Mwenyekiti UVCCM, Kheri James aomba radhi kwa watu wote waliokerwa na kauli yake

Sisi wenye akili tulijua sio kosa lake ni kosa liloanzia juu toka siku aliyoropoka
Wana haja ya kuandikiwa hints kabla ujatoa hutuba,ndo shida ya kutokuwa na vyuo vya uongozi ujifunze,maana maneno ya kibaguzi utolewa na wasio na DNA za kitanzania
 
Huyu alitakiwa ashitakiwe kwa uchochezi na uhaini,cha ajabu wapinzani tu ndio huandamwa na bad enough hata wanasheria binfasi wa nchi hii wamelala tu!!!
Msajili yuko kimyaaaa na NEC ndiyo wameufyata kabisa wanamgwaya ankali.
 



"Nachukua nafasi hii kuwaomba Radhi Watanzania Wenzangu wote walio kerwa na ujumbe huo,na ninawashukuru viongozi wote wa kisiasa na kiraia walio nikosoa na kunikemea kwa maslahi mapana ya Taifa letu,ninawashukuru sana" Kheri James Mwenyekiti UVCCM Taifa

View attachment 822683

Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Kheri James ametengua kauli yake inayosema ‘CCM ndiyo inayoamua maendeleo yaje au yasije na hakuna mwananchi anayeweza kuchukua hatua yoyote dhidi ya chama hicho’.

Akimnadi mgombea wa udiwani Kata ya Bagara, mkoani Manyara, Nicodemus Tlaghasi James alisema CCM haiwezi kupeleka maendeleo kwenye maeneo yanayoongozwa na upinzani.

James alitoa kauli hiyo wiki iliyopita katika mtaa wa Mpya wilayani Babati akisema CCM haiwezi kupeleka maendeleo kwa wananchi waliochagua viongozi wa upinzani badala ya CCM.

Akizungumza leo Julai 30, 2018 na Mwananchi James amesema amefikia uamuzi huo baada ya kupokea simu za kumkemea na kumuonya juu ya kauli hiyo.

“Anayepokea sentensi hiyo, hawezi kujua mwanzo ulisema nini na mwisho ulisema nini, nimeamua kufanya kitu cha kiungwana kwamba ilimradi kilichopokelewa kwenye jamii ni kibaya, tumeamua kuomba radhi bila kujali mwanzoni na mwisho nilisema nini,” amesema James.

Chanzo: Mwananchi

Mfano halisi; Huyu mtoto anazungumza hayo, halafu mtu umelazimishwa kukatwa 15% ya mshahara kulipia Mkopo wa Elimu ya Juu, na asilimia nyingine zaidi ya 15% kodi na kubakiwa na Shs187,000/= una familia, umepanga, hujapanda cheo kwa miaka 7 hujaongezwa ongezeko la mwaka la mshahara tangu 2015, halafu huyu anazungumza kwa kiburi cha wazi kabisa. Mungu atatulipa sisi ambao leo tunasema, 'Heri wapole .....
 
Huyu kijana mwehu, fedha za maendeleo ni kodi zetu

Ccm haina fedha anasemaje upumbavu wa kiasi hicho

Tunakatwa kodi, nakutoka makusanyo ya kodi Mipango ya maendeleo hutekelezwa
 
Mfano halisi; Huyu mtoto anazungumza hayo, halafu mtu umelazimishwa kukatwa 15% ya mshahara kulipia Mkopo wa Elimu ya Juu, na asilimia nyingine zaidi ya 15% kodi na kubakiwa na Shs187,000/= una familia, umepanga, hujapanda cheo kwa miaka 7 hujaongezwa ongezeko la mwaka la mshahara tangu 2015, halafu huyu anazungumza kwa kiburi cha wazi kabisa. Mungu atatulipa sisi ambao leo tunasema, 'Heri wapole .....
Pole, Lisu alisema tukimnyamazia Mtakatifu huyu, NCHII ITAANGAMIA KAMA HAIJAANGAMIA TAYARI
 
Kaomba radhi waliokerwa, wasiokerwa vipi?

Anajua hata anaomba radhi kw akitu gani?

