Mwigulu na tuhuma dhidi ya CHADEMA

UGO

Member
Dec 24, 2012
14
1
Naangalia EATV, namuona Mh. Mwigulu Nchemba akiijadili CHADEMA na moja ya vitu anavyozungumza ni CHADEMA kuwa na makundi mawili huku kundi moja lenye nguvu linaongozwa na wanakaskazini ambao wanawatumia wanachama wao kama karai wakimaliza kazi Yao (CHASATA).

Lakini mheshimiwa alienda mbali zaidi akisema anamshangaa msajili wa vyama vya siasa kwa kukiacha chama hicho kiendelee na kazi huku akijua ni chama kinachopanga mauaji ya watanzania na yeye akiwa na ushahidi wa mkanda video.

Wadau ikoje
 
Nchemba ni kati ya watu waliopewa nafasi ndani ya chama cha mabubaliano ya kutaka kukichafua CHADEMA kwa mbinu ambayo inaonekana kuwa dhaifu maana waliomtuma pia dhaifu. Hivyo anahaha kujinasua asije akatemwa kabla ya wakati. Atazunguka channels zote nchini kutangazia umma kuwa CHADEMA wanapanga mauaji bila mafanikio, mwisho wake waliomtuma watamtema kama walivyomtema mkongwe WM-Wilson Mkama!! Jeshi la polisi lenye watu wa profession za upelelezi wameshindwa kubaini kuwa CHADEMA wanapanga mauaji, leo yeye hata sifa za kuwa polisi jamii hana, anakuja na polojo za kitumwa, try other options, hiyo ime-fail!!
 
Naumia sana napoona kiongozi kama huyo anapoleta porojo zake kwa kizazi hiki cha sasa,kila kitu kiko chini yao,Why wactoe hyo video au wawakamate hao viongozi wanaopanga mauaji(Yawezekana hao viongozi ni wale masalia au PM7 walitaka cheza chezo la video) MAISHA BILA CCM INAWEZEKANA
 
Uongo ni asili yake,jina analotumia si lake,mtu anaeiba hata jina ni kuogopwa,leta huo mkanda kaka tuuone. Watanzania wa leo si kama wa jana. Kwa kumtazama tu Mwigulu anaonekana ana mtindio wa ubongo,tumsamehe bure anahitaji maombi.
 
mwigulu wewe ni kilazaaa wewe ni ugolo!nawasi wasi na elimu yako ni kweli umesoma chuo wewe!
 
Hili jinga la kwanza limekosa hoja. Mbona hajadili mitandao mia ndani ya Magamba? Kweli nimeamini kuwa huyu Lameck Madelu alighushi vyeti na hana usomi wowote zaidi ya uvuvuzela. Hivi ile kashfa yake ya ugoni Igunga imeishia wapi huyu gamba uchwara?
 
Huyu mtu je hakuna anachujua kukizungumza zaidi ya cdm popote anapohojiwa yeye anachojua ni cdm.Vipi kuhusu maswala ya ufisadi umasikini na gasi hayajui hayo? Kama yeye ni mchumi si aje na sera za kiuchumi na akausaidie mkoa wake kutoka kwenye umasikini
 
Huyu bwana anakidhalilisha sana chama chake na waliomchagua.Kweli Enzi ikipita hairudi.Enzi za CCM huyu asingeweza kuwa hata Mwenyekiti wa Kitongoji.Hivi kweli unamwona Jambazi anaficha Bunduki Makaburi na Ushahidi wote Unao na ameshaua Baadhi ya Watu na ushahidi unao wa Kutosha halafu hutaki kuupeleka Polisi kwa nini tusiseme unashiriki kwenye Ujambazi huo.CCM angalien watu kama hawa ndio wanawaharibia Chama.Nafasi ya Naibu Katibu Mkuu ni Nzito.Aangalie Wenzake,CHADEMA kuna ZITO na CUF kuna MTATIRO.Hawezi kumkaribia hata Mmoja hapo.Maskini CCM.
 
Nchemba ni kati ya watu waliopewa nafasi ndani ya chama cha mabubaliano ya kutaka kukichafua CHADEMA kwa mbinu ambayo inaonekana kuwa dhaifu maana waliomtuma pia dhaifu. Hivyo anahaha kujinasua asije akatemwa kabla ya wakati. Atazunguka channels zote nchini kutangazia umma kuwa CHADEMA wanapanga mauaji bila mafanikio, mwisho wake waliomtuma watamtema kama walivyomtema mkongwe WM-Wilson Mkama!! Jeshi la polisi lenye watu wa profession za upelelezi wameshindwa kubaini kuwa CHADEMA wanapanga mauaji, leo yeye hata sifa za kuwa polisi jamii hana, anakuja na polojo za kitumwa, try other options, hiyo ime-fail!!

Kwenye mkutano wake wa Manzese hakutaja tena si alisema atataja na kutoa ushahidi ?
 
