Mwigulu nchemba: Kirusi cha elimu tanzania

Mwigulu nchemba: Kirusi cha elimu tanzania

KasomaJr

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2010
Posts
368
Reaction score
144
Nimesikitishwa sana na kauli ya Mh. Mwigulu Nchemba, kwamba serikali inapaswa kupunguza viwango vya ufaulu vinavyoweza kuwapa fursa vijana wanaomaliza elimu ya kidato cha nne kujiunga na vyuo vya ualimu kwa gradi A. Huu binafsi naona ni upuuzi na muendelezo wa kudidimiza elimu ya nchi hii, na kwa tafsiri nyingine ni yale yale ya kuendelea kutowarendea haki wapiga kula, kwa maana kwamba kuendelea kuandaa tabaka tawaliwa.

Kudai alama za ufaulu zirudi kuwa point 28 & 29 toka 26 na zaid kama ilivyoamliwa na serikali hivi karibuni maana yake ni kwamba;
  1. Tuendelee kutumia waalimu ambao wao binafsi hawakufaul lakini ndio hao watufundishie watoto wetu huko shule za kata, na matokeo yake bila shaka wote tunayafahamu.
  2. Kuifanya serikali isione umuhimu wa kutekeleza majukumu yake ikiwa ni pamoja na kujenga miungo mbinu kufanya mazingira bora ya kupata waalimu bora na walio faulu kwa viwango stahiki, na hatimaye kupata vijana walio faulu kidato cha nne kuweza kuendelea na kidato cha sita, vyuo nk.
  3. Kuendelea kutengeneza tabaka tawala na tawaliwa, kwani watakao endelea kuumia ni wale tu watoto wetu wanaosoma shule za misingi huko vijijini ambako miundo mbinu imeendelea kuwa mibovu kwa miaka mingi sasa.
My Take:
Mwigulu umeonyesha usivyo na uchungu na hali halisi ambayo imeendelea kuwa mbaya kwa shule zetu, na kwa msingi huo uzalendo wako ni sifuri bali umedhihirisha ubinafsi ule ule mlionao viongozi wengi. Nilitarajia utumie nafasi yako kuishawishi serikali na zaidi kutumia taaluma yako kuielekeza serikali yako namna bora katika kuinua viwango vya elimu kwa taifa lako.
Personally umenisikitisha sana sana.​
 

Attachments

  • 70763_100001315017228_6999157_n.jpg
    70763_100001315017228_6999157_n.jpg
    7.2 KB · Views: 58
Kama kweli alitoa kauli hii, ni sawa na kuhamisha pesa toka mfuko wa kulia na kupeleka mfuko wa kushoto huku ukujiaminisha kuwa pesa hizo zimeongezeka. Ningempongeza kama angesisitiza kuwa, serikali iboreshe mazingira ya elimu duni iliyokithiri sasa ili kuongeza ufaulu. Kushusha kiwango cha ufaulu ni dhana potofu sana. Hivi huyu jamaa su nasikia ana First class degree, iweje atoe ushauri mbovu lama huu????
 
Sishangai maana ndio upeo wake ulipoishia hana jipya la kuwasaidia watanzania,vilaza wengi kwa system. mi sijui waliomchagua walipiga kura usiku au ?
 
huyu sijui ni mnyiramba gani?
anashusha heshima ya kina kitila mkumbo na wenzake.
hivi ukikaa ccm akili yako wanaichukua kisukule?
 
Uwezo wake wa kufikiri ndipo ulipo fikia
 
Ndio sera za elimu za ccm hizo!

Cram & Pass ndio iko sokoni muda huu. Kuboresha zaidi unapunguza kiwango cha ufaulu! That's ccm at best.

Is coincedence they've managed to keep the masses almost at the state of a zoo? Enough, get them out and start afresh.
 
Mi nadhani alikua na sababu ya kusema hivyo. Pengine mleta mada hakupata mantiki yake kusema hivyo. ngoja tumwite hapa jamvini aelezee kimaudhui alichomaanisha. It's better to hear from the horse's mouth!
 
Kama kweli alitoa kauli hii, ni sawa na kuhamisha pesa toka mfuko wa kulia na kupeleka mfuko wa kushoto huku ukujiaminisha kuwa pesa hizo zimeongezeka. Ningempongeza kama angesisitiza kuwa, serikali iboreshe mazingira ya elimu duni iliyokithiri sasa ili kuongeza ufaulu. Kushusha kiwango cha ufaulu ni dhana potofu sana. Hivi huyu jamaa su nasikia ana First class degree, iweje atoe ushauri mbovu lama huu????

