chumachakavu
Member
- Oct 1, 2017
- 53
- 62
Habari ndg zangu,naomba yeyote mwenye ufahamu wa kampuni ijulikanayo kwa jina tajwa hapo juu anijuze,maana kuna mtoto wa dada yangu amejiunga na hiyo kampuni lakini imekuwa ngumu kupata taarifa zake baada ya kufika Dar wa Salaam ambapo ndiko kwenye hiyo kampuni hana uhuru wa simu yake,kila ukipiga simu anapokea mtu mwingine na akipelekewa simu haongei kwa uhuru, kila swali ninalomuuliza anasema nitakwambia baadae, na hiyo Baadae ukipiga hapokei, hata ukipiga mara mia moja hapokei, napata mashaka na hiyo kampuni, mpaka sasa amelipa ada ya mafunzo sh 2,000,000 kama ada ya mafunzo naambiwa bado milioni moja kukamilisha hiyo ada yao ya mafunzo,baada ya mafunzo sijajua amehaidi nini, yaani ni giza mwanzo mwisho.napata wasiwasi isiwe ni ndugu yake Qnet.
Kiukweli sijapata taarifa yeyote ya kitu gani wanafundishwa kwenye hiyo kampuni kiasi cha kulipa pesa nyingi hivyo,plz mwenye ufahamu juu la hii kampuni atujuze kwa faida yangu na wengine.
Kiukweli sijapata taarifa yeyote ya kitu gani wanafundishwa kwenye hiyo kampuni kiasi cha kulipa pesa nyingi hivyo,plz mwenye ufahamu juu la hii kampuni atujuze kwa faida yangu na wengine.