Pendaelli
JF-Expert Member
- Feb 13, 2014
- 12,105
- 35,136
nimeenda kanisani na furaha ile kuingia tu! namuona mpenzi wangu alieniacha kipindi kama hiki hiki mwaka jana. moyo umekufa ganzi miguu imenilegea na akili yangu imevurugika na hata kwa bahati mbaya ibada haijaenda vizuri kwangu.tokea aniache kwasababu alizoziita yeye ndugu zangu mimi hawakumpenda,lakin kilichomtoa kwangu ni mwanaume mwingine dereva wa bodaboda,pamoja nilikuwa nachukuliwa mwanamke wangu sikuridhia aondoke japokuwa kulikuwa na migogoro ya kifamilia iliosababisha tusifunge ndoa ingawa nilikaa nae miaka 3. nampenda sana namuota maranyingi sana,kwa kipindindi chote alichoondaka hajanitoka ktk mawazo yangu. na sijawai kumuona isipokuwa leo na tamani kurudiana nae ila najiuliza nianzie wapi sijui ameshaolewa? sijui anakaa kwa nani? sijui atanikubali tena? sijui baba yake ataridhia?. ninaamini jumapili ijayo nitamuona tena na natajikaza kuzungumza nae sijui itakuwaje. kabla sijakutananae 2009 nilimuomba Mungu nimuomba anipende akakubali na saiv naenda tena kwa JINA LA BWANA.