Mwili wa mateka Ran Gvil wapatikana-Huyu ni mateka wa mwisho

Mwili wa mateka Ran Gvil wapatikana-Huyu ni mateka wa mwisho

Echolima1

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2019
Posts
6,929
Reaction score
6,030
WOW. Mara tu mwili wa Ran Gvili ulipopatikana na ulipotambuliwa, wanajeshi wa Israeli walianza kuimba:

"Ninaamini katika kuja kwa Masihi!"

Sasa kazi tu imebaki ni kubonda magaidi wa Hamas na kuwapokonya silaha zao

Rais wa Israeli Isaac Herzog: naye leo hii kasema;

Ran Gvili, shujaa wetu, amerudi nyumbani baada ya siku 843.

Ran, afisa wa polisi wa kikosi maalum, alitoka kupigana kishujaa ili kuokoa maisha mnamo Oktoba 7. Hatimaye, Ran amerudishwa nyumbani kwa familia yake huko Israeli.

Watu wote wa Israeli wameguswa na machozi. Mioyo yetu iko pamoja na wazazi wake, Talik na Itzik, waliopigana vita vya kishujaa na vya heshima ili kumrudisha nyumbani.

Asante kwa wote waliohusika katika operesheni ya kumrudisha Ran nyumbani. Hii ilikuwa operesheni ya umuhimu usiopimika katika kutimiza wajibu mtakatifu wa kuwakomboa mateka.

Baada ya miaka mingi migumu, kwa mara ya kwanza tangu 2014, hakuna raia wa Israeli aliyeshikiliwa mateka huko Gaza. Taifa zima liliomba na kusubiri wakati huu.

Kumbukumbu ya Ran iwe baraka.

IMG_20260126_175815_561.jpg


 
Sasa magaidi wa Hamas wasalimishe silaha zao na wapalestina waache kabisa kujihusisha na vitendo vya kigaidi kwani wameona wenyewe madhara waliyopata na adha wanayoendelea kupata hadi sasa.

Ni vema watambue kwamba ugaidi haulipi. Wamepoteza zaidi ya watu 70,000 kwa sababu za kijinga tu na mwisho wa siku hawajapata faida yoyote ila ni hasara tu. Bure kabisa.
 
Sasa magaidi wa Hamas wasalimishe silaha zao na wapalestina waache kabisa kujihusisha na vitendo vya kigaidi kwani wameona wenyewe madhara waliyopata na adha wanayoendelea kupata hadi sasa.

Ni vema watambue kwamba ugaidi haulipi. Wamepoteza zaidi ya watu 70,000 kwa sababu za kijinga tu na mwisho wa siku hawajapata faida yoyote ila ni hasara tu. Bure kabisa.
Kifo ni ibada
 
Back
Top Bottom