Mwenye update juu ya kesi ya hawa masheikh

Mwenye update juu ya kesi ya hawa masheikh

Padri aliyeuwawa walikuja wachunguzi kitoka nje walisema padri alikuwa anafanya biashara ya cocain
Vip na lile kanisa lilichomwa pale kariakoo TAG. Na lile la kule kwa Mchina ? Vip kuhusu wale akina dada wa kibongo waliokuwa wanachapwa na waya na vijana waendesha vespa. Wanaotoka kwenye mihadhara wakidai hawawataki wabongo zanzibar?
Vip kuhusu lile bomu lililo okotwa pale mwanakwerekwe KKKT..
Yote yalihusiana na cocaine.?

Nani asiyejua unga ndio biashara kubwa kwa vijana wa kizanzibar hebu nenda pale miembeni makao makuu ya club ya miembeni hakuna wauzaji pale? Kwanini wasiuwawe wale?
 
Ndugu ulikuwepo Zanzibar wakati wa vuguvugu lile la uamsho?
Ulihudhuria ile mihadhara yao iliyokuwa ikifanyika.? Kuanzia pale Darajani, lumumba, au kule mahonda.?
Unafahamu kilichokuwa kinatokea mitaa ya jang'ombe na kiembe samaki au kwa mchina baada ya mihadhara ile?
Unafahamu madhara waliyoyapata watu baada ya mihadhara ile..?

Hebu fikiri kidogo kama wasinge zuiliwa hii Nchi leo hii ingekuwa wapi? Unakumbuka wale mapadri walio uwawa kule zanzibar?
Unakumbuka zile tindikali walizomwagiwa watu kule unguja.? Tulia kidogo vuta kumbukumbu kisha waza kama hawa masheke! Wangekuwa huru leo hii zanzibar ingekuwa wapi?

Bila shaka hawa na wale wa Kibiti ni ndugu moja, na wale waliokuwa wanasema Pwani si Kenya ni hawa hawa na style zao ni zilezile.
Ndugu kukamua jipu ili kutoa usaha ndani kuna hitaji roho ngumu ni lazima anayekamuliwa alalamike sana.kwa maumivu lakini hiyo ndiyo dawa pekee.

Tunashukuru serikali kwa hatua makini walizo chukua ningekuwa na uwezo ningekutumia hapa hotuba zao, na madhara yaliyotokea kwenye jamii baada ya hotuba zile. Kama uko Unguja hadithi hizi sio ngeni kwako.
Ktk kudai haki lazima kuna madhara yatakayotokea....na ukiogopa kudhurika ukubali kupoteza haki yako"

Ktk dini imeelekezwa kudai haki na kupinga maonevu, kumbuka uamsho ilikuwa ni kikundi cha kidini"

Mihadhara waliokuwa wakifanya serekali ndo ilikuwa inatoa kibali\ kama ilivokuwa huku kipindi cha kampeni, wanatoa kibali, katikati ya mkutano poliss wanvamia na kutawanya watu.

Jaribu kuangalia video zao YouTube halafu upinge kwa hoja. (Ndo serkali ilipokwama)

Kuna njia nyingi za kudai haki, wale walipitia kwenye dini. (Ndo kada yao) ilitakiwa na makundi mengine ktk jamii yasapot

Nakuhakikishia majority ya wazanzibar wanawapenda uamsho, na ndio maana walikuwa wanafurika kwenye mihadhara yao, (ilikuwa ni mwiba kwa serkal) mpaka kesho bado wazanzbar wanachangia hela kwa ajili ya hawa masheikh.

Japo unaishukur serekali kuwaweka ndani lakini sijui ni kwa nn huoni kama ni uonevu kumuweka mtu ndani zaidi ya mika 5! Bila kumfungulia kesi!!

Unaweza kufurahia tu kwasababu yametokea upande wa Pili, (waislam)!!

Tunawajibu wa kuitetea jamii yetu thidi ya uonevu bila kujali dini kabila wala vyama"

Yaa rabii...wajaalie viongozi wetu, uwape hekima na mioyo ya imani watutendee mema wanaotuongoza'

"uwape stahamala masheikh wetu walioko mahabasu"

Mungu ibariki Tanzania yetu"
 
Jitafakari mkuu, unawatuhumu tuhuma nyingi sana! Lakini mbona hawapelekwi mahakamani kwa tuhuma hizo!? ni zaidi ya miaka mitano wako mahabusu!
Wewe unaona haki inatendeka!?

Unajua sheikh ponda kapigwa risasi Mara ngapi na polisi!? Kawekwa ndani muda mrefu sana! Unajua sababu?

