Mwl. Nyerere: Tanganyika sio sera ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)

Mwl. Nyerere: Tanganyika sio sera ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)

saggy

Senior Member
Joined
Nov 12, 2008
Posts
153
Reaction score
70
Hiyo ni moja ya Nukuu maarufu za Baba wa Taifa ,Hayati Mwl.Julius K.Nyerere miaka ya 1995 wakati harakati za kuzima vuguvugu la " Tanganyika na G55" alipoutaka Uongozi wa chama wa wakati huo kutangaza Rasmi kwam Umma wa Watanzania kwamba Tanganyika Sio Sera ya Chama Cha Mapinguzi . Msingi wa hoja hii ya Mwalimu ndio ya SIRI kubwa sana ambayo Watanzania hawaijui kuhusiana na Muundo wa Muungano wetu,nina imani Waasisi wa Taifa hili na Wazee wangu ,nawaheshimu sana, wanaijua SIRI hii kuu ambayo ndio chimbuko ya mvutano mkubwa sana wa Kisiasa unaoligawa Taifa Letu.

Kwanini Tanganyika Sio Sera ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)?

Tanzania ni ni matokeo ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar mwaka 1964. Nchi hizi mbili zilikuwa na Vyama viwili vya Siasa,Tanganyika – TANU na Zanzibar – ASP. Ukweli ni kwamba, vyama hivi viwili kutoka kwenye Mataifa mawili tofauti vilikuwa na Itikadi na Sera tofauti na swala hili lilidumu kwa takribani miaka 12 na zaidi.Huu ulikuwa ni muungano wa DOLA .

Kwa busara za waasisi wa Muungano Muungano, manamo mwaka 1977 wakaona ili kujenga Muungano ulio Imara na dhabiti ni vyema kuunganisha vyama hivyo (TANU na ASP) ili kuunda CHAMA Kimoja ambacho kitaungana na DOLA (Tanzania) kushika hatamu za uongozi, ndipo CCM kikazaliwa. Sasa basi kwa maana hiyo muhimili wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni Muungano wa TANU na ASP, nje ya Muungano huo hakuna CCM, bali kuna TANU- Tanganyika na ASP –Zanzibar. Nadhani hapo kila mtu anayesoma hii thread ameleewa ni kwanini Mwalimu alisema Tanganyika Sio Sera ya CCM.

Kwa Mantiki hiyo, Muundo wa Serikali Tatu ukipitishwa una maana kwamba,Zanzibar ambao Tayari wana Katiba yao wenyewe wataondoka na ASP na Tanganyika watalazimika kuandika Katiba mpya (ya Tanganyika) na kubaki na chama chao cha TANU na huo ndio utakuwa mwisho wa CCM! Mtu mwenye akili na anayefirkiri sawa sawa atakuwa anaelewa dhima ya Mwl. Nyerere kuunganisha TANU na ASP mwa 1977, ilikuwa ni Kujenga na kuuimarisha Muungano wa mwaka 1964 ili kujenga Taifa imara kabisa ambalo limedumu kwa zaidi ya miaka 50 sasa.Kwa maana hiyo, Serikali TATU ni kuvunja Muungano wa TANU na ASP ambao ulizaa CCM ambayo ndiyo Muhimili wa DOLA.

Tunaomba Waasisi wa TANU na ASP waliopo watumabie nini ilikuwa Sera za ASP na zipi zilikuwa Sera za TANU ambazo ziliunganishwa na kuunda CCM ambayo inashika DOLA ambayo ni Muungano wa Tanganyika –TANU na Zanzibar –ASP.

Kwa maoni yangu,bila kuulewa huu Muungano wa DOLA Na CHAMA natutaweza kujenga hoja ya kuunda Serikali Tatu nchini ya Mwamvuli wa CCM, kuunda Serikali tatu maana yake CCM haipo tena.!!!!Mwalimu Nyerere alionya Jambo hili mapema kwakuwa alijua kuvunjwa kwa Muungano huu utakuwa ndio mwisho wa Chama Cha Mapinduzi.

Hakuna mwana CCM atakayeunga Mkono Serikali TATU hata iweje, kwa maoni yangu na kama yupo AFUKUZWE mara moja kwenye chama maana hiyo siyo sera ya Chama chake.

