kitambiheshima
JF-Expert Member
- May 27, 2013
- 452
- 116
Jana Naibu katibu mkuu wa ccm Mwigulu Nchemba amekabidhi kadi za ccm kwa wanafunzi 200 wa vyuo vikuu Songea, amewapokea wanachama watatu walioihama chadema na kujiunga na ccm.
- Slaa ni mwongo kwa kusema kuwa bomba la gesi linajengwa kuelekea Ulaya.
- Chadema wanapewa fedha na wafadhili wasioitakia mema nchi hii. Amesema kama chadema imekosa fedha za kuitishia kikao cha halmashauri kuu, wamepata wapi fedha za kukodi chopper mil. 40 kwa siku?.
-Ameelezea sababu ya ccm na watanzania wengi kutaka muungano wa serikali mbili kuwa ndiyo muungano wenye maslahi ya taifa. Ametoboa ukweli wa msimamo wa vyama vya upinzani kutaka serikali tatu kuwa ni kutaka muungano uvunjike kwasababu ya uroho wa madaraka. Amesema, ukiondoa ccm, vyama vingine havina sura ya muungano hivyo vinataka muungano uvunjike vikidhani vitatawala kirahisi kwenye vipande vya muungano.
-Ameichana chadema live kuwa mtaji wa chama hicho ni matatizo ya watanzania. Amesema chadema hupenda kuona mambo yakienda mlama ili wapate ajenda ya kuzungumza. Alisema kuwa wamezoea kuwaandamanisha watanzania wakati watoto wao wanawaficha majumbani.
-Viongozi wa chadema wanahongwa majumba Ulaya na mabwana zao wa magharibi ili kuleta machafuko ndani ya nchi. Alisema kuwa tangu maandamano na mikutano ya chadema imeanza watanzania zaidi ya 10 wamepoteza maisha kwa kuwatoa sadaka na kusingizia jeshi la polisi.
- Alipongeza hekima na busara za Rais Kikwete kuwa pamoja na chokochoko za upinzani wanazotumwa na mabwana zao kuzifanya ili kuivuruga nchi, bado amewapiga bao. Ametolea mfano wa katiba mpya akisema anashindwa kuwaelewa wapinzani ambao waliahidi katiba mpya kwa muda wa siku mia na wengine wakasema tayari wanayo rasimu mfukoni, leo wanasema muda uliotengwa na serikali ni mdogo!.
-Alisema kuwa ccm imebaini janja ya upinzani na hasa chadema kuwa kelele zoooooote si chochote bali ni kutaka nchi ivurugike, uroho wa madaraka na rasilimali za nchi kwa kutumiwa na mabwana zao.
Alisema kuwa iwe muungano wa serikali moja, mbili, tatu ama nne, chadema ilishapigwa bao siku nyiiiiingi!
- Slaa ni mwongo kwa kusema kuwa bomba la gesi linajengwa kuelekea Ulaya.
- Chadema wanapewa fedha na wafadhili wasioitakia mema nchi hii. Amesema kama chadema imekosa fedha za kuitishia kikao cha halmashauri kuu, wamepata wapi fedha za kukodi chopper mil. 40 kwa siku?.
-Ameelezea sababu ya ccm na watanzania wengi kutaka muungano wa serikali mbili kuwa ndiyo muungano wenye maslahi ya taifa. Ametoboa ukweli wa msimamo wa vyama vya upinzani kutaka serikali tatu kuwa ni kutaka muungano uvunjike kwasababu ya uroho wa madaraka. Amesema, ukiondoa ccm, vyama vingine havina sura ya muungano hivyo vinataka muungano uvunjike vikidhani vitatawala kirahisi kwenye vipande vya muungano.
-Ameichana chadema live kuwa mtaji wa chama hicho ni matatizo ya watanzania. Amesema chadema hupenda kuona mambo yakienda mlama ili wapate ajenda ya kuzungumza. Alisema kuwa wamezoea kuwaandamanisha watanzania wakati watoto wao wanawaficha majumbani.
-Viongozi wa chadema wanahongwa majumba Ulaya na mabwana zao wa magharibi ili kuleta machafuko ndani ya nchi. Alisema kuwa tangu maandamano na mikutano ya chadema imeanza watanzania zaidi ya 10 wamepoteza maisha kwa kuwatoa sadaka na kusingizia jeshi la polisi.
- Alipongeza hekima na busara za Rais Kikwete kuwa pamoja na chokochoko za upinzani wanazotumwa na mabwana zao kuzifanya ili kuivuruga nchi, bado amewapiga bao. Ametolea mfano wa katiba mpya akisema anashindwa kuwaelewa wapinzani ambao waliahidi katiba mpya kwa muda wa siku mia na wengine wakasema tayari wanayo rasimu mfukoni, leo wanasema muda uliotengwa na serikali ni mdogo!.
-Alisema kuwa ccm imebaini janja ya upinzani na hasa chadema kuwa kelele zoooooote si chochote bali ni kutaka nchi ivurugike, uroho wa madaraka na rasilimali za nchi kwa kutumiwa na mabwana zao.
Alisema kuwa iwe muungano wa serikali moja, mbili, tatu ama nne, chadema ilishapigwa bao siku nyiiiiingi!