maelezo kuhusu degree ya pili kuwa hakuPata 1st class hayajajitosheleza, rudi katafute evidence uje upya. Pia ilete CV iliyopo kwenye tofuti ya bunge uweke hapa tuone wapi unaposema kadanganya.. Ulete pia CV ya mbowe na lema
Maajabu duniani ni mengi mno, na wanadamu huwa na maajabu ktk kuishi kwao; Bw. Sixgates, wewe ni mtu wa maajabu mengi kweli.
Ndg. Sixgates, umekuwa ni mkosoaji ktk mada iliyoletwa na mtu mwingine na, kwa ufahamu wangu, kama unapinga/kukosoa hoja ya mwenzio basi unatakiwa kuleta hoja yenye ushahidi bila shaka ili kulisadia jukwaa hili na mtoa mada binafsi, na sio kuacha maswali mengi ya nani ni mkweli ktk mada inayojadiliwa.
Wasomi huwa na kawaida ya kutafuta ukweli, na sio kwa njia unayotumia wewe kupinga taarifa alizoleta mwenzio bila ushahidi wowote, hebu badilika kidogo na uonyeshe kuwa wewe umekwenda shule na unatumia akili, na sio miguu, ktk kutoa michango yako.
Mathalani, wewe unapinga taarifa ya digrii ya pili (Masters), unaonyesha unajua lolote, unachotakiwa kufanya ni kuleta ushahidi wa ukweli wa digrii hiyo na sio kumrudisha mtoa mada aende kuleta ushahidi wakati ameshatoa hoja yake. Zaidi, unaonekana kutetea taarifa iliyopo kwenye tovuti ya Bunge, kwanini usiende pale chuo kikuu cha DSM ukapata taarifa sahihi na kutuletea hapa?
Hivyo basi, ukosoaji au kujua kwako juu ya elimu ya Mwigulu, ni wewe kutusaidia kwa kuleta vielelezo na sio kuweka malumbano yasiyokuwa na msingi.
Vile vile, tovuti ya Bunge sio mwisho wa kupata taarifa za watu, maana kuna shule na vyuo walivyosoma hao watu ambapo unaweza kupata taarifa sahihi zaidi badala ya kuja kutoa hoja zisizokuwa za kisomi.
Tubadilike katika akili zetu na badala ya kutumia miguu ktk kufikiri kwetu basi tutumie akili zetu ipasavyo.