ameongeza kufunga “LOCKDOWN” kwa siku 21;

Kenya wagonjwa wamefika 2,021,

Burundi Rais, Mke wa Rais na Mawaziri saba ni baadhi ya wagonjwa wapywa!!

Tanzania tumeishinda Corona na hadi sasa nchi nzima tuna wagonjwa wanne (4) tu!
Hatari sana mkuu! Ni ujinga kujidanganya kutatua matatizo kwa kujifanya hayapo...Majirani wagonjwa wanazidi kuongezeka wakati kwetu wanapungua na kufikia wanne tu.
 
Kila nchi ina mapokeo yake ya janga hili. Kwa Tanzania, watu wanaendelea na kazi huku wakichukua tahadhari na hekaheka za uchaguzi ndiyo zinazidi kupamba moto kabisaaaa. Kila mtu awe mlinzi wa afya nadhani tutakuwa salama
 
Museveni ameongeza kufunga “LOCKDOWN” kwa siku 21;

Kenya wagonjwa wamefika 2,021,

Burundi Rais, Mke wa Rais na Mawaziri saba ni baadhi ya wagonjwa wapywa!!

Tanzania tumeishinda Corona na hadi sasa nchi nzima tuna wagonjwa wanne (4) tu!
Tuko vizuri
 
Kila nchi ina mapokeo yake ya janga hili. Kwa Tanzania, watu wanaendelea na kazi huku wakichukua tahadhari na hekaheka za uchaguzi ndiyo zinazidi kupamba moto kabisaaaa. Kila mtu awe mlinzi wa afya nadhani tutakuwa salama
Nimeona comment yako ya kwanza aisee,huwa naona nyuzi tu.
============
Ujumbe mzuri.
 
Tangu kutangazwa kuwa maambukizi yanapungua watu wameanza kupuuzia kuchukua tahadhari, hali inayonipa shaka ya kurudi upya kwa maambukizi
 
Kama Serikali ingekuwa inatoa takwimu basi ingekuwa kizazi, takwimu zinazotolewa kwa sasa ni za waliopona tu na wanaoendelea kupata matibabu, hakuna wagonjwa wapya zaidi ya mwezi. Jirani zetu naona wanapigwa ipasavyo na wagonjwa wasio raia wa huko wanarudishwa kwenye nchi zao. Mpaka sasa nikipiga hesabu kwa wagonjwa wa Tanzania waliorudishwa, nashindwa kukubaliana na Takwimu za Tanzania.

Kikubwa ni mtu mmoja mmoja kuchukua tahadhari na kuwalinda wanaomzunguka, naamini tutakuwa salama.
 
Hatari sana mkuu! Ni ujinga kujidanganya kutatua matatizo kwa kujifanya hayapo...Majirani wagonjwa wanazidi kuongezeka wakati kwetu wanapungua na kufikia wanne tu.
Kuna watumishi wa umma wana wake au waume zao wanaugua corona ila wanaogopa kuripoti hospitalini
 
Museveni ameongeza kufunga “LOCKDOWN” kwa siku 21;

Kenya wagonjwa wamefika 2,021,

Burundi Rais, Mke wa Rais na Mawaziri saba ni baadhi ya wagonjwa wapywa!!

Tanzania tumeishinda Corona na hadi sasa nchi nzima tuna wagonjwa wanne (4) tu!

Mkuu ile sentence ya mwisho napendekeza nyongeza ya maneno mawili pale:

Tanzania *bila aibu* tumeishinda Corona na hadi sasa nchi nzima tuna wagonjwa wanne (4) tu!
 
Kama Serikali ingekuwa inatoa takwimu basi ingekuwa kizazi, takwimu zinazotolewa kwa sasa ni za waliopona tu na wanaoendelea kupata matibabu, hakuna wagonjwa wapya zaidi ya mwezi. Jirani zetu naona wanapigwa ipasavyo na wagonjwa wasio raia wa huko wanarudishwa kwenye nchi zao. Mpaka sasa nikipiga hesabu kwa wagonjwa wa Tanzania waliorudishwa, nashindwa kukubaliana na Takwimu za Tanzania.

Kikubwa ni mtu mmoja mmoja kuchukua tahadhari na kuwalinda wanaomzunguka, naamini tutakuwa salama.

Bahati mbaya kuwa pana watu wengi wanawekwa kwenye hatari ambayo wangeweza kuiepuka.

Kama hali ya ugonjwa Dar kwa mfano ingekuwa wazi hata leo, wanaorudi Dar wangebakia mikoani.

Kama hali ya bungeni au Dodoma ingekuwa wazi, wabunge wale kama kilicho wasibu ni matokeo ya huu ugonjwa wangekuwa walibakia salama makwao.

RIP waheshimiwa wabunge wetu. Mmetangulia nasi tupo nyuma yenu.
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom