Leo asubuhi Mwigulu katoa tuhuma nzito kwamba 1-kuna mpango wa CHADEMA kuua raia katika mikutano yao, na 2- kwamba eti Polisi wanashirikiana na CHADEMA kuua raia.
Hili la pili ni la kipuuzi kwa maana hata mwenyekiti wake anajua nani kati ya CHADEMA na CCM anayeitumia polisi, lakini la kwanza japo linaonekana pia ni la kipuuzi ukijaribu kusoma between lines lina ujumbe mzito kwa CHADEMA.
Hivi sasa ni dhahiri kabisa kuwa CCM hawana tena hoja za kuishinda CHADEMA, watasema nini juu ya wizi wa Twiga wetu? watasema nini juu ya utapeli wa DOWANS wakati kumbe hata mgao wa umeme ulikuwa unapangwa mezani? watasema nini juu ya kupanda kwa deni la taifa? watasema nini juu ya utekaji na unyama aliofanyiwa Dr Ulimboka?.
Hivi sasa wanajaribu kumtukana Dr Slaa na CHADEMA, lakini nadhani kuna wenye hekima ndani ya CCM wameona hiyo haiisaidii CCM zaidi ya kuzidi kuidhalilisha.
Yawezekana kabisa Mwigulu karopoka siri ya kuichafua CHADEMA kwa kusababisha mauaji kwenye mikutano yao, hili sio jipya walishajaribu Morogoro na Iringa lakini ushahidi uliwaumbua.
Ni kwa nini JK amekataa kuunda tume huru ya kimahakama kuchunguza mauaji haya? - jibu ni rahisi wanaujua mchezo mzima na hawawezi kujichunguza wenyewe. Kauli ya Nchemba leo ni kwamba pamoja na plan A ya kuua raia kwenye mikutano ya CHADEMA kushindwa hawajakata tamaa, wanayo plan B. Wamepanga kutumia vurugu zinazoanzishwa na kundi la masalia ndani ya CHADEMA kuleta mauaji. Wanaweza kabisa kuwadhuru au kuwaua akina ZZK na kundi lake ili kujustify kuwa akina Dr Slaa ni wauaji. Kuelekea 2015 yataweza tokea mambo mazito ya kustua. Tujipange kuyatafsiri vizuri. Alichofanya Mwigulu Nchemba leo ni kutupa tip.
Hili la pili ni la kipuuzi kwa maana hata mwenyekiti wake anajua nani kati ya CHADEMA na CCM anayeitumia polisi, lakini la kwanza japo linaonekana pia ni la kipuuzi ukijaribu kusoma between lines lina ujumbe mzito kwa CHADEMA.
Hivi sasa ni dhahiri kabisa kuwa CCM hawana tena hoja za kuishinda CHADEMA, watasema nini juu ya wizi wa Twiga wetu? watasema nini juu ya utapeli wa DOWANS wakati kumbe hata mgao wa umeme ulikuwa unapangwa mezani? watasema nini juu ya kupanda kwa deni la taifa? watasema nini juu ya utekaji na unyama aliofanyiwa Dr Ulimboka?.
Hivi sasa wanajaribu kumtukana Dr Slaa na CHADEMA, lakini nadhani kuna wenye hekima ndani ya CCM wameona hiyo haiisaidii CCM zaidi ya kuzidi kuidhalilisha.
Yawezekana kabisa Mwigulu karopoka siri ya kuichafua CHADEMA kwa kusababisha mauaji kwenye mikutano yao, hili sio jipya walishajaribu Morogoro na Iringa lakini ushahidi uliwaumbua.
Ni kwa nini JK amekataa kuunda tume huru ya kimahakama kuchunguza mauaji haya? - jibu ni rahisi wanaujua mchezo mzima na hawawezi kujichunguza wenyewe. Kauli ya Nchemba leo ni kwamba pamoja na plan A ya kuua raia kwenye mikutano ya CHADEMA kushindwa hawajakata tamaa, wanayo plan B. Wamepanga kutumia vurugu zinazoanzishwa na kundi la masalia ndani ya CHADEMA kuleta mauaji. Wanaweza kabisa kuwadhuru au kuwaua akina ZZK na kundi lake ili kujustify kuwa akina Dr Slaa ni wauaji. Kuelekea 2015 yataweza tokea mambo mazito ya kustua. Tujipange kuyatafsiri vizuri. Alichofanya Mwigulu Nchemba leo ni kutupa tip.