Mwenyekiti wa UVCCM Taifa apiga marufuku vijana kukaa bila kufanya kazi

kilagalila

JF-Expert Member
Nov 8, 2018
320
154
1544715016906.jpeg
picha ya mtandaoni

Mwenyekiti wa jumuiya ya umoja wa vijana Uvccm taifa Kheri james amepiga marufuku vijana kote nchini kukaa bila kufanya kazi ili kuondokana na umaskini unaotokana na uzembe

Mwenyekiti huyo amepiga marufuku hiyo mkoani Njombe alipokuwa akizungumza na vijana pamoja na wanachama wa chama cha mapinduzi CCM mjini Njombe katika ukumbi wa Turbo akitokea katika kata ya Makowo iliyopo katika halmashauri ya mji huo alikokuwa akikagua miradi mbali mbali ya maendeleo inayotekelezwa na ilani ya chama hicho.

James amesema kuwa anapata tabu anapoona vijana wanakaa bila kazi wakati wana nguvu za kufanya kazi na kuwaacha wazee vijijini wakihanagaika bila usadidizi.

“mwenye nguvu za kupasua mbao akapasue,mwenye uwezo wa kulima aklime na mwenye uwezo wa kufanya biashara akafanye biashara ni marufuku kijana kukaa tu, ukiona kijana wako amekaa tu ujue amejiandalia aibu mbele ya safari heshima ya kijana ni kazi, maisha mazuri utayapataje bila kazi tunataka vijana mkafanye kazi”alisema mwenyekiti

Aidha mwenyekiti huyo amesema kuwa halmashauri zote nchini kupitia ilani ya chama cha mapinduzi zimelekezwa kutenga asilimia nne ya makusanyo ya ndani ili kuwawezesha vijana waliotayari kufanya kazi.

“ilani ya chama imeelekeza halmashauri zote nchini kutenga asilimia nne za fedha ya makusanyo ya ndani ili kuwawezesha vijana ambao tayari wameamua kufanya kazi na sisi tupo tayari kuwawezesha vijana waliotayari, na ukikopa pesa utailejesha ile ile bila riba ukikopa kumi unaludisha kumi Raisi wetu amesema lengo la fedha hizo ni kuwawezesha wanyonge bila riba”alisema Kher james

Katika hatua nyingine mwenyekiti huyo amesema kuwa halmashauri zimeelekezwa kutenga maeneo maalumu ya kilimo na kwa ajili ya biashara kwa vijana ili kuondoa sababu kwa vijana za kuto kufanya kazi.

Mara baada ya kuzungumza na vijana pamoja na wanachama mwenyekiti amewakabidhi kadi vijana na wanachama wapya zaidi ya mia moja ambao wamejiunga na chama hicho.

mr.mtaani/mc.amiri
 
View attachment 967191picha ya mtandaoni

Mwenyekiti wa jumuiya ya umoja wa vijana Uvccm taifa Kheri james amepiga marufuku vijana kote nchini kukaa bila kufanya kazi ili kuondokana na umaskini unaotokana na uzembe

Mwenyekiti huyo amepiga marufuku hiyo mkoani Njombe alipokuwa akizungumza na vijana pamoja na wanachama wa chama cha mapinduzi CCM mjini Njombe katika ukumbi wa Turbo akitokea katika kata ya Makowo iliyopo katika halmashauri ya mji huo alikokuwa akikagua miradi mbali mbali ya maendeleo inayotekelezwa na ilani ya chama hicho.

James amesema kuwa anapata tabu anapoona vijana wanakaa bila kazi wakati wana nguvu za kufanya kazi na kuwaacha wazee vijijini wakihanagaika bila usadidizi.

“mwenye nguvu za kupasua mbao akapasue,mwenye uwezo wa kulima aklime na mwenye uwezo wa kufanya biashara akafanye biashara ni marufuku kijana kukaa tu, ukiona kijana wako amekaa tu ujue amejiandalia aibu mbele ya safari heshima ya kijana ni kazi, maisha mazuri utayapataje bila kazi tunataka vijana mkafanye kazi”alisema mwenyekiti

Aidha mwenyekiti huyo amesema kuwa halmashauri zote nchini kupitia ilani ya chama cha mapinduzi zimelekezwa kutenga asilimia nne ya makusanyo ya ndani ili kuwawezesha vijana waliotayari kufanya kazi.

“ilani ya chama imeelekeza halmashauri zote nchini kutenga asilimia nne za fedha ya makusanyo ya ndani ili kuwawezesha vijana ambao tayari wameamua kufanya kazi na sisi tupo tayari kuwawezesha vijana waliotayari, na ukikopa pesa utailejesha ile ile bila riba ukikopa kumi unaludisha kumi Raisi wetu amesema lengo la fedha hizo ni kuwawezesha wanyonge bila riba”alisema Kher james

Katika hatua nyingine mwenyekiti huyo amesema kuwa halmashauri zimeelekezwa kutenga maeneo maalumu ya kilimo na kwa ajili ya biashara kwa vijana ili kuondoa sababu kwa vijana za kuto kufanya kazi.

Mara baada ya kuzungumza na vijana pamoja na wanachama mwenyekiti amewakabidhi kadi vijana na wanachama wapya zaidi ya mia moja ambao wamejiunga na chama hicho.

mr.mtaani/mc.amiri
Tuache kulishwa habar kama watoto.Kichwa cha habari hakina mantiki. Employment opportunities are created.Vijana wa polepole ushabiki wenu wa kijuha sana
 
Na wale ambao wanatafuta kazi na hawapati anawambiaje?Kila mtu kukurupuka tu kama hawana vichwa!Linchi limekuwa hovyo kweli kweli kwa upande mmoja, kwasababu ya Strong man Politics, ambapo wengine wanafuata tu kama mitetea.

Kuku ukiwatupia chakula, jogoo akiwa miongoni mwao, huwa anawaongopea wale mitetea kuwa hicho chakula ni yeye amekitafuta, na wao huamini.
 
Mimi nilidhan amewapa ajira hao vijana huyu Kheri. Sasa anapga marufuku vijana kutofanya kazi.

Vijana wanasubr 50m
 
Huyo dogo nilikuwa namuona sana star tv sana kwenye vipindi vya mahojiano nafikiri ni mvuvi wa sato
Huyu heri kabla ya Uncle wake hajawa mkubwa kuliko wote nji hii ( in Mrema voice) alikua anafanyakazi gani?

Au ndio yale ya kama mkate umeadimika wale Keki
 
Back
Top Bottom