Nakaribisha Mjadala
 
Tatizo unayatazama hayo katika mfumo wa Chama kimoja ,CCM imesajiliwa kama vyama vingine sasa kamahuko kwa msajili wamewakilisha kuwa wao ni muungano wa vyama viwili inabidi watu wakigawana mbao na wao wajipapatue ,ila Muungano hauvunjiki kama wanavyodai CCM na kutaka waTz wote waamini hivyo ,Muungano utakuwepo na utakuwa more powerfull kuliko unavyoamini ,Kama ulisikiliza majadiliano ya waheshimiwa akina Warioba basi wangekutosheleza .
 
Kwa hiyo busara hizi ziliwaaminisha CCM itatawala milele....ili kuulinda muungano ulio na dhamira ya kichama zaidi na sio dola?

Mahitaji ya dunia yanaenda yakibadilika.....kama Mwl angekuwa hai kwa upepo huu angekubaliana na rasimu iliyopendekezwa kwa maslahi ya taifa. Binafsi sioni ugumu wowote wa CCM kuwepo Zanzibar na Tanganyika....kama kweli dhamira ya umoja ipo mioyoni mwao...kumbuka mwl alikuwa flexible na maono chanya mfano ni pale alipokubaliana na maoni ya wachache waliotaka mfumo wa vyama vingi na kuyakataa maoni ya wengi.

Umeshajiuliza endapo tungeendelea na mfumo wa chama kimoja hali ingekuwaje sasa?.......swali hilo uendelee kujiuliza hali itakuwaje endapo tutaendelea kukumbatia mfumo wa Serikali mbili hali ya kuwa kuna manung'uniko miongoni mwa nchi washirika?
 
Na AZIMIO LA ARUSHA na UJAMAA zilizokuwa sera za msingi za CCM enzi za Mwalimu leo hata makuburi yake hayajulikani yalipo!!!
Muundo wa wa muungano kati ya Zanzibar na Tanzania (bara, I guess) uliofaa au kuonekana unafanya kazi kwa ufanisi katika miaka ya 1960 hadi 1980 huwezi kuutarajia au hata kuulazimisha ufanye kazi kwa namna ile ile kama ulivyokuwa hapo awali.

Utawala bora ni ule ambao pia uko tayari kubadilika kufuatana na nyakati. Nawapongeza sana MaCCM kwa kubadili sera ya kiuchumi-jamii kutoka 'ujamaa' kwenda 'ujapari' (ubepari uchwara) walipoona upepo umebadilika.

Ninawashangaa sana kwanini leo hii wanasita kubadilisha muundo wa muungano pamoja na dalili zote za mabadiliko kuwagongea hodi mlangoni. Bila kubadili muundo wa muungano leo hii ni kuwatengenezea mgogoro mkubwa wajukuu!
 
1.TANU + ASP = CCM

2 . TANGANYIKA + ZANZIBAR = TANZANIA

Kama unakubali No 1 kwanini basi unang'ang'ania S2? Kwa analogy yako hapo juu. tulitakiwa tuwe na S1 na sio S2 wala S3.

Kama kweli CCM is not a great magician of all times waje na hoja ya S1 basi.

Maana Nyerere wakati anazima hoja ya G55 alisema kwamba sera ya CCM ni S2 kuelekea S1
 
Hiyo ni moja ya Nukuu maarufu za Baba wa Taifa ,Hayati Mwl.Julius K.Nyerere miaka ya 1995 wakati harakati za kuzima vuguvugu la " Tanganyika na G55" alipoutaka Uongozi wa chama wa wakati huo kutangaza Rasmi kwam Umma wa Watanzania kwamba Tanganyika Sio Sera ya Chama Cha Mapinguzi . Msingi wa hoja hii ya Mwalimu ndio ya SIRI kubwa sana ambayo Watanzania hawaijui kuhusiana na Muundo wa Muungano wetu,nina imani Waasisi wa Taifa hili na Wazee wangu ,nawaheshimu sana, wanaijua SIRI hii kuu ambayo ndio chimbuko ya mvutano mkubwa sana wa Kisiasa unaoligawa Taifa Letu.

Kwanini Tanganyika Sio Sera ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)?