Ktk mihadhara yake alipigania Mali za waislam zilizotaifishwa na serekali zirudishwe kama zilivorudishwa za wakristo. (Alikuwa mwiba)

Alivoingia makufuli aliahidi kuwarudishia bakwata Mali zao na akamtoa sheikh ponda"

Kimsingi kama walivo uamsho sheikh ponda hakuwa na hatia!

Ndugu tumeelekezwa tuwaombee viongozi wetu mungu awape hekima"
Vip na lile kanisa lilichomwa pale kariakoo TAG. Na lile la kule kwa Mchina ? Vip kuhusu wale akina dada wa kibongo waliokuwa wanachapwa na waya na vijana waendesha vespa. Wanaotoka kwenye mihadhara wakidai hawawataki wabongo zanzibar?
Vip kuhusu lile bomu lililo okotwa pale mwanakwerekwe KKKT..
Yote yalihusiana na cocaine.?

Nani asiyejua unga ndio biashara kubwa kwa vijana wa kizanzibar hebu nenda pale miembeni makao makuu ya club ya miembeni hakuna wauzaji pale? Kwanini wasiuwawe wale?
 
Ndugu ulikuwepo Zanzibar wakati wa vuguvugu lile la uamsho?
Ulihudhuria ile mihadhara yao iliyokuwa ikifanyika.? Kuanzia pale Darajani, lumumba, au kule mahonda.?
Unafahamu kilichokuwa kinatokea mitaa ya jang'ombe na kiembe samaki au kwa mchina baada ya mihadhara ile?
Unafahamu madhara waliyoyapata watu baada ya mihadhara ile..?

Hebu fikiri kidogo kama wasinge zuiliwa hii Nchi leo hii ingekuwa wapi? Unakumbuka wale mapadri walio uwawa kule zanzibar?
Unakumbuka zile tindikali walizomwagiwa watu kule unguja.? Tulia kidogo vuta kumbukumbu kisha waza kama hawa masheke! Wangekuwa huru leo hii zanzibar ingekuwa wapi?

Bila shaka hawa na wale wa Kibiti ni ndugu moja, na wale waliokuwa wanasema Pwani si Kenya ni hawa hawa na style zao ni zilezile.
Ndugu kukamua jipu ili kutoa usaha ndani kuna hitaji roho ngumu ni lazima anayekamuliwa alalamike sana.kwa maumivu lakini hiyo ndiyo dawa pekee.

Tunashukuru serikali kwa hatua makini walizo chukua ningekuwa na uwezo ningekutumia hapa hotuba zao, na madhara yaliyotokea kwenye jamii baada ya hotuba zile. Kama uko Unguja hadithi hizi sio ngeni kwako.
February 17, 2013 Padre katika Kanisa la Mtakatifu Teresa liliopo Beit al Raasi Evarist Mushi aliuliwa kwa kupigwa risasi. Kwenye Septemba hivi nakumbuka 2013 padre Joseph Magamba alimwagiwa tindikali.

Tukio la kuuliwa kwa Padre Evarist Mushi FBI waliitwa kuja kusaidia uchunguzi na michoro ilipatikana ya watu waliyofanya hilo. Ila jiulize kwa nini FBI walioondoka kimya kimya tofauti na walivyoingia na kwa nini hakuna taarifa ya wauaji walichukuliwa hatua gani? Halikadhalika kwa Padre Magembe Znz si sababu ya kudai masheikh wa UAMSHO wamehusika, matokeo ya watu kumwagiwa tindikali kwa kipindi kile yalishamiri na hata huku Bara yalikuwa yanatokea. Licha ya hivyo, Masheikh wa UAMSHO wamekamatwa 2012. Matukio yametokea 2013 wapi na wapi? Unataka kusema ni wafuasi wao? Nafikiri bado una uchache wa habari kuhusu UAMSHO.

Kwa mujibu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Masheikh wa UAMSHO wamekamatwa kwa sababu wanapinga Muungano, wanataka Zanzibar huru. Na hiki ndicho kichaka kilichowaumiza.

Binafsi si Mzanzibari ila mihadhara yao nilibahatika kuiona na kuisikia. Kikubwa ni uwasilishaji wao lugha ilikuwa ni kali lakini ndiyo ukweli wenyewe waliyokuwa wanaozungumza. Sheikh Farid na Sheikh Mselem hawa walizungumza wazi kuhusu Muungano, kwamba Muungano wa sasa hivi( kwa kipindi chao kile) hauwafai bali wao wanahitaji Serikali tatu. Na ni haki yao kama RAIA wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa taarifa tu vilevile waliongezewa kesi kwamba wanahusika na mauaji ya KIBITI. Ila fahamu sababu ya hawa Masheikh kukamatwa ni kugusa suala la Muungano tu.
 
