Nimemsikiliza Naibu Waziri wa Fedha Mh.Mwigulu Nchemba katika kipindi cha Dk.45 ITV,anayo majibu kuhusu kwanini nchi ni maskini kulinganisha na January Makamba katika kitabu chake kilichozungumzwa sana cha Maswali 40.January amepiga tu blah blah za kisiasa lakini Mwigulu speaks substance.
Kwa mfano anashangaa kwamba mashirika ya umma yanayopaswa kuchangia zaidi ya asilimia 50 ya budget,mabosi wa mashirika hayo wameyageuza kuwa mali zao binafsi na wanajipigia tu hela,pia anashangaa kuwa mtu mwenye ng'ombe 10,000 halipi kodi.Naona anazungumza vitu halisia kuliko hata Mkuu wa Kaya mwenyewe aliyewahi kusema haelewi kwanini nchi hii ni maskini.