ameokoka kutoka wapi na kwenda wapi? wewe unasali lutheran ambako tunajua hawajaokoka, sisi wenyewe tulikuwa huko na tunajua usaliji wa huko ulivyo na kwamba hakuna Mungu, unakusanya watu na kuwahubiria, unawaombea sala ya toba na kuwaacha hapohapo wafundishwe mafundisho yaleyale manyonge yasiyookoa, wakusubirie hadi semina nyingine. wokovu ni kitu cha ajabu sana, usipokaa umezungukwa na watu waliookoka hata mwezi humalizi, hata kama ulikuwa na nguvu ya Mungu itanyonywa utakuwa mkavu na utaishi bila Mungu ndio maana lazima uondoke ukaungane na watu wenye imani ya kuokoka, huwezi kusema umeokoka ukaendelea kukaa kwenye imani ya watu wasiookoka. ni nguvu kulielewa hili kama wewe ni mfuasi wa mwakasege.
Kanisa la lutheran halihubiri wokovu, ndio maana bado wanatumia vitabu hata kusali, ile liturgia, katekisimo mtu anasoma na kuwaambia watu amesali, wameibuka watu miaka kadhaa iliyopita, wanafeloship, hawa walikuwa wanafuata desturi za wokovu, na ninafikiri hata mwakasege aliibukia huko (new life in christ), lakini still maaskofu na wachungaji wanawapinga. Malasusa hadi alimsimamisha Kimaro kijitonyama hoja mojawapo ilikuwa ni anatoka kwenye desturi ya kuabudu za kilutheran, wana desturi yao ambayo haipo mbali sanaa na desturi ambayo Martin Luther alitoka nayo Katoliki. hao fellowship wanaokoka wanaabudu na Mungu anaonekana lakini wachungaji wao wanawapinga, maaskofu ambao tunajua wanashinda kwa waganga na wana mambo ya ajabuajabu wanawapinga, wanataka walutheran wabaki kwenye desturi zileee za kuabudu. NDIO MAANA TUNASEMA, hata kama utaokoka na kubaki hapo umepoteza muda, haujaokoka.
kutubu ni kitu kimoja, ila kuuishi wokovu ni kitu kingine. kuuishi wokovu kunahitaji mtu akishaokoka anaanza kulishwa chakula kama cha mtoto amjue Mungu hadi baadaye awe mtu mzima kwenye wokovu. sasa wachungaji na maaskofu wanaokuongozeni hawajaokoka na wewe unahubiria mtu na kumwacha mikononi mwa mchungaji asiyeokoka, unategemea atamfundisha mafundisho ya kuukulia wokovu hadi asimame? kutubu ni kitu kimoja, kuuisho wokovu ni kitu kingine, unaweza kutubu leo kwamba unaokoka, mwezi mmoja tu umekuwa mtoto wa shetani mzuri tu kwasababu haujalishwa chakula, haujachungwa na mtu aliyeokoka. this is the reason tunasema mwalimu wenu interest yake huwa ni kusustain watu watakaokuwa wanampa sadaka akiweka semina, ila sio kuwasaidia waokoke. kulikuwa na tetesi anataka kufungua ministry yake Dodoma kule anakotaka kujenga kambi, hatujui kama ni kweli, angefanya hivyo pengine wale wanaookoka angewabeba yeye mwenyewe akawafundishe mafundisho ya wokovu kuliko kuwatelekeza mikononi mwa watu wasio na chakula cha uzima.
Mwalimu wenu angekuwa amekulia kwenye mafundisho ya wokovu, asingekuja na fundisho la mzaliwa wa kwanza au la ukombozi wa vitu.
HAYA NIMEANDIKA HAUTAELEWA KAMA HAUJAWAHI KUOKOKA, NA WENGI WANASEMA WAMEOKOKA ILA KIUKWELI HAWAJAWAHI HATA KUKUTANA NA MUNGU WAKAFUNULIWA SIRI ZA AINA HII, NA WENGI WANAOGOPA KUSEMA UKWELI HUU KWASABABU MWALIMU WENU ANA WAFUASI WENGI SANA WANAOJIFARIJI KWAMBA WAMEOKOKA KUMBE SIO.