Ukiomba radhi waliokerwa maana yake unawaomba radhi kwa vile umewakera, hutaki kuwakera, lakini maneno yako kwa msingi hujayakana.

Kama unayakana maneno, unaomba radhi kwa kutoa maneno ambayo ni kinyume na maadili.

Sasa huyu anaomba radhi kwa kuwakera watu au kwa kutoa maneno yaliyo kinyume na maadili?

Maana kama anaomba radhi kwa kutoa maneno yaliyo kinyume na maadili, angeomba radhi kwa Watanzania wote, aliowakera na ambaohajawakera.

Maana kuna watu wengine hawajakera - wana kifua kikubwa cha kubeba maneno na hawakereki kirahisi - lakini pia hawajayapenda yale maneno.

Watu wanapewa uongozi wa kitaifa wa siasa lakini kuongea kimantiki hawajui?

Au hii ni "deliberate non-apology apology" ?
 
Last edited:
Huyu siasa sio fani yake,amelazimisha tu,
Alitakiwa awe mganga au bwana mfugo.
 
Hili jibwa linamuomba nani radhi ? Aendelee na hicho kiburi nchi si ya mama yake hii
 
Hii ni hadithi ya Nyani na Jiwe!

Katika pita pita zake baada ya kushiba mema ya nchi hata kuvimbiwa kwa kula kile ambacho hakukilima au kikipanda akaamua apumzike juu ya Jiwe (mwamba) na hata kuujambia!

Kwa kuwa mwamba ulikuwa umepata joto kutokana na shida ya jua kali, uliamua kumuunguza NYANI matako yake na hata kubabuka!

Nyani akaruka kwa kuungua kule, ...akaondoka zake huku akitoa maneno ya kashfa kwa JIWE, ..."pamoja kwamba umeniunguza, nimekujambia"

Kati ya haya nani ni Nyani na Nani ni Jiwe?

Ameshasema, ameshaleta madhara hawezi kuponyesha nafsi zilizoraruliwa kwa kauli yake!...anaenda zake huku akisema "amekemewa kwa kauli yake"
dah
 
Mtu kama huyu baadae unamkabidhi uongozi nyeti kwa Taifa hili alafu ukarajia ataamashisha wananchi kuleta umoja/muungano na maendeleo

Only in Tz
Si wanaiga, mtoto umleavyo ndio akuavyo. Mbona aliwahasa vijana wamchague mtu atakae kuwa na uwezo wa kuonana nae mara kwa mara!!
 



"Nachukua nafasi hii kuwaomba Radhi Watanzania Wenzangu wote walio kerwa na ujumbe huo,na ninawashukuru viongozi wote wa kisiasa na kiraia walio nikosoa na kunikemea kwa maslahi mapana ya Taifa letu,ninawashukuru sana" Kheri James Mwenyekiti UVCCM Taifa

View attachment 822683

Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Kheri James ametengua kauli yake inayosema ‘CCM ndiyo inayoamua maendeleo yaje au yasije na hakuna mwananchi anayeweza kuchukua hatua yoyote dhidi ya chama hicho’.

Akimnadi mgombea wa udiwani Kata ya Bagara, mkoani Manyara, Nicodemus Tlaghasi James alisema CCM haiwezi kupeleka maendeleo kwenye maeneo yanayoongozwa na upinzani.

James alitoa kauli hiyo wiki iliyopita katika mtaa wa Mpya wilayani Babati akisema CCM haiwezi kupeleka maendeleo kwa wananchi waliochagua viongozi wa upinzani badala ya CCM.

Akizungumza leo Julai 30, 2018 na Mwananchi James amesema amefikia uamuzi huo baada ya kupokea simu za kumkemea na kumuonya juu ya kauli hiyo.

“Anayepokea sentensi hiyo, hawezi kujua mwanzo ulisema nini na mwisho ulisema nini, nimeamua kufanya kitu cha kiungwana kwamba ilimradi kilichopokelewa kwenye jamii ni kibaya, tumeamua kuomba radhi bila kujali mwanzoni na mwisho nilisema nini,” amesema James.

Chanzo: Mwananchi
Hajaomba radhi kabisa. Huu ni usanii.
 
Back
Top Bottom