Inside10
JF-Expert Member
- May 20, 2011
- 33,614
- 40,160
Mgombea Ubunge wa Iramba Magharibi na Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Nchemba, amewataka Watanzania kuwapuuza watu wanaosambaza taarifa za uongo mtandaoni kwamba serikali imechapisha fedha kwa ajili ya kufadhili shughuli za Uchaguzi Mkuu ujao.
Amesema taarifa hizo hazina ukweli wowote na zinalenga kupotosha umma pamoja na kuchochea taharuki kisiasa.
Akizungumza kwenye mkutano mkubwa wa kampeni wa Mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, uliofanyika mjini Mpanda mkoani Katavi, Dkt. Mwigulu alisisitiza kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inasimamia kwa umakini masuala ya fedha na uchumi wa taifa.
Amebainisha kuwa serikali ina akiba ya kutosha na haina haja wala mpango wa kuchapisha fedha mpya kama inavyodaiwa.
Dkt. Mwigulu pia alieleza kuwa mchakato wa kuchapisha fedha ni wa kitaalamu, unaohusisha taasisi maalum zenye uwajibikaji mkubwa, hivyo hauwezi kufanywa kiholela.
Kumbuka wakati tukielekea Oktoba 29 kwenye Uchaguzi Mkuu, fyucha ya Tanzania iko mikononi mwako kwa kuhakikisha unashiriki kwa kujitokeza kupiga kura.
Amesema taarifa hizo hazina ukweli wowote na zinalenga kupotosha umma pamoja na kuchochea taharuki kisiasa.
Akizungumza kwenye mkutano mkubwa wa kampeni wa Mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, uliofanyika mjini Mpanda mkoani Katavi, Dkt. Mwigulu alisisitiza kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inasimamia kwa umakini masuala ya fedha na uchumi wa taifa.
Amebainisha kuwa serikali ina akiba ya kutosha na haina haja wala mpango wa kuchapisha fedha mpya kama inavyodaiwa.
Dkt. Mwigulu pia alieleza kuwa mchakato wa kuchapisha fedha ni wa kitaalamu, unaohusisha taasisi maalum zenye uwajibikaji mkubwa, hivyo hauwezi kufanywa kiholela.
Kumbuka wakati tukielekea Oktoba 29 kwenye Uchaguzi Mkuu, fyucha ya Tanzania iko mikononi mwako kwa kuhakikisha unashiriki kwa kujitokeza kupiga kura.