Mi Ni mwislam lakini Uamsho style walokuja nayo ilionyesha kabisa wanna ajenda ya Siri nyuma ya pazia katika mahubiri yao, Kama ndo Mimi mtawala wa nchi ningewatamkia RIP kwao...
 
Mi Ni mwislam lakini Uamsho style walokuja nayo ilionyesha kabisa wanna ajenda ya Siri nyuma ya pazia katika mahubiri yao, Kama ndo Mimi mtawala wa nchi ningewatamkia RIP kwao...
Ajenda ipi? na sisi tuifahamu.
 
February 17, 2013 Padre katika Kanisa la Mtakatifu Teresa liliopo Beit al Raasi Evarist Mushi aliuliwa kwa kupigwa risasi. Kwenye Septemba hivi nakumbuka 2013 padre Joseph Magamba alimwagiwa tindikali.

Tukio la kuuliwa kwa Padre Evarist Mushi FBI waliitwa kuja kusaidia uchunguzi na michoro ilipatikana ya watu waliyofanya hilo. Ila jiulize kwa nini FBI walioondoka kimya kimya tofauti na walivyoingia na kwa nini hakuna taarifa ya wauaji walichukuliwa hatua gani? Halikadhalika kwa Padre Magembe Znz si sababu ya kudai masheikh wa UAMSHO wamehusika, matokeo ya watu kumwagiwa tindikali kwa kipindi kile yalishamiri na hata huku Bara yalikuwa yanatokea. Licha ya hivyo, Masheikh wa UAMSHO wamekamatwa 2012. Matukio yametokea 2013 wapi na wapi? Unataka kusema ni wafuasi wao? Nafikiri bado una uchache wa habari kuhusu UAMSHO.

Kwa mujibu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Masheikh wa UAMSHO wamekamatwa kwa sababu wanapinga Muungano, wanataka Zanzibar huru. Na hiki ndicho kichaka kilichowaumiza.

Binafsi si Mzanzibari ila mihadhara yao nilibahatika kuiona na kuisikia. Kikubwa ni uwasilishaji wao lugha ilikuwa ni kali lakini ndiyo ukweli wenyewe waliyokuwa wanaozungumza. Sheikh Farid na Sheikh Mselem hawa walizungumza wazi kuhusu Muungano, kwamba Muungano wa sasa hivi( kwa kipindi chao kile) hauwafai bali wao wanahitaji Serikali tatu. Na ni haki yao kama RAIA wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa taarifa tu vilevile waliongezewa kesi kwamba wanahusika na mauaji ya KIBITI. Ila fahamu sababu ya hawa Masheikh kukamatwa ni kugusa suala la Muungano tu.
Ndugu mbegu haioti siku hiyo huchukua muda sana na hata mavuno yake huchelewa.! Umesema vema walikamatwa 2012. Matokeo ya kukamatwa kwao ama hasira za kukamatwa kwao zikaonekana 2013.
Na mengine tunayaona kibiti na mkuranga, mpaka muunganiko wa Msumbiji.

Kwa kukusaidia tu hebu oanisha adhma ya vikundi hivi
1: Al shabaab, ya somalia maana yake bila shaka unajua. (Yaani vijana shupavu)

2: Boko haram. ! (Elimu potevu ) ya magharibi wa Nigeria..

3: Vugu Vugu la Pwani Si Kenya kule Mombasa. Kenya..

4: Jumuiya ya Uamsho..
Kule zanzibar. Tanzania.

5: Vurugu ama kikundi cha kiharifu/ Tanga, (amboni), Mwanza, na Hatmaye Mkuranga na Kibiti Bara..

6: Al shabaaab wa Msumbiji. Na madhara wanayowanyia wananchi wa Msumbiji..


Angalia adhma ya Ndani ya makundi hayo na madhara yake kwenye jamii, angalia misingi ya hoja zao kama inashabihiana ama laa.
 
Ndugu mbegu haioti siku hiyo huchukua muda sana na hata mavuno yake huchelewa.! Umesema vema walikamatwa 2012. Matokeo ya kukamatwa kwao ama hasira za kukamatwa kwao zikaonekana 2013.
Na mengine tunayaona kibiti na mkuranga, mpaka muunganiko wa Msumbiji.

Kwa kukusaidia tu hebu oanisha adhma ya vikundi hivi
1: Al shabaab, ya somalia maana yake bila shaka unajua. (Yaani vijana shupavu)

2: Boko haram. ! (Elimu potevu ) ya magharibi wa Nigeria..