Tanzania ni ni matokeo ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar mwaka 1964. Nchi hizi mbili zilikuwa na Vyama viwili vya Siasa,Tanganyika – TANU na Zanzibar – ASP. Ukweli ni kwamba, vyama hivi viwili kutoka kwenye Mataifa mawili tofauti vilikuwa na Itikadi na Sera tofauti na swala hili lilidumu kwa takribani miaka 12 na zaidi.Huu ulikuwa ni muungano wa DOLA .

Kwa busara za waasisi wa Muungano Muungano, manamo mwaka 1977 wakaona ili kujenga Muungano ulio Imara na dhabiti ni vyema kuunganisha vyama hivyo (TANU na ASP) ili kuunda CHAMA Kimoja ambacho kitaungana na DOLA (Tanzania) kushika hatamu za uongozi, ndipo CCM kikazaliwa. Sasa basi kwa maana hiyo muhimili wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni Muungano wa TANU na ASP, nje ya Muungano huo hakuna CCM, bali kuna TANU- Tanganyika na ASP –Zanzibar. Nadhani hapo kila mtu anayesoma hii thread ameleewa ni kwanini Mwalimu alisema Tanganyika Sio Sera ya CCM.

Kwa Mantiki hiyo, Muundo wa Serikali Tatu ukipitishwa una maana kwamba,Zanzibar ambao Tayari wana Katiba yao wenyewe wataondoka na ASP na Tanganyika watalazimika kuandika Katiba mpya (ya Tanganyika) na kubaki na chama chao cha TANU na huo ndio utakuwa mwisho wa CCM! Mtu mwenye akili na anayefirkiri sawa sawa atakuwa anaelewa dhima ya Mwl. Nyerere kuunganisha TANU na ASP mwa 1977, ilikuwa ni Kujenga na kuuimarisha Muungano wa mwaka 1964 ili kujenga Taifa imara kabisa ambalo limedumu kwa zaidi ya miaka 50 sasa.Kwa maana hiyo, Serikali TATU ni kuvunja Muungano wa TANU na ASP ambao ulizaa CCM ambayo ndiyo Muhimili wa DOLA.

Tunaomba Waasisi wa TANU na ASP waliopo watumabie nini ilikuwa Sera za ASP na zipi zilikuwa Sera za TANU ambazo ziliunganishwa na kuunda CCM ambayo inashika DOLA ambayo ni Muungano wa Tanganyika –TANU na Zanzibar –ASP
.

Kwa maoni yangu,bila kuulewa huu Muungano wa DOLA Na CHAMA natutaweza kujenga hoja ya kuunda Serikali Tatu nchini ya Mwamvuli wa CCM, kuunda Serikali tatu maana yake CCM haipo tena.!!!!Mwalimu Nyerere alionya Jambo hili mapema kwakuwa alijua kuvunjwa kwa Muungano huu utakuwa ndio mwisho wa Chama Cha Mapinduzi.

Hakuna mwana CCM atakayeunga Mkono Serikali TATU hata iweje, kwa maoni yangu na kama yupo AFUKUZWE mara moja kwenye chama maana hiyo siyo sera ya Chama chake.

Nakaribisha Mjadala

Mkuu nakushangaa sana, vipi unaweza kuchambua jambo ambalo hujalifanyia utafiti wa kutosha, kwani unakiri kutozifahamu hata sera za TANU na ASP. Simple question hivi mfumo wa vyama vingi uliwahi kuwa sera ya TANU, ASP ama CCM, mbona ndio mfumo unao tumika siku za leo. Mkuu sera za vyama si misahafu, sera hubadilishwa kutokana na nyakati. Sera za ujamaa na kujitegemea ziko wapi ndani ya CCM. Sera za ubinafishaji ziko wapi, sera za UPE ziko wapi. Mwalimu alikuwa sahihi kusema kuwa Tanganyika haikuwa sera ya CCM, kwa sababu muundo wa serekali haujawahi kuwa sera ya chama. Chakushangaza ni nyie mnao ng'ang'ania kuwa muundo wa serekali mbili ni sera ya CCM. Mambo mazuri yaliyokuwa sera ya CCM, yaliyo kuwa na manufaa kwa taifa na wananchi kama ujamaa na kujitegemea na na umilikaji wa njia kuu za uchumi kwa uma, elimu bure na tiba bure, zimeachwa hakuna kati yenu aliyetoa povu kuzisemea, ila hili la serekali mbili. Mkuu mpaka unachachamaa kuwa asiye kubali serekali mbili, jambo ambalo halijawahi kuwa sera ya chama, afukuzwe CCM, lazima una maslahi makubwa katika muundo huo wa serekali mbili.
 
