Mwita Waitara, pamoja na kuunga mkono juhudi barabara jimboni kwako ni mahandaki matupu

Kinoamiguu

JF-Expert Member
Nov 29, 2018
10,597
13,094
Wakuu heshima ziwe kwenu.

Huyu mwamba alikuwa mbunge wa upinzani . Aliyechaguliwa na kuaminiwa na watu wa jimboni mwake wakiwemo wale wa kanda maalumu ambao ni wengi jimboni humo.

Alichaguliwa kwa sababu watu waliamini kwenye mabadiliko ya kweli sio ya ki propaganda. Wapo walioumizwa, kufungwa na pengine kuuwawa kwa kulinda kura za mwita. Alishinda
Baada ya muda akautangazia umma kwamba anarejea nyumbani atii kuunga mkono juhudi. Wapo waliomsifia na kumpongeza hata kumpa unaibu waziri kama zawadi au kifuta jasho kwa kazi nzuri aliyoifanya.

Ukisoma mitandaoni utaambiwa wabunge wa upinzani hawajaleta maendeleo majimbini hivyo hawafai hata kuitwa watanzania. aibu ya ubaguzi hii.
Nimekuwa nikipita jimboni kwa muunga mkono juhudi bwana Waitara.

Hali ya miundombinu jimboni humo inatia kinyaa. unashindwa kujua kwamba kweli hili ni jimbo lenye kupakana na uwanja wa ndege wenye mindege ya matrilion au nini.

Barabara zote ni mahandaki matupu kwanini hazitengenezwi wakati mbunge wake ameunga mkono juhudi?

Mwita umeshindwa Dar utaweza Tarime? Hutoshi
 
Uko sahihi kabisa Waitara anajisifu kuisambaratisha chadema ukonga badala ya kujisifu kwa kutimiza yale aliyoahidi kwa wanaukonga ukianzia mombasa,moshi bar,kwa diwani,mkoremba ni mashimo matupu njoo gongo la mboto ,majohe ni mashimo matupu,zunguka kivule ,msongola pote ni mashimo matupu
 
Hiyo barabara ya chanika nusura nigongane na daladala last year.ina mashimo njia nzima.yaani utafikiri si nchi hii
 
Huku katuacha zaidi ya yatima. Ukonga mzima utadhani haipo dsm; kwenye mafrai ova na makorokoro mazuri mno.

Any way tunaomba ccm ukonga& juu msitufanyie viroja sana ! Watia mshawajua tuleteeni anayejielewa. Kuna dada mmoja hapendi kujionesha , anaeleweka mno na ana nia ya ukonga ya kweli ! Yuko serikalini ila katulia na atatufaa. Hawa walevi na wadada wadhulumati wa 5000 tano za vikoba waacheni huko huko baa. Ova
 
ukitoka Airport kuingia machokoroni unaanza kuona mbona serikali haipo huko banana sijui mombasa gongo la mboto to chanika majohe to viwege sijui kitunda sijui mapori gani mengine sijataja ni mahandaki tupu , biashara ya lami nzuri na umeme wa uhakika huko hamna!! kila siku lazima Tanesco wakate umeme machokoroni huko jimbo la Waitara kama wamelaaniwa vile!!

siku moja nilipita njia ya Majohe to Viwege hakuna lami ni kijijini ila eti ni Ilala karibu na Airport ya kimataifa basi gari yangu ikakwama siku mbili kwa tope zito! sikujua kama kuna serikali na mbunge kule!!ndo nimemjua leo!!
 
Kweli kabisa Mimi natokea Mwanagati yaani tuna shida sana ya usafiri magari yapo ya Mwanagati M/Complex na Mwanagati M/Mmoja lkn hayafiki asubuhi yanaaanza kuja saa4 asubuhtunapata shida sana tunatembea kwa mguu mpaka Kitunda utafikiri hatuna mwakiloshi wetu wa kutusaidia kutatua changamoto.
 
Back
Top Bottom