3: Vugu Vugu la Pwani Si Kenya kule Mombasa. Kenya..

4: Jumuiya ya Uamsho..
Kule zanzibar. Tanzania.

5: Vurugu ama kikundi cha kiharifu/ Tanga, (amboni), Mwanza, na Hatmaye Mkuranga na Kibiti Bara..

6: Al shabaaab wa Msumbiji. Na madhara wanayowanyia wananchi wa Msumbiji..


Angalia adhma ya Ndani ya makundi hayo na madhara yake kwenye jamii, angalia misingi ya hoja zao kama inashabihiana ama laa.
Naona unatumia hisiya badala ya uhalisiiya kwenye uwasilishaji wako. Umeshawahi kuona hivyo vikundi vyengine uwasilishaji wao wa habari? Kisha wageukie UAMSHO, kisha fanya tathmini yakinifu ya kwamba vinalandana? Ulishawahi kusikia Al Shabbab mawaidha yao wanayotoa?

Haya, hebu tuwaangilie UAMSHO walichofanya. Wazanzibari waligawanyika kivyama, wao ni viongozi wa dini wakawaunganisha wakawa ni kitu kimoja ya kwamba wao ni Wazinzibari ni kitu kimoja. Na wakadai itikadi ya vyama ni kuwagawanya na kuwafanya wasahau kudai madai yao ya msingi, kwa sababu watakuwa wameparaganyika. Katika kuwaamsha huko ndiyo ilikuwa dhamira yao, ndiyo maana walijiita UAMSHO. Tusiamishe ajenda, elewa suala linalojadiliwa hapa.

Umetoa mifano ya baadhi ya vikundi kama Al Shabbab na vyengineo vyenye mfanano huo. Lakini mbona unachanganya mambo? Hivyo vikundi( kwa madai yao wao ni kusimamisha dola ya Kiislam) tukiangalia upande wa UAMSHO wao ni kuidai Zanzibar huru. Jumlisha clips zao zipo hata You tube utaona wanachokiongelea.

Kwa faida vilevile kwa kuanza na Al Shabbab, Al Qaeda, Boko Haram, ISIS na vyengine ulivyovitaja, hivyo vyote havipo katika Uislam. Scholars wa kiislam wameshawaondoa katika Uislam kwa sababu Uislam haukuruhusu kufanya jambo lolote bila ya kuwa na fact na kuliacha jambo lolote bila ya kuwa na fact. Na fact( ushahidi katika Uislam ni Hadithi na Qur'an na tunaangalia Jopo la watu waliyobobea katika elimu ya dini wametoa mustakabali gani katika jambo husika. Ukifanya kwa mapenzi yako ni wewe mwenyewe hata kama ukitamka ALLAHU AKBAR ni juu yako mwenyewe. Ndiyo maana Waislam wanaambiwa wasome dini yao ila wao wenyewe waislam ni vichwa box hawataki kusoma dini yao, wanaona utaonekana mshamba. Mwisho wa sikuwanautusi na Uislam wenyewe lakini ukiangalia tatizo ni nini? Tatizo ni elimu tu.

Licha ya hayo, hivyo vikundi ulivyoviorodhesha na UAMSHO ni magharib na mashariki. Tusihamishe ajenda tafadhali.
 
Uamsho walikuwa ni watu wa fujo tu na mashelhe zao.walikuwa wanataka kuchafua amani ya wazanzibar.

Muungano yeye unamuhusu nini?
Mbona saivi maisha yanaenda na Muungano bado upo?

Wangelinyamaza tuu yangewapata haya ya kuwa familia zao zinakosa wa kuwahudumia kutokana na baba zao kujifanya wanataka maslahi ya wazanzibar?

Hawakuona kama kuna madhara makubwa kwao yatatokea kuliko hayo madhara ya Muungano?

Ona sasa wao viongozi familia na wake zao zinavyodhalilika na kuyumba?

Mpaka wengine wanaenda kwa kadhi wapewe talaka wamechoka kukaa bila mume hali mbaya.

Haya yote waliambiwa kwamba madhara ya Muungano ni madogo kuliko yatakayowapa nyinyi hapo baadae,sasa hamjaona yamewapata haya ya kusikitisha?

Hivi mashekhe wakubwa kama akina nassor bachu hawakuona kama muungano una tatizo?

Kwa nini wasikemee munadhani?

Wale waliona kwamba maslahi ya watu kuishi kwa amni ni makubwa kuliko kuanza kuingilia serikali mambo ya Muungano.