Kaka, kwa mazingira ya Elimu yetu ya Bongo, Mtu kupata First Class si kwamba ni Kichwa saana. Ni rahisi kuipata na pia ni rahisi kupata Pass. Si kila aliyepata First Class ni Kichwa zaidi ya aliyepata Pass. Tuliosoma pale Mlimani tunalijua hilo. Kwa hiyo zungumzia vigezo vingine. Na kama hujui Madesa ni nini waulize waliosoma huko.
 
Mwigulu akiwa pale UDSM alikuwa anajitahidi hasa nakumbuka wakati anasoma MA(Economics) ni mtu aliyekuwa anasoma hasa,kila wakati hata weekend utamkuta Seminar room anabukua huku pembeni akiwa na mtoto mmoja mkali(aliikuwa mnene mnene hivi ana wowowo la kutosha daah jamaa alikuwa anafaidi haswaa!!, huenda ndo ilikuwa appetizer ya kusoma) SWALI ameingiaje kwenye siasa? huyu Mwigulu ni best wa Riz1 toka UDSM so baada ya Baba Riz kushika madaraka, dogo alihakikisha washkaji nao wanapata position kwenye chama na serikalini. SASA hiyo comment yake kuwa serikali ishushe viwango vya ufaulu ni lugha ya kisiasa tu na huenda aliisema akiwa ameshalewa au alikuwa anamtongoza binti fulani kwa hiyo akaropoka bila kupima kauli yake. au labda alialikwa kwenye mahafali fulani katika hali ya kutaka kupigiwa makofi akazusha kitu cha kuwavuta watu(audience) hisia
 
huyu sijui ni mnyiramba gani?
anashusha heshima ya kina kitila mkumbo na wenzake.
hivi ukikaa ccm akili yako wanaichukua kisukule?

nimekupenda ......tatizo letu nyumbani wanachagua chama ni aibu sana kwetu ..lakini kazi imeanza makosa haya hayatarudiwa
 
Kama kweli alitoa kauli hii, ni sawa na kuhamisha pesa toka mfuko wa kulia na kupeleka mfuko wa kushoto huku ukujiaminisha kuwa pesa hizo zimeongezeka. Ningempongeza kama angesisitiza kuwa, serikali iboreshe mazingira ya elimu duni iliyokithiri sasa ili kuongeza ufaulu. Kushusha kiwango cha ufaulu ni dhana potofu sana. Hivi huyu jamaa su nasikia ana First class degree, iweje atoe ushauri mbovu lama huu????
Mara nyingi watu wa hivyo wako hivyo usitarajie prof. Ana mawazo chanya maranyingi wanakuwa na mawazo ya ajabuajabu.
 
huyu sijui ni mnyiramba gani?
anashusha heshima ya kina kitila mkumbo na wenzake.
hivi ukikaa ccm akili yako wanaichukua kisukule?
Huyu ni msukuma ila baba yake alihamia huko singida irambani akiwa mdogo na kabla hajanunua jina[emoji86][emoji86][emoji86]
 
Huyu kasahau yaliyo mkumba awamu ya tano [emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91]
 
Mwigulu anaongea kishamba sana kimatamshi, kwenye tozo tafsiri mojawapo ni serikali ya hii ilikuwa inafilisika Kwa aibu, why? Mwigulu ni sharp minded anajua potential areas za kujikwamua haraka na ujinga wa kibongo, tozo za kibenki ni ujambazi ila wanajua watz ni utopolo. Acha aringe huyo ndio brain wa serikali hii, dikteta anaetangulizwa mbele Kwa kivuli Cha boss dikteta wa ufilisi wa kiuchumi wa raia. Mwigulu yeye anafanyq kazi kama ya Rashid Mfaume Kawawa Kwa msiojua historia, Rais hathubutu kumtoa huyu, bila akili, ujasili na uthubutu wa Mwigulu serikali hii itaanguka.

Mwigulu ni Opposite version ya Magufuli ambaye ni fisadi, He pushes the agenda ambayo yeye haumii nayo, Msiojua serikali Kwa Sasa haiwezi mikopo mikubwa, ulegelege wa kusimamia x,y,z za kimapato.
 
Back
Top Bottom