Mwenye uelewa wa Kifaa hiki Tafadhali

Farolito

JF-Expert Member
Sep 10, 2018
11,634
26,373
Wakuu Salaam!
Njia za Kisasa za uzazi wa mpango ambazo zimekua zikitumika hasa nchi za kiafrika pamoja na kuwa na msaada lakini zimekua zikisababisha madhara makubwa ya Kiafya lakini Mara nyingi matangazo ya njia hizi yamekua yakisema ni maudhi madogo madogo tu.

Nimebahatika kusoma kitabu cha Shirika la Pro-life Tanzania ambacho kimeelezea njia zote na madhara yake kwa kila njia kiukweli madhara ni makubwa sana ikiwemo saratani nk.

Katika kupita mitandaoni nilibahatika kukutana na kifaa hiki kinachoitwa LADY-COMP
Hiki ni kifaa ambacho kinatumika kama mbadala wa njia za kisasa za uzazi wa mpango kwani hakiingizi kemikali wala kifaa chochote ndani ya mwili wa binadamu na hakina madhara yoyote .

Ni kifaa ambacho kina mfumo wa computer kwa ajili ya kupima na kuhifadhi taarifa za hali ya uzazi(Fertility) ili kukuonesha Siku ambazo ni salama na sio salama katika mzunguko wa mwanamke.

Kwa mujibu wa maelezo jinsi kinavyofanya Nazi ni rahisi sana kwani kinachotakiwa ni mwanamke kupima joto lake kila Siku asubuhi(mdomoni)na kuingiza kwenye kifaa hicho zoezi ambalo linachukua sekunde 30 tu,pia kama upo kwenye hedhi utatakiwa kuingiza taarifa hio na hapo kitakua kinaweza kuhifadhi na kukupa taarifa za Siku salama za zisizo salama kwa uhakika kwa asilimia 99.3 kwa kuonesha taa nyekundu, njano na kijani.

Najua humu kuna madaktari na wataaam mbalimbali lakini pia wapo watu pengine wameshakiona au kutumia kifaa hiki ,Je ni salama na kinafanya kazi kama inavyoelezwa?

Kifaa hiki kimeanza kutengenezwa nchini Ujerumani tangu mwaka 1986 ni kinatumika zaidi ya nchi 35 na wanasema ukinunua hakuna gharama zingine za ziada na kinauwezo wa kudumu zaidi ya miaka 10 na bei yake nimejaribu kuangalia inaanzia $375.

Karibuni tupeane uzoefu pengine inaweza ikawa msaada kwetu kukwepa madhara zaidi.

NB.kifaa hiki hakizuii magonjwa ya Zinaa.

Lady Comp Ovulation Calculator - Ovulation Calculation safe & easy
IMG_20190304_123256.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 

Attachments

  • lady-comp2.jpg__700x700_q85_crop_subject_location-1640%2C2995_upscale.jpeg
    lady-comp2.jpg__700x700_q85_crop_subject_location-1640%2C2995_upscale.jpeg
    17.4 KB · Views: 46
  • Screenshot_20190301-212332.jpeg
    Screenshot_20190301-212332.jpeg
    48.7 KB · Views: 56
Aisee, Technology imeenda mbali sanaa, ngoja tusubiri wajuzi

Daima toa bila kukumbuka na Pokea bila kusahau
 
OK mkuu nashukuru sana,vipi kinafanya kazi kama kinavyotegemewa?hakijawahi kuwaangusha?tupe uzoefu kidogo na umekua ukitumia kwa mda gani

Yes hii device ipo vizuri.

Kifupi inatoa majibu sahihi kwahiyo hakijawahi kutuangusha.

Amekuwa akitumia muda sasa (more than two years now)
 
Asante mkuu,ngoja nijipange ninakihitaji nitakutafuta unisaidie,vp naweza kupata kwa bei gani?
Yes hii device ipo vizuri.

Kifupi inatoa majibu sahihi kwahiyo hakijawahi kutuangusha.

Amekuwa akitumia muda sasa (more than two years now)
 
Bei ni $420

Hii ni Pearly

Ni yakisasa, ndogo na pia inatumia battery zinakaa for years.

Pia hiyo ni gharama hadi unapata hapa Tz.
 
Hiki kifaa ni moja kati ya best invention kuwasaidia wanawake kupata njia salama ya kupanga au kuzuia ujauzito.

Na usuri wake ni rahisi sana kutumia.

Ndani ya hiki kifaa kuna program iliyoundwa inayowezesha kufahamu iwapo mwanamke leo yupo katika siku salama au siku za hatari
 
Kutumia ni rahisi tu.

Asubuhi ukiamka una washa halafu unaingiza hiko kimkono chake mdomoni kwa sekunde 30 hivi.

Kina sensor (thermometer) ina-record taarifa kupitia joto la mwanamke.

Baada ya hapo itawaka taa nyekundu (upo siku za hatari)

Njano (hii inatokea siku za mwanzo wakati unaanza kutumia kwasababu bado taarifa zako zinakusanywa kwaajili ya matokea ya uhakika zaidi)

Kijani (upo siku salama)
 
Hiki kifaa ni moja kati ya best invention kuwasaidia wanawake kupata njia salama ya kupanga au kuzuia ujauzito.

Na usuri wake ni rahisi sana kutumia.

Ndani ya hiki kifaa kuna program iliyoundwa inayowezesha kufahamu iwapo mwanamke leo yupo katika siku salama au siku za hatari
Nilipokiona mtandaoni nilihitaji nipate mtu ambaye tayari amekitumia kama wewe,nafarijika kwamba kipo vizuri na ni natural,maana athari za njia za kisasa mkuu ni nyingi sana,wenzetu wanazikwepa kwa teknolojia,
Asante kwa mchango wako,nikiwa tayari nitakucheki.
 
Nilipokiona mtandaoni nilihitaji nipate mtu ambaye tayari amekitumia kama wewe,nafarijika kwamba kipo vizuri na ni natural,maana athari za njia za kisasa mkuu ni nyingi sana,wenzetu wanazikwepa kwa teknolojia,
Asante kwa mchango wako,nikiwa tayari nitakucheki.

Ndiyo.

Ni kifaa kizuri.

Nadhani wakina dada wenye kipato kizuri na wenye kuchukizwa na njia artificial za kupanga uzazi wanaweza wakapendezwa na hii device.

Karibu ukiwa tayari tuwasiliane.
 
Back
Top Bottom