MUAMSHO WAKATI WANATANGAZA DINI WALIKUWA MIGADHARA YAO HAKUNA ANAEPITA ILA WATU WACHACHE TU HAPO MWANZONI.

ILA WALIPOINGIA KWENYE SIASA SASA(KUZUNGUMZA MUUNGANO)NA WAZANZIBAR WAKAINGIA NA KUWA WENGI KATIKA KUNDI KUTOKANA NA WAZANZIBARI KUPENDA KWAO SIASA.

ILA UKWELI NI KWAMBA MUAMSHO WALIKUWA WAMETOKA KUTANGAZA DINI WAKAINGILIA SIASA ZA NCHI.

Familia zetu na nafsi zetu zina maslahi makubwa na thamani kuliko unyonyaji wa Muungano kwa wazanzibar na watanganyika.

Kibaya zaidi wakawa wanajionyesha kwa sura ya dini kumbe hatadini yenyewe haifundishi hivyo walivokuwa wanafanya wao,wao waliweka jazba mbele kuliko maslahi.DINI INATAKA KUANGALIA MASLAHI YA WATU NA MALI NA DAMU ZAO.

nina mengi ya kusema ila nawaombea kwa Mungu kama kukosea wameshakosea kilichobaki ni wao kujifunza kutokan na makosa Allah awape subira huko waliko na Awafanyie wepesi watoke salama.
 
Wakuu
Habari za usiku nimekaa na kuwaza sana juu ya hawa Masheikh wetu ambao tumekuwa tukiaminishwa kwamba uchunguzi wa kesi yao bado haujaisha

Je wachunguzi wa mambo
Kuna dalili yoyote ya hawa mabwana kushinda na kuchomoka kwenye kesi yao?View attachment 914348
Kiukweli hawa Masheikh wa Uamsho hawana kesi yoyote bali wamewekwa kizuizini tu , aliyewaweka anaitwa Kikwete , sababu anazijua mwenyewe , Mwenyezi Mungu ndiye ajuaye siku ya kutoka kwao .
 
Uamsho walikuwa ni watu wa fujo tu na mashelhe zao.walikuwa wanataka kuchafua amani ya wazanzibar.

Muungano yeye unamuhusu nini?
Mbona saivi maisha yanaenda na Muungano bado upo?

Wangelinyamaza tuu yangewapata haya ya kuwa familia zao zinakosa wa kuwahudumia kutokana na baba zao kujifanya wanataka maslahi ya wazanzibar?

Hawakuona kama kuna madhara makubwa kwao yatatokea kuliko hayo madhara ya Muungano?

Ona sasa wao viongozi familia na wake zao zinavyodhalilika na kuyumba?

Mpaka wengine wanaenda kwa kadhi wapewe talaka wamechoka kukaa bila mume hali mbaya.

Haya yote waliambiwa kwamba madhara ya Muungano ni madogo kuliko yatakayowapa nyinyi hapo baadae,sasa hamjaona yamewapata haya ya kusikitisha?

Hivi mashekhe wakubwa kama akina nassor bachu hawakuona kama muungano una tatizo?

Kwa nini wasikemee munadhani?

Wale waliona kwamba maslahi ya watu kuishi kwa amni ni makubwa kuliko kuanza kuingilia serikali mambo ya Muungano.

MUAMSHO WAKATI WANATANGAZA DINI WALIKUWA MIGADHARA YAO HAKUNA ANAEPITA ILA WATU WACHACHE TU HAPO MWANZONI.

ILA WALIPOINGIA KWENYE SIASA SASA(KUZUNGUMZA MUUNGANO)NA WAZANZIBAR WAKAINGIA NA KUWA WENGI KATIKA KUNDI KUTOKANA NA WAZANZIBARI KUPENDA KWAO SIASA.

ILA UKWELI NI KWAMBA MUAMSHO WALIKUWA WAMETOKA KUTANGAZA DINI WAKAINGILIA SIASA ZA NCHI.

Familia zetu na nafsi zetu zina maslahi makubwa na thamani kuliko unyonyaji wa Muungano kwa wazanzibar na watanganyika.

Kibaya zaidi wakawa wanajionyesha kwa sura ya dini kumbe hatadini yenyewe haifundishi hivyo walivokuwa wanafanya wao,wao waliweka jazba mbele kuliko maslahi.DINI INATAKA KUANGALIA MASLAHI YA WATU NA MALI NA DAMU ZAO.

nina mengi ya kusema ila nawaombea kwa Mungu kama kukosea wameshakosea kilichobaki ni wao kujifunza kutokan na makosa Allah awape subira huko waliko na Awafanyie wepesi watoke salama.
Watoke salama ili waje kuendeleza ugaidi wao mkuu...
 