Muungano wa serikali 2 au 3 hauna tija. Serikali inayotakiwa na itakayokuwa imara ni moja. Zenji tunagawa mikoa tunaweka wakuu wa mikoa, ikulu ya Zanzibar inabaki kuwa ikulu ndogo kama zilivyo za mikoa period.

Tukifika hapo Tanzania kama DOLA MOJA itaimarika na udugu tunaoimba kila leo utakuwa na mshiko.
 
Muungano wa serikali 2 au 3 hauna tija. Serikali inayotakiwa na itakayokuwa imara ni moja. Zenji tunagawa mikoa tunaweka wakuu wa mikoa, ikulu ya Zanzibar inabaki kuwa ikulu ndogo kama zilivyo za mikoa period.

Tukifika hapo Tanzania kama DOLA MOJA itaimarika na udugu tunaoimba kila leo utakuwa na mshiko.

Ndoto ya mchana kweupe tayari zanzibar ni nchi kamili hilo la kuifanya mkoa ni moja ya ndoto mnazoota mchana hapo lumumba
 
Muungano wa serikali 2 au 3 hauna tija. Serikali inayotakiwa na itakayokuwa imara ni moja. Zenji tunagawa mikoa tunaweka wakuu wa mikoa, ikulu ya Zanzibar inabaki kuwa ikulu ndogo kama zilivyo za mikoa period.

Tukifika hapo Tanzania kama DOLA MOJA itaimarika na udugu tunaoimba kila leo utakuwa na mshiko.

Kwa nini dola hiyo moja isiwe zanzibar na tanganyika tukaigawa mikoa kisha makao makuu ya shughuli zote za serekali zikahamia zanzibar?wazanzibar hatupo tayari kusalimisha identity yetu eti kisa muungano,zanzibar ilikuwepo,itakuwepo na itaendelea kuwepo milele,imemshinda kuifuta zanzbar nyererere mutakuja kuiweza nyie vifuu tundu? zanzibar kwanza,tuachiwe tupumueeeeeeee.....
 
tatizo ulie tuma post ujui ulicho tuma..
cha kukusaidia maana unalazimisha kumchambua mwalimu huku umjui
serekali 3 ni sera ya chadema..kwa manufaa ya kuigawa inchi ili wapate upenyo wa kutawala

serekali ya mkataba nisera ya cuf ili wapate upenyo wa kuendesha dola ..
serekali upepo unapovumia ni sera ya nccr ..mageuz ilikiweza kujulikana zaidi....

ccm sera yake ni kuhakikisha muungano unakuwepo kwa kutoruhusu serekali ya tanganyika au muungano legelege ..
 
Ndoto ya mchana kweupe tayari zanzibar ni nchi kamili hilo la kuifanya mkoa ni moja ya ndoto mnazoota mchana hapo lumumba
Inatakiwa iwe nchi kamili ili muungano uwe kamili.....kuna tatizo hapo?
 
Kwa nini dola hiyo moja isiwe zanzibar na tanganyika tukaigawa mikoa kisha makao makuu ya shughuli zote za serekali zikahamia zanzibar?wazanzibar hatupo tayari kusalimisha identity yetu eti kisa muungano,zanzibar ilikuwepo,itakuwepo na itaendelea kuwepo milele,imemshinda kuifuta zanzbar nyererere mutakuja kuiweza nyie vifuu tundu? zanzibar kwanza,tuachiwe tupumueeeeeeee.....

Hilo nalo neno...ikulu ihamie zenji...wala sina tatizo la ikulu ikae wapi...ninachozungumzia ni muungano kuwa wa nchi moja yenye serikali moja....hata kama itaitwa Zanzibar!....suala siyo jina la nchi, ni aina gani ya muungano!
 
Back
Top Bottom