Mwigulu Nchemba ampa shule Ado Shaibu

Mwigulu Nchemba ampa shule Ado Shaibu

Shigganza

Senior Member
Joined
May 24, 2018
Posts
160
Reaction score
412
IMG_1756.jpg
IMG_1757.jpg
 
Upuuzi mtupu, nani asiyejua kinachowapa Ushindi ccm
 
Yaani Kila nikimwangalia huyu Comrade Mwigulu nasema ..hiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii...Ahaaaaaaaaaaaa!

Huyu jama alikuwa na nafasi ya kuwa kiongozi wa mfano (kulinganisha na waliomzunguka). Lakini akadhani kwamba akifanya madudu at all cost kumridhisha namba moja atatoboa..thubutu!

Wewe endelea kuisoma namba tuu hakuna namna.
 
Mwiguluuuu, nyie zaidi ya msaada wa polisi na tume kupitia wakurugenzi nyie hamna kitu ni wepesi kuliko kilo moja ya manyoya ya kuku wa kisasa, watu wanahitajika maisha Bora ambayo hayaletwi na izo mbembwe zenu, CCM imekuwa adui na watumishi wa serikali 90%, wafanya biashara ndo wapo taabani,wakulima ndo hao wakorosho, izo Kura zenu Nani anawapa? Ukweli mwiguluuuu anaujua uchaguzi huru na was haki ccm kabla ya misa ya Kwanza kwisha watakuwa wamepoteza nusu ya nafasi za ubunge na udiwani nchi hii.
 
..ilani BORA.

..sera BORA.

..wagombea BORA.

..Je, 2020 CCM itavizidi vyama vyote ktk maeneo hayo matatu?
 
Acheni sasa kukata rufaa tuone ukweli hayo unayoyasema,mnahangaika nini?
 
MWIGULU amesha tupwa chini,sasa anajipendekeza kwa vijineno vya kinafiki ili ccm immbebe,ccm hata ikishinda mwigulu kama yeye asitegemee kurudi bungeni kwa kutegemea jimbo LA Iramba,eti sasa hivi anajiegeza Singida mjini hata huko hapiti,namshauri arudi kijijini kwao makunda akalime lile shamba alilo pora kule mbugani maisha yatasonga tu bwana mdogo.
 
Huo ndio ukweli halisi na mchungu kwa upinzani nchini,badala ya wao kwenda underground,wamejikita mjini, kwa ajili ya kusubiri matukio.
Kazi yao ni kuuza sura twitter,magazetini na kuhudhuria mahakamani,
Watakua wanatafuta mchawi wakati wachawi ni wao,wapiga kura wako nje ya dar-es-salaam,acha wajimalize kwa kupenda wenyewe
 
Mwehugulu anaimani yatamtokea kama ya Mwinyi kuwa waziri mambo ya ndani ukatoka alafu ukawa rais,anajidai kada kindakindaki lkn kiufupi hafai hata kidogo. Ubaya nivile wasiofaa wanajaribisha nao wanapata hivyo kila asofaa anaamini anaeza okota dodo jangwani.
Ushindi wa chama tawala unafahamika unavyopatikana na kila mwabudu Mungu katika kweli anaelewa hilo. Huwezi kujisifu unachama imaara wakati lowasa alitaka kuwaangusha pamoja na kashfa zoote na uzee juu. Poor mp.
 
Mwigulu acha unafiki ! Suala la Wakurugenzi kusimamia uchaguzi siyo sawa hata kwa logic ya kawaidi! PHD ya kukariri nzito sana!
Najua unajipendekeza kwa No.1 ili akufikirie tena kwenye Cabinet.Wewe ni mnafiki na mbinafsi sana !
 
Back
Top Bottom