Naona unatumia hisiya badala ya uhalisiiya kwenye uwasilishaji wako. Umeshawahi kuona hivyo vikundi vyengine uwasilishaji wao wa habari? Kisha wageukie UAMSHO, kisha fanya tathmini yakinifu ya kwamba vinalandana? Ulishawahi kusikia Al Shabbab mawaidha yao wanayotoa?

Haya, hebu tuwaangilie UAMSHO walichofanya. Wazanzibari waligawanyika kivyama, wao ni viongozi wa dini wakawaunganisha wakawa ni kitu kimoja ya kwamba wao ni Wazinzibari ni kitu kimoja. Na wakadai itikadi ya vyama ni kuwagawanya na kuwafanya wasahau kudai madai yao ya msingi, kwa sababu watakuwa wameparaganyika. Katika kuwaamsha huko ndiyo ilikuwa dhamira yao, ndiyo maana walijiita UAMSHO. Tusiamishe ajenda, elewa suala linalojadiliwa hapa.

Umetoa mifano ya baadhi ya vikundi kama Al Shabbab na vyengineo vyenye mfanano huo. Lakini mbona unachanganya mambo? Hivyo vikundi( kwa madai yao wao ni kusimamisha dola ya Kiislam) tukiangalia upande wa UAMSHO wao ni kuidai Zanzibar huru. Jumlisha clips zao zipo hata You tube utaona wanachokiongelea.

Kwa faida vilevile kwa kuanza na Al Shabbab, Al Qaeda, Boko Haram, ISIS na vyengine ulivyovitaja, hivyo vyote havipo katika Uislam. Scholars wa kiislam wameshawaondoa katika Uislam kwa sababu Uislam haukuruhusu kufanya jambo lolote bila ya kuwa na fact na kuliacha jambo lolote bila ya kuwa na fact. Na fact( ushahidi katika Uislam ni Hadithi na Qur'an na tunaangalia Jopo la watu waliyobobea katika elimu ya dini wametoa mustakabali gani katika jambo husika. Ukifanya kwa mapenzi yako ni wewe mwenyewe hata kama ukitamka ALLAHU AKBAR ni juu yako mwenyewe. Ndiyo maana Waislam wanaambiwa wasome dini yao ila wao wenyewe waislam ni vichwa box hawataki kusoma dini yao, wanaona utaonekana mshamba. Mwisho wa sikuwanautusi na Uislam wenyewe lakini ukiangalia tatizo ni nini? Tatizo ni elimu tu.

Licha ya hayo, hivyo vikundi ulivyoviorodhesha na UAMSHO ni magharib na mashariki. Tusihamishe ajenda tafadhali.
Ndugu yamkini huelewi ama unaelewa lakini unaelewa ukiwa ndani ya lile unalotaka kulielewa.
Nilikuwepo kwenye mihadhara nilisikiliza hoja zao na ushawishi wao. Kwa mfano maelezo ya mhadhara uliofanyika katika uwanja wa skuli ya Lumumba. Haukuwa muhadhara wa dini.
Ulikuwa wa siasa na maelezo yalikuwa yanatolewa pale bila shaka yalikuwa na uwezo wa kuamsha hisia za chuki kati ya watu wa bara na visiwani (nazungumzia Unguja na Pemba).
Ndio maana baada ya hotuba zao kilichofuatia ilikuwa ni mashambulizi kwa watu wa bara
Kuhusu itikadi za Hivi vikundi kutofautiana sidhani kama kuna tofauti Al shaabb wanadai nini ? Kama sio kujitenga kwa somalia ili maeneo yao yawe na utawala wa sharia za kiislam? Nadhani mifano iko wazi kwa maeneo ambayo walikuwa wanayamiliki ama chini ya utawala,

Kenya sio pwani walikuwa wanadai nini?
Kama sio kujitenga ili waweze kujiendesha kwa sheria zao wenyewe..? Na bila shaka kwa kutumia sharia..!

UAMSHO Zanzibar walikuwa wanataka nini katika harakati zao za kuhamasisha watu? Zanzibar huru yenye mamlaka yake kamili, bila shaka wazo likiwa lilelile kujitenga na Bara.

Kibiti na Mkuranga kama ukiwasikiliza hoja ni nini? Walipokuwa wanawaua viongozi wa CCM na kupata hifadhi misikitini walikuwa wanawaaminisha watu kuwa wao kisiasa ama viongozi wao kisiasa watakuwa bora zaidi .