Huyu anawaogopa watu wa peoples power hadi atokwe na povu. Sisi wananchi hatudanganyiki ng'o hadi tuiondoe ccm madarakani. Kuna rafiki yangu mmoja alienda Arusha kwenye hosp fulani kwa ajili ya kufanya mambo ya electrical maintanance. Sasa alirudi hapa Dec 21 na kwa sasa ameniambia anataka kurudi maana nchi yetu ina amani sana. Ilibidi nimwambie anipe dakika 10 min nirudi nikaenda kumchukulia ile doc inayoonyesha mauaji yanayofanywa na polccm. Alipokuwa akiangalia kilichomsikitisha sana ni wale wanafunzi oops! He felt very bad for that! Alishangaa sana kama ile ilikuwa Tz alivyozidi kusoma akakuta ni Tz ndo mwisho wake wa kuamini Tz ni nchi yenye amani. Aliondoka na ile doc!
Naangalia EATV, namuona Mh. Mwigulu Nchemba akiijadili CHADEMA na moja ya vitu anavyozungumza ni CHADEMA kuwa na makundi mawili huku kundi moja lenye nguvu linaongozwa na wanakaskazini ambao wanawatumia wanachama wao kama karai wakimaliza kazi Yao (CHASATA).

Lakini mheshimiwa alienda mbali zaidi akisema anamshangaa msajili wa vyama vya siasa kwa kukiacha chama hicho kiendelee na kazi huku akijua ni chama kinachopanga mauaji ya watanzania na yeye akiwa na ushahidi wa mkanda video.

Wadau ikoje
 
Lamaeck Mkumbo Madelu aliyeiba jina la Mwigulu Nchemba, hawezi kuacha kuweweseka na kuiota CHADEMA kila wakati, anajaribu kuzuia mafuriko ya mto Rufiji kwa kuweka magogo "yatasombwa na maji ya mafuriko tu". Lameck Mkumbo Madelu "Madevu" huna jipya kaka, au umepewa Unaibu Katibu Mkuu wa Magamba ili uwe unaweweseka na CDM. kwanza kafanye suluhu na Mwigulu Nchemba kwani anatarajia kudai jina lake
 
naangalia eatv, namuona mh. Mwigulu nchemba akiijadili chadema na moja ya vitu anavyozungumza ni chadema kuwa na makundi mawili huku kundi moja lenye nguvu linaongozwa na wanakaskazini ambao wanawatumia wanachama wao kama karai wakimaliza kazi yao (chasata).

Lakini mheshimiwa alienda mbali zaidi akisema anamshangaa msajili wa vyama vya siasa kwa kukiacha chama hicho kiendelee na kazi huku akijua ni chama kinachopanga mauaji ya watanzania na yeye akiwa na ushahidi wa mkanda video.

Wadau ikoje

anashangaa nini, si amuambie tu dr. Jk ampe kitengo halafu yeye akifute hicho chama, mbona anawasakizia wenzake kazi ambayo hata yeye haiwezi. Hata kama hana qualification ya sheria amwambie tu, sio tatizo atampatia. Tena si nasikia huyo babu amemaliza muda wake? Achangamkie hiyo post, itakuwa kwake rahisi zaidi kuishughulikia cdm
 
Maswali kwa Mwigulu:
1. Mwigulu wewe ni dini gani ? Maana umetaja sana jina la BWANA kwenye uzandiki wako
2. Hivi unadhani ukifa utaikuta CCM mbinguni ?
3. Na je, unajua dhamana uliyonayo kwa mustakabali wa taifa ?
 
Wananchi wanakiamini sana chama cha CDM,lakini propaganda ambayo inafanywa na naibu katibu mkuu wa CCM Mwigulu Mchemba ikiachiwa hivi hivi ikapita kama upepo mwisho wa siku italeta mtafaruku kwa chama hiki.Ni mara ya tatu sasa namsikia akihusisha CHADEMA na mauaji ya raia wasio na hatia ilihali chama kimekaa kimya.

Mbaya zaidi kada huyu wa CCM ana thubutu kusema mbona toka azungumze hakuna aliyethubutu kukanusha kwa kuwa tu wana hofu ni mkanda upi ambao anao, ulioratibu mauaji hayo,alifika mbali zaidi kwa kusema kuwa hata yule kijana aliyetekwa na kutaka kuuwawa huko Igunga kipindi cha uchaguzi mdogo wa jimbo hilo ulikuwa ni mpango wa CHADEMA.

Kauli hii ikiachwa ikapita hivi hivi inaweza kuwa mbegu mbaya kwa mustakabali wa chama na wananchi waliojenga imani kuwa ndicho chama mkombozi wa uhuru wa kweli wa Mtanzania.Watanzania kamwe hawawezi kuvumilia propaganda hii ikiachiwa bila kukanushwa wakaendelea kukiamini chama hiki.

CHADEMA kuna kurugenzi ya sheria iliyo chini ya Tundu Lissu mbona imekaa kimya,kwakuwa ushahidi ana dai anao,tunaomba wa frame kesi na kuifikisha katika vyombo vya dola ili ushahidi huo ukithibitika haki ichukue mkondo wake.Hatuwezi kuendelea kusikiliza tuhuma ambazo mwisho wa siku unaweza kuwagawa wananchi.

Uko wapi mh.Mnyika mbona kwa hili umenyamaza kimya au halina athari kwa mustakabali wa siasa za CHADEMA?Tafakari
 
Mwanadamu mwenye heshima,iwapo hana akili, amefanana na wanyama wazururao hovyo wasiojua waendako .mheshimiwa nchemba ni kama haukupata kukulia nyumbani .kufundishwa kuwa na adabu mbele ya jamii .zaidi ya kuishi porini ukichunga mifugo .
 
Back
Top Bottom