Hata wale wa Msumbiji dhana yao ni hiyo hiyo, hivyo binafsi nadhani kilichowaponza viongozi wenu ni agenda waliyokuwa nayo na wala sio uonevu wa serikali.
 
Ndugu ulikuwepo Zanzibar wakati wa vuguvugu lile la uamsho?
Ulihudhuria ile mihadhara yao iliyokuwa ikifanyika.? Kuanzia pale Darajani, lumumba, au kule mahonda.?
Unafahamu kilichokuwa kinatokea mitaa ya jang'ombe na kiembe samaki au kwa mchina baada ya mihadhara ile?
Unafahamu madhara waliyoyapata watu baada ya mihadhara ile..?

Hebu fikiri kidogo kama wasinge zuiliwa hii Nchi leo hii ingekuwa wapi? Unakumbuka wale mapadri walio uwawa kule zanzibar?
Unakumbuka zile tindikali walizomwagiwa watu kule unguja.? Tulia kidogo vuta kumbukumbu kisha waza kama hawa masheke! Wangekuwa huru leo hii zanzibar ingekuwa wapi?

Bila shaka hawa na wale wa Kibiti ni ndugu moja, na wale waliokuwa wanasema Pwani si Kenya ni hawa hawa na style zao ni zilezile.
Ndugu kukamua jipu ili kutoa usaha ndani kuna hitaji roho ngumu ni lazima anayekamuliwa alalamike sana.kwa maumivu lakini hiyo ndiyo dawa pekee.

Tunashukuru serikali kwa hatua makini walizo chukua ningekuwa na uwezo ningekutumia hapa hotuba zao, na madhara yaliyotokea kwenye jamii baada ya hotuba zile. Kama uko Unguja hadithi hizi sio ngeni kwako.
....amka kifikra damu yako iwe chachu ya ukomboaz mkuu,achana na propaganda za kijinga hv kabisa issue ya kbti,kutekwa kwa watu,kupotea kwa watu yanahusiana vp na hao mashekh?
 
Hawa wengi wao sio Watanzania bali ni wahamiaji haram kutoka Somalia na Uarabuni. Kikwete aliyajua haya ndio mana akawafunga. Hawa lengolao ilikuwa kuleta uislam wa kigaidi Tanzania na walishaanza. Nibora waendelee kukaa ndani paka aliyewatuma aombe msamaa.

Wahami Harman?
 
....amka kifikra damu yako iwe chachu ya ukomboaz mkuu,achana na propaganda za kijinga hv kabisa issue ya kbti,kutekwa kwa watu,kupotea kwa watu yanahusiana vp na hao mashekh?
Siwezi kuwa sehemu ya ukombozi kwa kipuuzi.! Hivi huo ukombozi unaoongelewa hapo ni kwa faida ya nani? Ili iweje?
Siwezi kulishwa matango pori kupumbavu pumbavu kisha nikakubali eti ukombozi
How.? Its nonesense!

Kama ukombozi wenyewe ndo huo bora waendeleee kuozea huko gerezani.
 
Ndugu yamkini huelewi ama unaelewa lakini unaelewa ukiwa ndani ya lile unalotaka kulielewa.
Nilikuwepo kwenye mihadhara nilisikiliza hoja zao na ushawishi wao. Kwa mfano maelezo ya mhadhara uliofanyika katika uwanja wa skuli ya Lumumba. Haukuwa muhadhara wa dini.
Ulikuwa wa siasa na maelezo yalikuwa yanatolewa pale bila shaka yalikuwa na uwezo wa kuamsha hisia za chuki kati ya watu wa bara na visiwani (nazungumzia Unguja na Pemba).
Ndio maana baada ya hotuba zao kilichofuatia ilikuwa ni mashambulizi kwa watu wa bara
Kuhusu itikadi za Hivi vikundi kutofautiana sidhani kama kuna tofauti Al shaabb wanadai nini ? Kama sio kujitenga kwa somalia ili maeneo yao yawe na utawala wa sharia za kiislam? Nadhani mifano iko wazi kwa maeneo ambayo walikuwa wanayamiliki ama chini ya utawala,

Kenya sio pwani walikuwa wanadai nini?
Kama sio kujitenga ili waweze kujiendesha kwa sheria zao wenyewe..? Na bila shaka kwa kutumia sharia..!

UAMSHO Zanzibar walikuwa wanataka nini katika harakati zao za kuhamasisha watu? Zanzibar huru yenye mamlaka yake kamili, bila shaka wazo likiwa lilelile kujitenga na Bara.

Kibiti na Mkuranga kama ukiwasikiliza hoja ni nini? Walipokuwa wanawaua viongozi wa CCM na kupata hifadhi misikitini walikuwa wanawaaminisha watu kuwa wao kisiasa ama viongozi wao kisiasa watakuwa bora zaidi .

Hata wale wa Msumbiji dhana yao ni hiyo hiyo, hivyo binafsi nadhani kilichowaponza viongozi wenu ni agenda waliyokuwa nayo na wala sio uonevu wa serikali.
Kuhusu mhadhara wa skuli ya Lumumba kuna tatizo gani viongozi wa dini wakizungumzia siasa? Unafahamu falsafa ya dini na siasa zisichanganywe mantiki yake ni nini? Kiongozi amechaguliwa kisiasa ila akiapishwa anashika Bible au Qur'an, then unaambiwa usichanganye dini na siasa.

Kwenye bunge la katiba 2014 kulikuwa na wajumbe kutoka taasisi za kidini 13 toka bara 7 kutoka Znz, then siasa na dini zikiwa ndani ya kapu moja unaona ni najisi? Fikiri kiufanisi pasipo na mipaka brother. Kwa ujumla siasa ni mfumo uliyobeba maisha ya watu, Dini nao ni mfumo unaozunguka maisha ya watu kwa ujumla. Kuna tatizo gani viongozi wa Dini wakizungumzia dhulma inayofanyiwa jamii? Kwa vile inawagusa moja kwa moja viongozi wanaotawala? Dini na Siasa ni simbi yenye chapa pande mbili. Au unafikiri kwa nini Maskofu wanatoa waraka? Wakae kimya waone nchi inateketea? Kwa hiyo wakizungumzia mustakabali wa nchi wanazungumzia siasa? Itazame tena falsafa ya kutenganisha Dini na Siasa mantiki yake ni nini, bila shaka utafahamu mantiki ya waliyosema hivyo ni nini.

Na suala la kuvamiwa kwa Watu wa Bara ni suala la mapokeo ya wasikilizaji wenyewe na si suala la wazungumzaji. Sheikh Ponda alikuwepo pale kwenye ule mhadhara, ni Mbara yule mkazi wa Kigoma lakini Mbona hakuvamiwa?

Mkuu, Al Shabab fujo yao ni kutaka kuweka utawala wa kisharia Somalia. UAMSHO Madai yao mamlaka kamili ya Znz yameporwa na Tanzania Bara, kwa hilo wakawa wanahamasisha raia wa Znz wadai mamlaka kamili ya nchi yao. Tena wakapendekeza kuwe na Serikali 3 na hata ukiangalia kosa lililowakamatisha kwa SMZ ni madai ya kwamba wanaka kuvunja Muungano. Hata Balozi Seif kalizungumza hili hadharani lakini wewe unatoa unayoyataka mwenyewe kuhusu UAMSHO ajenda yao.

Pwani ya Kenya kutaka kujitenga walikuwa na sababu yao. Siyo hiyo ajenda unayojaribu kui' push ili kuwalisha watu dhana potofu. Madai ya wao kutaka kujitenga yalikuwa(nanukuu) " Makabila mengine yametengwa na Serikali ya Kenya tangu 1963, na kilichosalia kwa sasa ni maeneo yanayosongwa na athari ya kutengwa kuanza kujitawala" Bila shaka unafahamu Kenya ni nchi ya namna gani.

Kuhusu Musumbiji, mambo mengine hayahitaji nguvu kuyaelewa. Cabo Delgado kuna hiyo gas asilia, hao ni wahuni tu wamejipa jina la Al shabab kama huku kwetu walivyokuwa Panya road. Kwa hiyo wahuni waliona kwao ni kama fursa ndo wakafanya mambo ya ajabu.

Plus kibiti na Mkuranga unachotumia ni hisiya tu wala huna uhakika nalo na hata kama nikikuambia uhalisia wake sidhani kama utalisadiki.
 
Amefafanua vizuri Sana tatizo ni hayo matakwa kwa njia haram.
Haiwezekani kikundi cha watu kikajiona bora dhidi ya kikundi kingine kwa mwamvuli wa dini uliyoletewa na wakoloni njia pekee ya kistaarabu ni kutenganishwa na jamii. Mungu huyu ni wetu sote sasa inakuwaje uwauwe wengine eti kwasababu siyo wa dini yako? Ajabu unawaita makafiri lakini Unapanda Ndege zao, ukiishiwa damu unaongezewa damu zao, unatibiwa na madaktari wao!!Naamini hata Mungu hapendi kabisa tafuteni njia muafaka ya kupata mnachoona mmekikosa
 
Back
Top Bottom